Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w15 11/15 kur. 14-15
  • Thamini Ukarimu wa Yehova

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Thamini Ukarimu wa Yehova
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2015
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • MFANO BORA WA UKARIMU
  • “Kazi Ni Kubwa”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2016
  • Ziada Yao Ilijazia Upungufu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2012
  • Yehova Huwabariki Sana Wenye Nia ya Kutoa
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2014
  • Jinsi Tunavyoweza Kuwasaidia Wenye Uhitaji
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2013
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2015
w15 11/15 kur. 14-15
Mwanamke akitoa mchango kwa kutumia kadi ya benki

Thamini Ukarimu wa Yehova

YEHOVA ni Mungu mkarimu. (Yak. 1:17) Tunaona wazi ukarimu wa Yehova tunapotazama uumbaji wake, kuanzia anga lenye nyota nyingi hadi mimea inayofunika dunia.—Zab. 65:12, 13; 147:7, 8; 148:3, 4.

Mtunga zaburi alithamini sana uumbaji wa Yehova hivi kwamba alichochewa kutunga wimbo ili kumsifu. Soma Zaburi ya 104, ili uone ikiwa una maoni kama yake. Alisema hivi: “Nitamwimbia Yehova katika maisha yangu yote; nitampigia Mungu wangu muziki maadamu nipo.” (Zab. 104:33) Je, ungependa kufanya vivyo hivyo?

MFANO BORA WA UKARIMU

Yehova anataka tuige ukarimu wake. Anatusaidia pia kuelewa umuhimu wa kuwa wakarimu. Alimwongoza mtume Paulo kuandika hivi: “Uwape maagizo wale walio matajiri katika mfumo wa mambo wa sasa wasitake makuu, na waweke tumaini lao, si katika utajiri usio hakika, bali katika Mungu, ambaye hutupa sisi vitu vyote kwa wingi ili tuvifurahie; wafanye mema, wawe matajiri katika matendo mazuri, wawe wakarimu, tayari kushiriki, wakijiwekea wenyewe kwa usalama hazina ya msingi mzuri kwa ajili ya wakati ujao, ili waushike imara uzima ulio wa kweli.”—1 Tim. 6:17-19.

Mtume Paulo alipowaandikia Wakorintho barua yake ya pili, alikazia mtazamo unaofaa kuhusu kutoa. Alisema hivi: “Kila mmoja na afanye kama alivyoazimia moyoni mwake, si kwa kutopenda wala kwa kulazimishwa, kwa maana Mungu humpenda mtoaji mchangamfu.” (2 Kor. 9:7) Kisha, Paulo alieleza faida za ukarimu; wapokeaji hunufaika kwa kuwa uhitaji wao unatoshelezwa, na watoaji hufaidika kwa kupokea baraka za kiroho.—2 Kor. 9:11-14.

Paulo alimalizia sehemu ya barua yake kwa kueleza jambo la pekee linalothibitisha kwamba Mungu ni mkarimu sana. Alisema hivi: “Mungu apewe shukrani kwa ajili ya zawadi yake ya bure isiyoelezeka.” (2 Kor. 9:15) Ni wazi kwamba zawadi ya Yehova inahusisha wema wote ambao amewafanyia wanadamu kupitia Yesu Kristo. Zawadi hiyo ni ya pekee sana hivi kwamba hatuwezi kufafanua kikamili thamani yake.

Tunaweza kuonyeshaje kwamba tunathamini mambo yote ambayo Yehova na Mwana wake wametufanyia na yale watakayotufanyia? Njia moja ni kuwa wakarimu kwa kutoa wakati, nguvu, na mali zetu ili kuendeleza masilahi ya ibada safi, iwe michango yetu ni midogo au mikubwa.—1 Nya. 22:14; 29:3-5; Luka 21:1-4.

Jinsi Ambavyo Wengine Hutoa Michango Kwa Ajili Ya Kazi Ya Ulimwenguni Pote

Kama ilivyokuwa katika siku za mtume Paulo, watu wengi leo ‘huweka kando kitu fulani,’ au kiasi fulani cha pesa ambacho wanatumbukiza katika masanduku ya michango yaliyoandikwa “Kazi ya Ulimwenguni Pote.” (1 Kor. 16:2) Kila mwezi, makutaniko hutuma michango hiyo katika ofisi ya tawi ya Mashahidi wa Yehova inayosimamia kazi katika nchi yao. Unaweza pia kutuma michango yako moja kwa moja katika shirika la kisheria linalotumiwa na Mashahidi wa Yehova nchini mwenu. Ili kujua shirika la kisheria linalotumiwa na Mashahidi wa Yehova katika nchi yenu, tafadhali wasiliana na ofisi ya tawi. Anwani za ofisi za tawi zinapatikana katika tovuti ya www.jw.org/sw. Michango ifuatayo inaweza kutumwa moja kwa moja:

MICHANGO YA MOJA KWA MOJA

  • Michango inayotumwa kupitia mfumo wa elektroniki au kadi za benki. Ofisi nyingine za tawi zinatumia pia tovuti ya jw.org au tovuti nyingine inayopendekezwa kupokea michango.

  • Michango ya pesa taslimu, vito, au mali yoyote ya kibinafsi iliyo na thamani. Ambatanisha barua inayoonyesha kwamba pesa taslimu au mali hizo ni michango ya moja kwa moja.

MPANGO WA MICHANGO YENYE MASHARTI

  • Hii ni michango ya pesa taslimu zinazotolewa kwa masharti kwamba zinaweza kurudishwa kwa aliyechangia akizihitaji.

  • Ambatanisha barua inayoonyesha kwamba ni mchango wenye masharti.

UTOAJI ULIOPANGWA

Mbali na zawadi za pesa na mali zenye thamani, kuna njia nyingine za kutoa michango kwa ajili ya kazi ya Ufalme ya ulimwenguni pote. Njia hizo zimeorodheshwa hapa chini. Haidhuru ni njia gani ambayo ungependa kutumia, tafadhali wasiliana kwanza na ofisi ya tawi inayosimamia kazi nchini mwenu ili kujua ni njia gani zinazotumika katika nchi yenu. Kwa kuwa matakwa na sheria za kodi zinatofautiana, ni muhimu kuwasiliana na washauri wa mambo ya kisheria na kodi kabla ya kuchagua njia bora ya kutoa mchango.

Bima: Mchango huu unatolewa kwa kutaja kihususa shirika la Mashahidi wa Yehova kuwa ndilo litakalofaidika na bima ya maisha au malipo ya uzeeni au ya kustaafu.

Akaunti za Benki: Akaunti za benki, hati za amana, au akiba za pesa za kustaafu zinaweza kuwekwa zikiwa amana, au baada ya mtu kufa, zinaweza kulipwa kwa shirika linalotumiwa na Mashahidi wa Yehova, kulingana na matakwa ya benki za kwenu.

Hisa na Dhamana: Hisa na dhamana zinaweza kuchangwa kwa shirika la Mashahidi wa Yehova zikiwa zawadi ya moja kwa moja, au mtoaji anaweza kuandika kwamba shirika hilo lipewe hisa na dhamana zake baada ya yeye kufa.

Ardhi na Nyumba: Ardhi au nyumba zinaweza kutolewa kama mchango kwa shirika la Mashahidi wa Yehova, zikiwa zawadi ya moja kwa moja au zawadi yenye masharti, yaani, mtoaji anaweza kuendelea kuishi humo hadi kifo chake.

Malipo ya Mwaka: Pesa au amana zinazotolewa zikiwa mchango kwa shirika la Mashahidi wa Yehova chini ya makubaliano kwamba anayetoa mchango huo atapata kiasi fulani cha pesa kila mwaka katika maisha yake yote. Huenda mtoaji akapunguziwa kodi ya serikali katika mwaka ambao mpango huo unaanzishwa.

Wosia na Amana: Mali au pesa zinaweza kuachiwa shirika la Mashahidi wa Yehova kama urithi kwa njia ya wosia halali, au linaweza kutajwa kuwa shirika ambalo litafaidika na mkataba wa amana. Chini ya mpango huu, kodi fulani zinaweza kupunguzwa.

Maneno “utoaji uliopangwa” yanaonyesha kwamba mtu anapaswa kufanya mipango hususa ili atoe michango ya aina hiyo. Broshua ya Kiingereza na Kihispania yenye kichwa Charitable Planning to Benefit Kingdom Service Worldwide imetayarishwa ili kuwasaidia watu wanaotaka kutegemeza kazi inayofanywa na Mashahidi wa Yehova ulimwenguni pote. Broshua hiyo iliandikwa ili kueleza njia mbalimbali za kuchangia sasa au wakati ujao, kama vile urithi mtu anapokufa. Huenda habari fulani katika broshua hiyo hazitumiki katika nchi yenu kwa sababu ya sheria za kodi au sheria nyingine. Kwa hiyo, baada ya kusoma broshua hiyo, zungumza na washauri wa mambo ya kisheria au kodi. Kwa kutumia njia kama hizo za kutoa michango, watu wengi wametegemeza shughuli zetu za kidini na kazi yetu ya kutoa misaada ulimwenguni pote, nao wamepunguziwa kodi. Ikiwa broshua hiyo inapatikana katika nchi yenu, unaweza kuomba nakala kutoka kwa mwandishi wa kutaniko lenu.

Kwa habari zaidi, unaweza kuwasiliana na ofisi ya tawi.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki