Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w14 8/1 uku. 5
  • Mungu Anakuelewa

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Mungu Anakuelewa
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2014
  • Habari Zinazolingana
  • Yehova Atujua Vema!
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1990
  • Je! Kweli Mungu Anakujua?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1993
  • Je, Mungu Anakuelewa?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Toleo la Watu wote)—2018
  • Tumeumbwa kwa Njia ya Ajabu
    Daftari la Mkutano wa Huduma na Maisha Yetu ya Kikristo (2016)
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2014
w14 8/1 uku. 5

HABARI KUU | JE, MUNGU ANAKUJALI?

Mungu Anakuelewa

“Ee Yehova, umenichunguza kabisa, nawe unanijua.”—ZABURI 139:1.

Uzi wa DNA na kiini-tete

“Macho yako yalikiona kiini-tete changu.” —ZABURI 139:16

KWA NINI WENGINE HAWAAMINI? Watu wengi wanahisi kwamba Mungu huwaona wanadamu kuwa wenye dhambi—wasio safi na wasiofaa. Kendra, aliyepatwa na ugonjwa wa kushuka moyo, alijihisi mwenye hatia sana kwa sababu alidhani hangeweza kufuata viwango vya Mungu kikamili. Kwa hiyo, anasema: “Niliacha kusali.”

BIBLIA INAFUNDISHA NINI? Yehova haangalii tu dhambi zako bali pia anaelewa vizuri kabisa utu wako. Biblia inasema: “Analijua vema umbo letu. Akikumbuka kwamba sisi ni mavumbi.” Zaidi ya hayo, hashughuliki nasi “kulingana na makosa yetu” bali anatusamehe kwa rehema tunapotubu.—Zaburi 103:10, 14.

Mfikirie Daudi, mfalme wa Israeli aliyetajwa kwenye makala ya kwanza ya mfululizo huu. Alipokuwa akisali kwa Mungu alisema hivi: “Macho yako yalikiona kiini-tete changu, na katika kitabu chako sehemu zake zote zilikuwa zimeandikwa . . . Unichunguze kabisa, Ee Mungu, uujue moyo wangu.” (Zaburi 139:16, 23) Naam, Daudi alikuwa na hakika kwamba ingawa alitenda dhambi—hata dhambi nzito—Yehova angeweza kutambua moyo wake wenye toba.

Yehova anakuelewa vizuri zaidi kuliko binadamu yeyote yule. Biblia inasema: “Mwanadamu huona kile kinachoonekana kwa macho, lakini Yehova huona jinsi moyo ulivyo.” (1 Samweli 16:7) Mungu anakujua kwa undani, yaani, chembe za urithi, malezi, mazingira, na mambo yote yanayochangia utu wako. Mungu anaona na kuthamini jitihada zako za kuwa mtu mwema, hata ingawa unakosea.

Hata hivyo, Mungu hutumiaje mambo anayojua kukuhusu ili kukusaidia?

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki