Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w15 2/1 uku. 3
  • Kazi Ngumu​—Je, Imepitwa na Wakati?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Kazi Ngumu​—Je, Imepitwa na Wakati?
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2015
  • Habari Zinazolingana
  • Jinsi ya Kufurahia Kazi Ngumu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2015
  • Ona Mema kwa Ajili ya Kazi Yako Ngumu
    “Jitunzeni Katika Upendo wa Mungu”
  • Furahia Kazi Yako
    Jinsi ya Kudumu Katika Upendo wa Mungu
  • Ona Mema kwa Ajili ya Kazi Yako Yote Ngumu
    Daftari la Mkutano wa Huduma na Maisha Yetu ya Kikristo (2016)
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2015
w15 2/1 uku. 3
Mwanamume akiwa amekata tamaa wakati wafanyakazi wenzake wakiendelea na kazi

HABARI KUU | JINSI YA KUFURAHIA KAZI NGUMU

Kazi Ngumu—Je, Imepitwa na Wakati?

Alex anahema anapojitahidi kunyanyua boksi na kupakia kwenye lori la kampuni. Anajiuliza hivi: ‘Kwa nini naendelea kufanya kazi hii ngumu? Je, kuna siku nitafanikiwa? Maisha yangu yangekuwa mazuri kama nisingelazimika kufanya kazi!’

Kama Alex, watu wengi leo hawafurahii kufanya kazi ngumu. Fundi wa magari aitwaye Aaron anasema hivi: “Watu wengi wanafikiri kwamba hawastahili kufanya kazi za hali ya chini. Wanafikiri kwamba wanafanya kazi ngumu kwa muda tu wakisubiri kupata kazi bora zaidi.”

Kwa nini watu wengi wanahisi kwamba hawastahili kufanya kazi ngumu? Huenda maoni yao yameathiriwa na vyombo vya habari, ambavyo mara nyingi hueleza kwamba watu wenye mafanikio ni wale wanaoishi maisha ya starehe, bila kazi ngumu. Fundi wa ujenzi aitwaye Matthew anasema hivi: “Watu wanadhani kwamba unapofanya kazi ngumu ili kupata riziki huna mafanikio.” Shane ambaye anafanya kazi ya usafi na utunzaji wa majengo anasema hivi: “Watu hawataki tena kufanya kazi ya kibarua ili kulipwa ujira wa siku moja tu.”

Kwa upande mwingine, watu wengi waliofanikiwa hufurahia kufanya kazi ngumu. Daniel, fundi wa ujenzi mwenye umri wa miaka 25 anasema hivi: “Kazi ngumu ni nzuri sana hasa inapomsaidia mtu kutimiza malengo yake.” Andre, mwenye umri wa miaka 23 anakubaliana naye. Anasema hivi: “Naamini kwamba furaha na kuridhika hutegemea kazi. Mtu asipofanya kazi hawezi kuwa na furaha, na mwishowe atakata tamaa!”

Hata hivyo, watu kama Daniel na Andre wamewezaje kuwa na mtazamo mzuri kuhusu kazi ngumu? Kwa ufupi, wamefuata ushauri wa Biblia kuhusu kazi. Badala ya kuwavunja moyo watu wasifanye kazi ngumu, Biblia inawatia moyo wafanye kazi kwa bidii na uvumilivu. Hata hivyo, Biblia haituambii tu kwamba tunapaswa kufanya kazi, bali pia inatueleza jinsi ya kufurahia kazi zetu.

Ni kanuni zipi za Biblia zinazoweza kukusaidia ufurahie kazi yako? Tunakualika uchunguze baadhi ya kanuni hizo katika makala inayofuata.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki