Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w15 6/1 kur. 6-7
  • Sayansi Ina Mipaka

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Sayansi Ina Mipaka
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2015
  • Habari Zinazolingana
  • Jinsi Sayansi Inavyoathiri Maisha Yako
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2015
  • Chanzo cha Ulimwengu na Uhai Ni Nini?
    Amkeni!—2002
  • Kupatanisha Sayansi na Dini
    Amkeni!—2002
  • Waweza Kuitumaini Sayansi Kadiri Gani?
    Amkeni!—1998
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2015
w15 6/1 kur. 6-7
Mwanasayansi akiwa katika maabara

HABARI KUU JE, SAYANSI | IMECHUKUA NAFASI YA BIBLIA?

Sayansi ina Mipaka

Katika miaka ya hivi karibuni, vitabu vingi vinavyoeleza maoni ya watu wasioamini kuwapo kwa Mungu vimechapishwa. Vitabu hivyo vimewavutia watu wengi na vimechochea mazungumzo na mijadala mikubwa. Kuhusiana na hilo, mwanasayansi wa mfumo wa neva, David Eagleman aliandika hivi: “Baadhi ya wasomaji wanaamini kwamba wanasayansi wanajua kila kitu.” Kisha akaongezea hivi: “Mwanasayansi bora hukubali kujifunza mambo mapya, na kufanya hivyo kunamwezesha kugundua mambo mapya.”

Mtaalamu wa nyota akitumia darubini

Tangu zamani, wanasayansi stadi wamefanya ugunduzi wenye kutokeza walipokuwa wakitafuta majibu ya maswali magumu kuhusu uumbaji. Hata hivyo, baadhi yao wamefanya makosa makubwa sana katika jitihada hizo. Isaac Newton alikuwa mmoja kati ya wanasayansi mashuhuri sana. Alieleza jinsi ambavyo nguvu ya uvutano inavyoongoza sayari, nyota, na makundi ya nyota katika ulimwengu. Pia, alianzisha kanuni ya hesabu ambayo hutumiwa kutengeneza kompyuta, safari za angani na fizikia ya nyuklia. Hata hivyo, Newton alifuatilia alkemia, sayansi ya uwongo ambayo hutumia unajimu na uchawi kujaribu kugeuza metali ya kawaida kuwa dhahabu.

Zaidi ya miaka 1,500 kabla ya Newton, mtaalamu wa nyota Mgiriki Ptolemy alichunguza mbingu kwa kutumia macho tu. Ptolemy alifuatilia sayari zilizopita katika anga la usiku na alikuwa stadi katika kuchora ramani. Lakini aliamini kwamba dunia ni kitovu cha vitu vyote. Mwanasayansi Carl Sagan aliandika hivi kuhusu Ptolemy: “Maoni yake kuhusu dunia kuwa ndio kitovu cha ulimwengu yaliyokubaliwa kwa miaka 1,500 ni uthibitisho wa kwamba hata mtu awe na akili kadiri gani bado anaweza kuwa amekosea.”

Mwanasayansi akisoma Biblia

Leo pia, wanasayansi wanakabili changamoto zilezile. Je, wataweza kuuelewa ulimwengu kikamili? Ingawa ni jambo linalofaa kutambua maendeleo ambayo sayansi imefanya na faida ambazo imetuletea, ni muhimu kukumbuka mipaka yake. Mwanafizikia Paul Davies alisema hivi: “Haiwezekani kupata ufafanuzi kamili unaoeleweka na unaopatana katika kila hali kuhusu ulimwengu wetu.” Maneno hayo yanaeleza ukweli huu usiopingika: Wanadamu hawezi kuelewa kikamili uumbaji. Hivyo, wengine wanapodai kwamba sayansi inaweza kufafanua vizuri chanzo cha kila kitu kilichopo, ni vizuri kuchunguza madai hayo kwa usawaziko.

Ni wazi kwamba Biblia inatimiza uhitaji wetu katika njia ambazo sayansi haiwezi

Biblia hueleza maajabu ya uumbaji kwa maneno haya: “Tazama! Hizo ndizo kingo za njia zake [Mungu], nao ni mnong’ono ulioje wa jambo lililosikiwa juu yake!” (Ayubu 26:14) Kuna hazina kubwa ya ujuzi ambayo inazidi uwezo wa mwanadamu kuelewa. Kwa kweli, maneno ambayo mtume Paulo aliandika miaka 2,000 hivi iliyopita, bado ni ya kweli kabisa: “Lo! Jinsi kilivyo kina cha utajiri wa Mungu na hekima na ujuzi! Jinsi hukumu zake zisivyochunguzika na njia zake zisivyotafutika!”—Waroma 11:33.

Mwongozo Ambao Sayansi Haiwezi Kutoa

Ingawa sayansi hutupatia ujuzi kuhusu uumbaji, Biblia ina kanuni na mwongozo ambao hutusaidia kuwa na uhusiano wenye amani na wengine, kuishi maisha yenye furaha na yenye kuridhisha. Fikiria mifano ifuatayo.

  • Mkono unaonyesha alama ya kusimama

    Kuzuia Uhalifu

    Heshimu uhai

    “Usiue.”​—Kutoka 20:13.

    “Kila mtu anayemchukia ndugu yake ni muuaji.”​—1 Yohana 3:15.

    Fanya amani na kuidumisha

    “Geuka kutoka katika yaliyo mabaya, na kufanya yaliyo mema; utafute amani, na kuifuatia.”​—Zaburi 34:14.

    “Zaidi ya hayo, mbegu ya tunda la uadilifu hupandwa chini ya hali zenye amani kwa wale wanaofanya amani.”​—Yakobo 3:18.

    Epuka jeuri

    “Yehova humchunguza mwadilifu na pia mwovu, na mtu yeyote anayependa jeuri nafsi Yake hakika inamchukia.”​—Zaburi 11:5.

    “Usimwonee wivu mtu mwenye jeuri, wala kuchagua yoyote kati ya njia zake. Kwa maana mtu mwenye hila ni chukizo kwa Yehova.”​—Methali 3:31, 32.

  • Familia

    Kuwa na Furaha Katika Familia

    Tii wazazi wako

    “Enyi watoto, watiini wazazi wenu katika muungano na Bwana, kwa maana hilo ni jambo la uadilifu: ‘Mheshimu baba yako na mama yako,’ ambayo ndiyo amri ya kwanza yenye ahadi: ‘Ili mambo yakuendee vema nawe ukae muda mrefu duniani.’”​—Waefeso 6:1-3.

    Wafundishe watoto kwa njia inayofaa

    “Nanyi, akina baba, msiwe mkiwakasirisha watoto wenu, bali endeleeni kuwalea katika nidhamu na mwongozo wa akilini wa Yehova.”​—Waefeso 6:4.

    “Enyi akina baba, msiwe mkiwakasirisha watoto wenu, ili wasivunjike moyo.”​—Wakolosai 3:21.

    Mpende na mheshimu mwezi wako wa ndoa

    “Kila mtu mmoja-mmoja kati yenu na ampende hivyo mke wake kama vile anavyojipenda mwenyewe; kwa upande mwingine, mke anapaswa kumheshimu sana mume wake.”​—Waefeso 5:33.

  • Mti

    Kulinda Mazingira

    Kuhusu uharibifu wa mazingira katika Israeli la kale, Biblia ilisema hivi: “Nayo nchi imechafuliwa chini ya wakaaji wake. . . Na wakaaji wake wamehesabiwa hatia.” (Isaya 24:5, 6) Mungu atawahukumu watu wote wanaoharibu mazingira. ‘Atawaharibu wale wanaoiharibu dunia.’ (Ufunuo 11:18) Hawataikimbia adhabu yao.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki