Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w15 8/1 uku. 16
  • Majibu ya Maswali ya Biblia

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Majibu ya Maswali ya Biblia
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2015
  • Habari Zinazolingana
  • Mungu Ana Kusudi Gani kwa Wanadamu?
    Furahia Maisha Milele!—Masomo ya Kujifunza Biblia
  • Majibu ya Maswali ya Biblia
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2015
  • Uhai Ulianzaje?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2015
  • Kusudi Lenyewe la Uhai
    Amkeni!—1992
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2015
w15 8/1 uku. 16

Majibu Ya Maswali Ya Biblia

Je, maisha yana kusudi?

Mwanamume mzee na mtoto wakitazama mbali

Je, nyakati fulani wewe huona kwamba maisha ni mafupi?

Je, umewahi kujiuliza ikiwa maisha yana maana zaidi tu ya kufanya kazi, kufunga ndoa, kutunza familia, na kuzeeka? (Ayubu 14:1, 2) Biblia inaonyesha kwamba hata watu wenye hekima walijiuliza swali kama hilo.—Soma Mhubiri 2:11.

Je, maisha yana kusudi? Kwanza, tunapaswa kujiuliza hivi: Uhai alianzaje? Baada ya kutafakari kuhusu ubongo na jinsi mwili wetu ulivyoumbwa katika njia ya ajabu, wengi wamefikia mkataa wa kwamba lazima kuna Muumba mwenye hekima. (Soma Zaburi 139:14.) Ikiwa ndivyo, lazima Muumba huyo awe na kusudi la kutuumba! Kujua jambo hilo kunaweza kutusaidia kuwa na kusudi maishani.

Kwa nini wanadamu waliumbwa?

Mungu aliwabariki wanadamu wawili wa kwanza na kuwapa mgawo mzuri sana. Alikusudia waijaze dunia, waifanye kuwa paradiso, na kuishi milele.—Soma Mwanzo 1:28, 31.

Kusudi la Mungu halikutimia wanadamu walipoasi utawala wake. Lakini Mungu hajabadili kusudi lake kuelekea wanadamu. Biblia inatuhakikishia kwamba Mungu amekuwa akifanya yote awezayo ili kuwaokoa watu waaminifu na kwamba kusudi lake kuhusu dunia litatimia! Hivyo, Mungu anataka uwe na kusudi maishani! (Soma Zaburi 37:29.) Katika Biblia, utajifunza jinsi ambavyo wewe binafsi unavyoweza kustahili kupata baraka za Mungu za wakati ujao.

Kwa habari zaidi, ona sura ya 3 ya kitabu hiki, Biblia Inafundisha Nini Hasa? kilichochapishwa na Mashahidi wa Yehova

Pia kinapatikana kwenye www.jw.org/sw

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki