Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w17 Novemba kur. 18-19
  • ‘Mwenye Ukarimu Atabarikiwa’

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • ‘Mwenye Ukarimu Atabarikiwa’
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2017
  • Habari Zinazolingana
  • “Kazi Ni Kubwa”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2016
  • Thamini Ukarimu wa Yehova
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2015
  • Ziada Yao Ilijazia Upungufu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2012
  • Yehova Huwabariki Sana Wenye Nia ya Kutoa
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2014
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2017
w17 Novemba kur. 18-19
Hana akimleta mtoto Samweli kwenye maskani

‘Mwenye Ukarimu Atabarikiwa’

KWA MUDA mrefu, dhabihu zimekuwa sehemu muhimu ya ibada ya kweli. Waisraeli walitoa dhabihu za wanyama, na sikuzote Wakristo wamejulikana kwa kutoa “dhabihu ya sifa.” Hata hivyo, kuna dhabihu nyingine ambazo zinampendeza Mungu. (Ebr.  13:15, 16) Dhabihu hizo huleta shangwe na baraka kama mifano ifuatayo inavyoonyesha.

Hana, mtumishi mwaminifu wa zamani, alitamani sana kupata mwana lakini alikuwa tasa. Kupitia sala, alitoa nadhiri kwa Yehova kwamba ikiwa angepata mwana, ‘angemtoa kwa Yehova siku zote za maisha yake.’ (1 Sam. 1:10, 11) Baada ya muda, Hana alipata mimba akazaa mwana na kumwita Samweli. Baada ya Samweli kuachishwa kunyonya, Hana alimpeleka kwenye maskani, kama alivyokuwa ameahidi. Yehova alimbariki Hana kwa roho yake ya kujidhabihu. Alipata pendeleo la kuzaa watoto wengine watano, na Samweli akawa nabii na mwandikaji wa Biblia.—1 Sam. 2:21.

Kama Hana na Samweli, Wakristo leo wana pendeleo la kutumia maisha yao kumtumikia Muumba wao katika utumishi mtakatifu. Yesu aliahidi kwamba tutathawabishwa sana kwa dhabihu zozote tunazotoa tunapomtumikia Yehova.—Marko 10:28-30.

Katika karne ya kwanza, mwanamke Mkristo aliyeitwa Dorkasi alijulikana sana kwa “matendo mema na zawadi za rehema,” yaani, dhabihu alizotoa ili kuwasaidia wengine. Hata hivyo kwa kusikitisha, “alishikwa na ugonjwa akafa,” na kutaniko likahuzunika sana. Wanafunzi waliposikia kwamba Petro alikuwa katika eneo hilo, walimsihi aje mara moja. Wazia shangwe waliyopata Petro alipokuja na kumfufua Dorkasi! Huo ulikuwa ufufuo wa kwanza uliofanywa na mtume. (Mdo. 9:36-41) Mungu hakuwa amesahau dhabihu ambazo Dorkasi alikuwa ametoa. (Ebr. 6:10) Simulizi kuhusu ukarimu wake liliandikwa katika Neno la Mungu ili tuige mfano wake mzuri.

Mtume Paulo pia aliweka mfano bora wa ukarimu kwa kutumia wakati wake kuwasaidia wengine. Katika barua yake aliyowaandikia ndugu zake Wakristo huko Korintho, Paulo alisema hivi: “Kwa upande wangu mimi nitatumia kwa furaha zaidi na kutumiwa kabisa kwa ajili ya nafsi zenu.” (2 Kor. 12:15) Kupitia mambo aliyojionea, Paulo alijifunza kwamba kujidhabihu kwa ajili ya wengine hufanya mtu aridhike, na la muhimu hata zaidi, mtu hupata baraka na kibali cha Yehova.—Mdo. 20:24, 35.

Ni wazi kwamba Yehova anafurahi tunapotumia wakati na nguvu zetu kuendeleza masilahi ya Ufalme na kuwasaidia waabudu wenzetu. Lakini je, kuna njia nyingine za kuunga mkono kazi ya kuhubiri Ufalme? Ndiyo! Mbali na kutumia wakati na nguvu zetu, tunaweza kumheshimu Mungu kwa kutoa michango ya hiari. Michango hiyo hutumiwa kuendeleza kazi ya kuhubiri habari njema ulimwenguni pote, na pia kuwategemeza wamishonari na wengine walio katika utumishi wa pekee wa wakati wote. Isitoshe, michango hiyo ya hiari hutumiwa kutafsiri machapisho na kutayarisha video, kusaidia wakati wa majanga, na pia kujenga Majumba ya Ufalme. Tuna hakika kwamba ‘mwenye ukarimu atabarikiwa.’ Isitoshe, tunapompa Yehova vitu vyetu vyenye thamani, tunamheshimu Yeye.—Met. 3:9; 22:9.

Jinsi Ambavyo Wengine Hutoa Michango Kwa Ajili Ya Kazi Ya Ulimwenguni Pote

Kama ilivyokuwa katika siku za mtume Paulo, watu wengi leo ‘huweka kando kitu fulani,’ au kiasi fulani cha pesa ambacho wanatumbukiza katika masanduku ya michango yaliyoandikwa “Kazi ya Ulimwenguni Pote.” (1 Kor. 16:2) Kila mwezi, makutaniko hutuma michango hiyo katika ofisi ya tawi ya Mashahidi wa Yehova inayosimamia kazi katika nchi yao. Unaweza pia kutuma michango yako moja kwa moja katika shirika la kisheria linalotumiwa na Mashahidi wa Yehova nchini mwenu. Ili kujua shirika la kisheria linalotumiwa na Mashahidi wa Yehova katika nchi yenu, tafadhali wasiliana na ofisi ya tawi. Anwani ya ofisi ya tawi inapatikana katika Tovuti ya www.jw.org/sw. Ikitegemea sheria za nchi yenu, michango unayoweza kutuma moja kwa moja inatia ndani:

MICHANGO YA MOJA KWA MOJA

  • Michango inayotumwa kupitia mfumo wa elektroniki au kadi za benki. Ofisi nyingine za tawi zinatumia pia Tovuti ya jw.org au tovuti nyingine inayopendekezwa kupokea michango.

  • Michango ya pesa taslimu, vito, au mali yoyote ya kibinafsi iliyo na thamani. Ambatanisha barua inayoonyesha kwamba pesa taslimu au mali hizo ni michango ya moja kwa moja.

MPANGO WA MICHANGO YENYE MASHARTI

  • Hii ni michango ya pesa taslimu zinazotolewa kwa masharti kwamba zinaweza kurudishwa kwa aliyechangia akizihitaji.

  • Ambatanisha barua inayoonyesha kwamba ni mchango wenye masharti.

UTOAJI ULIOPANGWA

Mbali na zawadi za pesa na mali zenye thamani, kuna njia nyingine za kutoa michango kwa ajili ya kazi ya Ufalme ya ulimwenguni pote. Njia hizo zimeorodheshwa hapa chini. Haidhuru ni njia gani ambayo ungependa kutumia, tafadhali wasiliana kwanza na ofisi ya tawi inayosimamia kazi nchini mwenu ili kujua ni njia gani zinazotumika katika nchi yenu. Kwa kuwa matakwa na sheria za kodi zinatofautiana, ni muhimu kuwasiliana na washauri wa mambo ya kisheria na kodi kabla ya kuchagua njia bora ya kutoa mchango.

Bima na Malipo ya Kustaafu: Mchango huu unatolewa kwa kutaja kihususa shirika la Mashahidi wa Yehova kuwa ndilo litakalofaidika na bima ya maisha au malipo ya uzeeni au ya kustaafu.

Akaunti za Benki: Akaunti za benki zinaweza kulipwa baada ya mtu kufa kwa shirika linalotumiwa na Mashahidi wa Yehova, kulingana na matakwa ya benki za kwenu.

Hisa na Dhamana: Hisa na dhamana zinaweza kutolewa kama mchango kwa shirika la Mashahidi wa Yehova zikiwa zawadi ya moja kwa moja au mtoaji anaweza kuandika kwamba shirika hilo lipewe hisa na dhamana zake baada ya yeye kufa.

Ardhi na Nyumba: Ardhi au nyumba zinaweza kutolewa kama mchango kwa shirika la Mashahidi wa Yehova, zikiwa zawadi ya moja kwa moja au zawadi yenye masharti, yaani, mtoaji anaweza kuendelea kuishi humo hadi kifo chake.

Wosia na Amana: Mali au pesa zinaweza kuachiwa shirika la Mashahidi wa Yehova kama urithi kwa njia ya wosia halali, au linaweza kutajwa kuwa shirika ambalo litafaidika na mkataba wa amana. Chini ya mpango huu, kodi fulani zinaweza kupunguzwa.

Maneno “utoaji uliopangwa” yanaonyesha kwamba mtu anapaswa kufanya mipango hususa ili atoe michango ya aina hiyo. Broshua ya Kiingereza na Kihispania yenye kichwa Charitable Planning to Benefit Kingdom Service Worldwide imetayarishwa ili kuwasaidia watu wanaotaka kutegemeza kazi inayofanywa na Mashahidi wa Yehova ulimwenguni pote. Broshua hiyo iliandikwa ili kueleza njia mbalimbali za kuchangia sasa au wakati ujao, kama vile urithi mtu anapokufa. Huenda habari fulani katika broshua hiyo hazitumiki katika nchi yenu kwa sababu ya sheria za kodi au sheria nyingine. Kwa kutumia njia kama hizo za kutoa michango, watu wengi wametegemeza shughuli zetu za kidini na kazi yetu ya kutoa misaada ulimwenguni pote, nao wamepunguziwa kodi. Ikiwa broshua hiyo inapatikana katika nchi yenu, unaweza kuomba nakala kutoka kwa mwandishi wa kutaniko lenu.

Kwa habari zaidi, bofya kiunganishi “Toa Mchango kwa Ajili ya Kazi Yetu ya Ulimwenguni Pote” kwenye sehemu ya chini ya ukurasa wa kwanza wa jw.org/sw, au wasiliana na ofisi ya tawi.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki