Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • wp19 Na. 3 kur. 12-13
  • Maisha Bora​—Unaweza Kuyapataje?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Maisha Bora​—Unaweza Kuyapataje?
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Toleo la Watu Wote)—2019
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • MUNGU ANAAHIDI KUGEUZA MAISHA DUNIANI YAWE KAMA ALIVYOKUSUDIA
  • YESU ALIONYESHA JINSI ATAKAVYOBORESHA MAISHA YA WANADAMU WATIIFU
  • BARABARA INAYOONGOZA KWENYE MAISHA BORA—JINSI YA KUIPATA
  • KUPIGA HATUA YA KWANZA KWENYE SAFARI YAKO
  • Jinsi ya Kumwabudu Mungu Kwa Njia Inayofaa
    Biblia Inatufundisha Nini?
  • Mungu Atafanya Mambo Gani?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Toleo la Watu Wote)—2019
  • Endeleeni ‘Kumsikiliza’
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2021
  • Ibada Ambayo Mungu Anakubali
    Biblia Inafundisha Nini Hasa?
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Toleo la Watu Wote)—2019
wp19 Na. 3 kur. 12-13
Mwanasayansi mmoja aliyetajwa mwanzoni akisoma Biblia
Mwanasayansi mmoja aliyetajwa mwanzoni akisoma Biblia

Maisha Bora​—Unaweza Kuyapataje?

MAISHA leo ni tofauti na jinsi ambavyo Mungu alikusudia yawe. Dunia ilipaswa kuwa imejaa watu wanaoheshimu enzi kuu ya Muumba wao, wanaopenda mwongozo wake, na wanaoonyesha upendo na sifa nyingine alizo nazo. Wangeshirikiana kwa shangwe kutunza familia zao, kuvumbua vitu vipya, na kuifanya dunia yote iwe paradiso.

MUNGU ANAAHIDI KUGEUZA MAISHA DUNIANI YAWE KAMA ALIVYOKUSUDIA

  • “Anakomesha vita katika dunia yote.”​—Zaburi 46:9.

  • “Wakati uliowekwa ukafika . . . [wa] kuwaharibu wale wanaoiharibu dunia.”​—Ufunuo 11:18.

  • “Hakuna mkaaji atakayesema: ‘Mimi ni mgonjwa.’”—Isaya 33:24.

  • “Watu wangu niliowachagua watafurahia kikamili kazi ya mikono yao.”​—Isaya 65:22.

Unabii huu wote utatimizwaje? Mungu amemchagua Mwana wake, Yesu, kuwa Mfalme wa serikali isiyo na kasoro ambayo itatawala dunia kutoka mbinguni. Biblia inaiita serikali hiyo Ufalme wa Mungu. (Danieli 2:44) Biblia inasema hivi kumhusu Yesu: “Mungu atampa kiti cha ufalme . . . , naye atatawala akiwa Mfalme.”—Luka 1:32, 33.

Yesu alipokuwa duniani, alifanya miujiza mingi kuonyesha kwamba akiwa Mtawala, atafanya maisha yetu kuwa bora tofauti na yalivyo sasa.

YESU ALIONYESHA JINSI ATAKAVYOBORESHA MAISHA YA WANADAMU WATIIFU

  • Aliponya magonjwa ya kila aina na kuonyesha kwamba atawaondolea kabisa wanadamu hali hizo.—Mathayo 9:35.

  • Alituliza bahari, kuonyesha jinsi atakavyowalinda wanadamu kwa kudhibiti nguvu za asili.—Marko 4:36-39.

  • Alilisha maelfu ya watu, kuonyesha kwamba atatimiza mahitaji ya msingi ya watu.—Marko 6:41-44.

  • Aligeuza maji kuwa divai kwenye sherehe ya harusi akionyesha kwamba atawawezesha watu kufurahia maisha.—Yohana 2:7-11.

Unaweza kufanya nini ili ufurahie maisha ambayo Mungu anawaandalia wale wanaompenda? Kuna “barabara” unayopaswa kuifuata. Biblia inasema, hiyo ni “barabara inayoongoza kwenye uzima . . . , na ni wachache wanaoipata.”—Mathayo 7:14.

BARABARA INAYOONGOZA KWENYE MAISHA BORA—JINSI YA KUIPATA

Barabara inayoongoza kwenye uzima ni nini? Inawakilisha mambo yote ambayo Mungu anatuagiza tufanye. Mungu anasema: “Mimi, Yehova, ni Mungu wako, Ninayekufundisha ili ujifaidi mwenyewe, Ninayekuongoza katika njia unayopaswa kutembea.” (Isaya 48:17) Ukitembea katika njia hii, maisha yako yataboreka.

Yesu alisema hivi: “Mimi ndiye njia na kweli na uzima.” (Yohana 14:6) Ikiwa tutaamini kweli ambazo Yesu alifundisha na kuiga mfano wake, tutamkaribia Mungu na kuboresha maisha yetu.

Unaweza kuipataje barabara inayoongoza kwenye uzima? Kuna dini nyingi, lakini Yesu alionya hivi: “Si kila mtu anayeniambia, ‘Bwana, Bwana,’ atakayeingia katika Ufalme wa mbinguni, bali yule anayefanya mapenzi ya Baba yangu aliye mbinguni ndiye atakayeingia.” (Mathayo 7:21) Pia, alisema hivi: “Kwa matunda yao mtawatambua.” (Mathayo 7:16) Biblia inaweza kukusaidia uitambue ibada ya kweli na kuitofautisha na ibada ya uwongo.—Yohana 17:17.

Unaweza kuanzaje kutembea kwenye barabara inayoongoza kwenye uzima? Kwa kujifunza kumhusu Yule aliyetupatia uhai: Yeye ni nani? Anaitwa nani? Ana sifa gani? Anafanya nini? Anataka sisi tufanye nini?a

Mungu hakutaka tu wanadamu wafanye kazi, wale, wacheze, na kupata watoto. Badala yake, alitupa uwezo wa kumjua na kusitawisha urafiki naye. Tunaweza kumwonyesha tunampenda kwa kufanya mapenzi yake. Yesu alisema: “Uzima wa milele ndio huu, wakujue wewe, Mungu wa pekee wa kweli.”—Yohana 17:3.

KUPITIA BIBLIA, MUNGU ANAKUFUNDISHA “ILI UJIFAIDI MWENYEWE.”​—ISAYA 48:17

KUPIGA HATUA YA KWANZA KWENYE SAFARI YAKO

Utahitaji kufanya mabadiliko ili uweze kumpendeza Mungu wa pekee wa kweli. Huenda jambo hilo likaonekana kuwa gumu. Lakini ukweli ni kwamba, hiyo ni safari inayofurahisha, ambayo kama safari nyingine, inaanza kwa kupiga hatua moja ya kwanza. Ili kupata majibu ya maswali ya msingi kumhusu Mungu, Mashahidi wa Yehova wanakualika ujifunze nao Biblia bila malipo, mahali na wakati unaokufaa. Unaweza kuwasiliana nasi kwa kutembelea tovuti yetu www.jw.org/sw.

a Ona Mnara wa Mlinzi, Na. 1 2019.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki