Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 12/89 uku. 8
  • Kutangaza Habari Njema-Wakati wa Sikukuu

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Kutangaza Habari Njema-Wakati wa Sikukuu
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1989
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • UNGEWEZA KUSEMA NINI?
  • ONYESHA UFIKIRIO
  • Kutoa Habari Njema—Wakati wa Sikukuu
    Huduma Yetu ya Ufalme—1990
  • Utafanya Nini Wakati wa Sikukuu?
    Huduma ya Ufalme—2013
  • Chukua Msimamo Upande wa Ibada ya Kweli
    Biblia Inafundisha Nini Hasa?
  • Wasaidie Wengine Wajifunze Juu ya Mwana wa Mungu, Yesu Kristo
    Huduma Yetu ya Ufalme—1993
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—1989
km 12/89 uku. 8

Kutangaza Habari Njema-Wakati wa Sikukuu

1 Wakati huu wa mwaka watu wengi wanajaribu juu chini kufurahia shangwe fulani katikati ya mahangaiko ya ulimwengu huu. Je! umepata kuhisi mwelekeo usiofaa juu ya kujaribu kuwatolea ushahidi watu hao wakati huu ambao kwa wazi wanashughulika mno? Ijapokuwa mabaya na mambo ya kupita kiasi yanayokuwa kawaida ya majira ya sikukuu, akili za wengi zinaelekezwa kwa Mungu wanaposikia usemi unaorudiwa mara nyingi “Juu ya dunia amani miongoni mwa watu wa nia njema,” NW.

2 Hakuna shaka tutakuta watu wengi ambao kwa kweli wana shughuli mno wakati wa sikukuu. Jambo hilo litahitaji ufikirio upande wetu. Yesu alipokuwa duniani, si kwamba tu alitambua hisia za wengine na kuwahurumia bali pia alitambua uhitaji wao na akajaribu sana kuwasaidia. Leo watu wanaomwogopa Mungu wana uhitaji uo huo wa ujumbe wa Ufalme.—Mt. 9:36, 37.

3 Mwenye nyumba ajapo kwenye mlango, jaribu kuona hali katika nyumba hiyo na kuwa mwenye ufikirio. Je! anashughulika na kuhudumia wageni au katikati ya matayarisho makubwa? Ikiwa hivyo ingefaa zaidi kutoa mahubiri mafupi. Hata hivyo, katika kisa kingine huenda ukatambua kwamba mtu fulani hana shughuli mno, na kwa kuonyesha fadhili na kwa weupe wa moyo kupendezwa kibinafsi na mtu huyo, huenda ukaweza kuendelea kwa busara na kutoa ushahidi.

UNGEWEZA KUSEMA NINI?

4 Baada ya utangulizi wa urafiki, huenda ukasema: “Mengi yanasemwa siku hizi juu ya amani duniani na nia njema kuelekea watu. Je! matumizi ya kanuni za Biblia yatatusaidia kweli kweli tufanye na kudumisha mahusiano mazuri na wengine?” Mruhusu mwenye nyumba wako ajibu, halafu uendelee na Kichwa cha Mazungumzo cha wakati huu na kutoa toleo la fasihi.

5 Ukihisi kwamba utoaji mfupi zaidi ungefaa, huenda ukasema: “Pindi ya mwaka, tunakuta watu wengi wakifikiria juu ya kuzaliwa kwa Yesu. Hilo lilikuwa ni tukio la maana sana. Naweza kukuonyesha ambayo Biblia inasema juu ya tukio jingine la maana sana—kuja kwa Ufalme wa Mungu? Ni Yesu mwenyewe aliyesema . . . [Soma Mathayo 6:33.].” Halafu umtolee mwenye nyumba toleo la wakati huu, ukitaja jambo fulani juu ya Ufalme.

6 Watu wakitutakia sikukuu ya furaha, hakuna sababu ya kutokeza ubishi juu ya salamu zao za sikukuu. Badala yake, tunaweza kuwashukuru kwa ufupi kwa ajili ya fadhili zao na wakati wao katika kutusikiliza sisi. Bila shaka, kama wakituuliza hususa maoni yetu juu ya sikukuu, tutajibu kikweli na kwa heshima. Kitabu Reasoning kinatoa habari fulani bora sana kwenye kurasa 176-8 zitakazokusaidia. Ona pia Vichwa vya Mazungumzo; 39B.

ONYESHA UFIKIRIO

7 Mambo mengi ya kupendeza yametokana na kushiriki utoaji wa ushahidi wakati wa sikukuu. Hata hivyo, kutakuwako uhitaji kwetu sote kuwa wenye busara na kutoa ujumbe wa ukweli katika njia itakayovutia moyo na akili ya mwenye nyumba. Kumbuka shauri la Paulo kwenye Wakolosai 4:6, na kuacha ‘maneno yetu yawe na neema sikuzote, yakikolea munyu.’ Shauri hilo zuri linafaa hasa wakati wa sikukuu.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki