Kijitabu Blood Kitakachodarisiwa
1 Kijitabu Jehovah’s Witnesses and the Question of Blood (Mashahidi wa Yehova na Suala la Damu) kitafikiriwa kwenye Funzo la Kitabu la Kundi kwa majuma ya Juni 26 mpaka Agosti 7, 1988. Maswali ya Funzo yatakayotumiwa yanapatikana kwenye nyongeza ya Huduma ya Ufalme Yetu ya mwezi huu.
2 Kijitabu hicho, ambacho kilichapishwa mara ya kwanza katika 1977, kina habari ambazo ni zenye upendezo muhimu kwa Mashahidi wa Yehova na pia kwa wengine ambao wanatamani kushikilia yale ambayo Neno la Mungu linasema kuhusu utakato wa damu. Kufikiriwa kwa kijitabu Blood wakati huu kutawanufaisha sana wapya wengi walio kundini ambao huenda wasiwe wamejifunza habari hizi wakati uliopita. Kitasaidia kila mmoja ajiandae vizuri kukabili hali yo yote ya dharura ambayo huenda ikatokea ikitaka uthibitisho wa msimamo wetu wa Kimaandiko kuhusu suala linaloendelea la kutiwa damu mishipani.
3 Yaelekea kundi lenu lina vijitabu vya kutosha kumpa nakala kila mmoja anayehudhuria funzo. Ikiwa sivyo, mwangalizi wa utumishi amepaswa ajitahidi mara hiyo kupata nakala zaidi kutoka kwa makundi ya karibu badala ya kuagizwa kutoka kwa Sosaiti. Makundi mengi yana akiba kubwa ya vijitabu Blood, na hivi vinaweza kuhamishwa vipelekwe kwenye makundi mengine katika sehemu hiyo. Waangalizi wa mizunguko wanaweza kusaidia akina ndugu katika jambo hili. Bila shaka, ikiwa vitabu hivyo havipatikani mahali penu, vinaweza kuagizwa kutoka kwa Sosaiti pamoja na vichapo vingine. Tafadhali mziagize vijitabu vingi kuzidi mahitaji yenu kwa ajili ya mafunzo ya vitabu yaliyoratibiwa.
4 Wahubiri wote wanasihiwa watayarishe vizuri na kuwapo kila juma kwa ajili ya kufikiriwa kwa habari hii yenye maana sana. Hakikisheni kualika wapya wanaopendezwa ili wahudhurie pia, na pageni ili wawe na nakala yao wenyewe ya kijitabu Blood kwa ajili ya fikirio hili.