Sanduku la Swali-1
● Je! mapainia wanapaswa kuwachukulia washiriki wa jamaa fasihi (vitabu) kwa bei ya painia?
Ni vizuri kukumbuka kwa nini Sosaiti inafanya iwezekane kwa mapainia kupata fasihi kwa bei iliyopunguzwa. Huu ni uandalizi wa upendo wa Sosaiti, kwa gharama yayo yenyewe, ili kusaidia mapainia walipie gharama zao nyingine.
Kwa sababu hiyo, wahubiri wote ambao ni washiriki wa jamaa ya painia na ambao si mapainia, wawe ni watoto au watu wazima, wanapaswa kuchukua fasihi zao na magazeti kwa ajili ya utumishi wa shambani kwa bei za mhubiri wa kawaida.