Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 5/88 uku. 5
  • Wafunze Wanafunzi Jinsi ya Kutumia Biblia

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Wafunze Wanafunzi Jinsi ya Kutumia Biblia
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1988
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • TUMIA BIBLIA
  • Wasaidie Wanafunzi Wako wa Biblia Wafikie Ubatizo
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2021
  • Jinsi ya Kumsaidia Mwanafunzi wa Biblia Afikie Hatua ya Ubatizo—Sehemu ya Pili
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2020
  • Kazia Uangalifu ‘Ufundi Wako wa Kufundisha’
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2008
  • Kuongoza Funzo la Biblia Nyumbani
    Huduma Yetu ya Ufalme—1993
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—1988
km 5/88 uku. 5

Wafunze Wanafunzi Jinsi ya Kutumia Biblia

1 “Mlipopata lile neno la ujumbe la Mungu mlilolisikia kwetu, mlilipokea si kama neno la wanadamu, bali kama neno la Mungu; na ndivyo lilivyo kweli kweli.” (1 The. 2:13) Tukiwa Wakristo wa kweli, tunahangaikia kuacha Biblia ijisemee. Basi, unapoongoza funzo la Biblia, msaidie mwanafunzi wako athamini kwamba anajifunza fikira za Yehova, si za mwanadamu. Kwa kufundisha wanafunzi watumie Biblia vizuri, unaweza kujenga uhakika katika Maandiko, msingi imara wa imani, na uwezo wa kutetea itikadi zao kutoka katika Biblia.—2 Tim. 3:16, 17; 1 Pet. 3:15.

2 Unaanza kumfundisha mwanafunzi wako kutumia Biblia lini? Unamfundishaje orodha ya vitabu vya Biblia na jinsi anavyoweza kupata maandiko? Mwanafunzi anaweza kufanya nini kibinafsi ili ajifunze maandiko fulani ya msingi, na wewe unaweza kumsaidiaje? Kuna njia mbalimbali zinazoweza kutumiwa kwa mafanikio.

TUMIA BIBLIA

3 Tangu mwanzo, mwonyeshe mwanafunzi ukurasa ulio katika Biblia ambamo vitabu vyote vya Biblia vimeorodheshwa na umwonyeshe jinsi anavyoweza kupata kila kimoja. Maandiko mengi yamedondolewa katika vichapo vya Sosaiti, na mengine yamenukuliwa bila kudondolewa. Mwanzoni, ingependekezwa kufungua na kuyasoma yote kutoka katika Biblia, hivyo ukikazia kwamba ni funzo la Biblia. Hii itachukua wakati zaidi, lakini litamsaidia mwanafunzi azoelee Biblia yake. Pia litakuza uhakika wake kwamba yale ambayo yametaarifiwa katika vichapo yanategemea Biblia.

4 Mwanafunzi anapouliza maswali, msaidie apate majibu katika Biblia kwa kufungua maandiko yanayofaa. Katika njia hii yeye atajua kwamba anapata majibu ya Mungu kwa maswali yake. (Yn. 17:17) Msaidie mwanafunzi asababu katika maandiko na kuthamini kikamili jibu la Biblia. Mwishoni mwa funzo, huenda ukataka kurudia maandiko mawili au matatu ya msingi kwa kuacha mwanafunzi ayafungue na kuyaeleza katika maneno yake mwenyewe. Hilo litamwezesha atetee imani yake kutoka Biblia. Pia, kwa kutumia Biblia, atajifunza kuongea akiwa na mamlaka na usadikisho anaposhiriki na wengine yale ambayo amejifunza.—Mdo. 17:1-3.

5 Mtie moyo mwanafunzi afungue na kusababu katika maandiko ambayo yamenukuliwa anapotayarisha somo kwa ajili ya funzo lake la kibinafsi, Funzo la Mnara wa Mlinzi, na mikutano mingine. Hivyo, yeye atakuwa tayari kutumia vizuri Biblia yake wakati wa mikutano na kutoa maelezo yanayotegemea Maandiko ya habari inayozungumziwa. Pia, mwonyeshe orodha ya “Fahirisi ya Maneno ya Biblia” nyuma ya New World Translation. Fahirisi hiyo itamsaidia kupata maandiko kuhusu habari nyingi tofauti tofauti na pia majibu kwa maswali. Maandiko yanaposomwa kibinafsi na kuchunguzwa, kweli ambazo anajifunza zinapenya ndani na kuwa zenye kina kirefu.

6 Kuwafundisha wanafunzi jinsi ya kutumia Biblia kutakuwa na manufaa zenye kudumu. Mwanafunzi atang’amua kwamba fundisho analopokea linatoka kwa Mungu. Ndiyo, “neno la Mungu li hai” na ni lenye nguvu. (Ebr. 4:12) Tunataka kuwasaidia wengine wawe stadi katika ‘kutumia kwa halali neno la kweli.’—2 Tim. 2:15.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki