Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 6/88 kur. 1-3
  • Kutoa kwa Uchangamfu Ukiwa Painia

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Kutoa kwa Uchangamfu Ukiwa Painia
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1988
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • JAMBO AMBALO UNAWEZA KUFANYA
  • KUZA KAWAIDA NZURI
  • Wanatakwa—Mapainia-Wasaidizi 2,500
    Huduma Yetu ya Ufalme—1997
  • Mradi Mzuri kwa Ajili ya Mwaka Mpya wa Utumishi
    Huduma ya Ufalme—2007
  • Je! Wewe Unaweza Kufanya Upainia Msaidizi?
    Huduma Yetu ya Ufalme—1992
  • Sanduku La Swali
    Huduma Yetu ya Ufalme—1993
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—1988
km 6/88 kur. 1-3

Kutoa kwa Uchangamfu Ukiwa Painia

1 “Mungu anapenda mpaji mchangamfu.” (2 Kor. 9:7, NW) Mtume Paulo alithamini ukarimu wa Yehova na alionyesha jambo hili katika kazi zake zenye jitihada isiyozuiwa miongoni mwa Wathesalonike. Kwa hiyo, yeye aliwaandikia hivi baadaye: “Tulipendezwa sana kuwapa ninyi . . . habari njema za Mungu.”—1 The. 2:8, NW.

2 Je! sisi tunahisi hivyo hivyo kuhusu kushiriki hazini hiyo ya kiroho pamoja na wengine? Ikiwa ndivyo, je! tunaweza kuangalia kwa uzito matazamio yetu ya mbele ya kutumikia tukiwa painia msaidizi wakati wa Julai na Agosti na pengine kuingia katika utumishi wa painia wa kawaida katika Septemba?

JAMBO AMBALO UNAWEZA KUFANYA

3 Kuingia katika kazi ya painia msaidizi au wa kawaida si jambo ambalo linaweza kutukia tu. Jitihada inayofaa ikitokana na moyo uliochochewa vizuri italeta baraka ya Yehova. Mpelekee Yehova jambo hilo katika sala. Mweleze tamaa yako ya moyoni. (1 Yn. 5:14; 2 The. 3:1) Kadiria hali yako kwa ufuataji haki uone mahali ambapo unaweza kufanya marekebisho ili ufikie matakwa hayo. Kuamka mapema kidogo asubuhi ili uungane na mapainia wengine katika utumishi wa shambani huenda likawa ndilo jambo tu linalohitajiwa kwako ili utimize ratiba ya painia. Au labda kutoa ushuhuda wakati wa jioni kutakusaidia ufikie jambo hilo.

4 Zungumzo la waziwazi pamoja na mapainia wengine, mwangalizi wako wa utumishi, au kiongozi wako wa Funzo la Kitabu la Kundi anaweza kuandaa madokezo yenye msaada. (Mit. 15:22; 16:3) Washiriki wa jamaa wanaweza kutia moyo pia, hasa ikiwa wao ni waabudu wenzetu. Mambo mengi yaliyoonwa ya mapainia wasaidizi na wa kawaida wenye wajibu wa kutunza jamaa yamekuwa kwamba washiriki wao wa jamaa wanajitia upande wao na kushangilia hali ya kiroho iliyofanyiwa maendeleo katika jamaa inayotokana na mshiriki mmoja kufanya upainia.

KUZA KAWAIDA NZURI

5 Ni jambo la maana sana kujifunza kuratibu utendaji wako. Hata katika utoaji wa vitu vya kimwili, Paulo alipendekeza kwamba akina ndugu katika Korintho wafuate kielezi cha kawaida ili kuhakikisha kwamba makusudio mazuri ya mioyo yao yanatekelezwa. (1 Kor. 16:2) Kushikilia kwa uthabiti kawaida iliyofikiriwa vizuri ya kushiriki katika kazi ya haraka sana ya kuhubiri ni jambo lenye umaana mkubwa sana. Kujitia nidhamu, kuanza mambo mwenyewe, na kupiga moyo konde ni mambo yanayohitajiwa kabisa.—1 Kor. 9:23, 25, 27.

6 Yaone mambo jinsi yalivyo kuhusu kuingia kwako katika utumishi wa painia msaidizi na wa kawaida. Huwezi kupata hali zinazofaa kabisa katika mfumo huu. Yesu alisema kwamba wale wanaotanguliza ufalme wanapaswa kutazamia kupata dhiki pamoja na shangwe na baraka zilizoahidiwa sasa, na “katika mfumo wa mambo unaokuja uhai wa milele.” (Marko 10:29, 30; Mdo. 14:22, NW) Kwa hiyo ni jambo zuri kuiga imani na kielelezo cha wengi ambao wanapainia ijapokuwa afya mbaya, fedha za kiasi tu, au vizuizi vingine vikubwa. Wao wanaepuka kufanya kitu cho chote katika mfumo huu wa kale kuwa jambo kubwa katika maisha yao. (1 Kor. 7:29-31) Kama mapainia wengine wanavyosema, wao wamejifunza tu ‘kufanya kazi kuzunguka matatizo yao’ ili wapainie.—Linganisha 2 Wakorintho 12:7-10.

7 Kweli kweli, wote ambao wanatoa kwa nia kutoka kwa moyo mzuri kulingana na hali zao mmoja mmoja wanatamkwa kuwa wenye furaha na Yehova. (Isa. 65:14) Wao wanavuna kwa wingi kwa njia ya kupata amani ya ndani na uradhi pamoja na kuzaa matunda kwa wingi kwa kuwasaidia watu waje upande wa Yehova. Baraka kama hizo na nyingine nyingi zinaweza kuwa zako ikiwa wewe unakubali mwaliko wa kutoa kwa uchangamfu ukiwa painia msaidizi au wa kawaida.—2 Kor. 9:6; Mit. 11:25.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki