Vuka Uje Makedonia
1 Ilikuwa katika majira ya mwaka 50 C.E. Baada ya kupitia Frigia na Galatia kwenye safari yake ya pili ya umisionari mtume Paulo na waandamani wake wasafiri walikuja Troa upande wa magharibi wa Esia Ndogo. Huko Paulo aliona njozi isiyo ya kawaida, iliyokuwa juu ya mwanamume mmoja akimwita: “Vuka, uje Makedonia, utusaidie.” Mara moja maneno yalikatwa kwamba Mungu alikuwa ameamuru kikundi hicho kitangaze habari njema Makedonia. Basi, wakavuka Bahari ya Aegea mpaka Samothrake kisha wakaelekea Neapoli, bandari ya jiji la Filipi, jiji kuu la wilaya ya Makedonia.—Mdo. 16:8-12.
2 Matokeo ya ‘kuvuka huko kuingia Makedonia’ yamesimuliwa kwa msisimuo katika historia ya karne ya kwanza ya kundi la Kikristo. Baada ya kuanzisha kundi huko katika Filipi Paulo alisonga mbele kuingia Thesalonike, Beroya, Athene, na Korintho. Katika mengi ya majiji hayo makundi yalianzishwa na katika mengine waongofu mmoja mmoja walikubali njia ya ukweli. Lo! ni shangwe na baraka za namna gani zilizokijia kikundi hicho kilichoitikia mwito wa kuifikia sehemu za mbali kikiwa na ujumbe wa Biblia wenye kuchangamsha.
MAKEDONIA YA KI-SIKU-HIZI
3 Tangu 1975 kampeni ya kila mwaka kuanzia Julai mpaka Septemba ya kufikia eneo lililo mbali na lisilofanyiwa kazi kwa ukawaida imerejezewa kuwa Makedonia na akina ndugu wa Afrika Mashariki. Kwa Paulo na waandamani wake mvuko wa kuingia katika eneo jipya ulimaanisha kusafiri labda maili 150 kwa merikebu kutoka Esia Ndogo kufikia Ulaya na Makedonia. Vivyo hivyo, leo makundi fulani fulani na watu mmoja mmoja katika mahali petu wanasafiri kufikia maili 100 au zaidi ili kufikia eneo la mbali. Na, kama ilivyokuwa katika karne ya kwanza, makundi yameanzishwa na watu mmoja mmoja wakasaidiwa katika sehemu kama vile Maralal, Isiolo, Lunga Lunga, Kabale, Kasese, Sanga Njeru, Mpwapwa na nyinginezo. Baada ya kukata maneno kwamba ni mapenzi ya Mungu wao wahubiri habari njema katika Makedonia kikundi kile kilianza safari yacho. Kwa uhakika ni mapenzi ya Mungu leo ujumbe uwafikie watu wa aina zote ili kwamba wote wafikie toba.—Mdo. 16:10; 1 Tim. 2:4; 2 Pet. 3:9.
4 Ili kushiriki katika kampeni ya Makedonia ya mwaka huu na kwa kuitikia makala katika Huduma ya Ufalme Yetu ya Januari 1988 “Usiache Mkono Wako Upumzike,” wahubiri wengi wanajitayarisha kufanyia kazi maeneo yasiyogawiwa mtu au kusaidia kundi kwa muda kueneza eneo layo. Inadokezwa kwamba wakati wa Julai kila kundi lifanye jitihada ya pekee kueneza eneo lililogawiwa kundi ambalo halijafanyiwa kazi tangu Septemba 1987. Baada ya hapo, kundi linaweza kuingia katika eneo la mbali zaidi. Huku huenda makundi fulani yakapokea migawo ya “Makedonia” hususa, yaelekea kila kundi litapata kuwa jambo linalowezekana kufikia zaidi katika sehemu za nje-nje kwa habari njema kuliko ilivyo kawaida.
ANZA MATAYARISHO SASA
5 Mwangalizi wa utumishi atataka kupanga sasa eneo la kundi ambalo halifanyiwi kazi kwa ukawaida ambalo litafikiwa wakati wa Julai. Baada ya hapo mipango inaweza kukamilishwa kwa sehemu za nje-nje. Tumieni kwa faida siku za soko, mahali ambapo hali zinaruhusu, ili kufikia hesabu kubwa ya watu. Kundi lapaswa liwe na akiba ya kutosha ya vitabu Furaha na Kuokolewa kwa toleo la Juni na Julai. Kwa Agosti na Septemba tutaonyesha broshua kama ilivyotangazwa. Wakati wa kampeni ya Makedonia toleo la pekee la Mwalimu Mkuu katika Kikuyu pamoja na Furahia Maisha kwa Kshs. 6/= linaweza kutolewa mahali panapofaa. Bebeni akiba ya kutosha ya trakti zetu mpya zenye kuvutia ili kuziacha mahali pasipo na mtu nyumbani. Tunzeni maandishi sahihi na jitahidini kufuatia kupendezwa ko kote kunakopatikana. Tafadhali hakikisheni kuweka kando pesa za kutosha ili kujiandaa vizuri kwa matoleo na kukupa gharama ya kusafiri kwenda kwenye sehemu hizo za mbali.
6 Je! inawezekana kwako kuongeza ushiriki wako katika huduma wakati wa kipindi hiki? Agosti ni mwezi unaofaa sana kwa wazazi na vijana waliobatizwa kupanua huduma yao kwa sababu ya likizo ya shule. Wengi wanaweza kufanya upainia msaidizi. Wakisaidiwa na wazazi na vijana wenye madaraka au watu wenye umri mkubwa hata vijana ambao hawajabatizwa wanaweza kupanua utendaji wao wa Kikristo. Labda unapanga kuanza upainia wa kawaida katika Septemba 1, 1988. Ni njia bora kama nini ya kuanza mwaka mpya wa utumishi ukiwa painia wa kawaida katika kampeni ya eneo la mbali. Kisha, pia, tukitumia broshua kama toleo letu Agosti na Septemba ni miezi mizuri ya kuwasaidia wapya ambao wanastahili kuanza kueleza itikadi yao katika huduma rasmi.
7 Ndiyo, hata katika nyakati za ki-siku-hizi sauti za wale wanaotweta na kupiga kite kwa sababu ya makuruhi ya mfumo huu zinaendelea kupaaza sauti kwa mlio: “Vuka, uje Makedonia ukatusaidie.” Yehova na aendelee kubariki jitihada zetu za kuvuka katika sehemu hizi zisizogawiwa mtu na zisizofanyiwa kazi kwa ukawaida ili kusaidia watu wenye moyo wenye ufuataji haki wasikie habari njema.—Eze. 9:4.