Mikutano Inayotusaidia Kufanya Wanafunzi
JUMA LINALOANZA JUNI 6
Wimbo 29 (57)
Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Dokeza utoaji unaofaa wa magazeti ya karibuni, na tia moyo wahubiri wote washiriki katika kazi ya magazeti mwisho juma huu.
Dak. 20: “Kutoa kwa Uchangamfu Ukiwa Painia.” Maswali na majibu. Tumia dakika tano za mwisho kuhoji wahubiri ambao wanaanza kufanya upainia msaidizi mwezi huu au unaofuata. Au hoji painia wa kawaida aliyeanza akiwa painia msaidizi. Ni kitu gani ambacho kimesaidia wahubiri hawa waingie katika utumishi wa painia?
Dak. 15: Mahitaji ya kwenu. Ikiwa hakuna uhitaji hususa, mwangalizi msimamizi au mwangalizi wa utumishi anaweza kutoa ripoti yenye kutia moyo na hotuba kuhusu maendeleo ya huduma ya mahali penu. Tia ndani maelezo kuhusu uenezaji wa eneo, wastani wa saa, mafunzo yanayoongozwa, na mafunzo mapya yaliyoanzishwa, hesabu ya wale ambao wamepainia kufikia wakati huu katika mwaka wa utumishi, na kadhalika. Sifu akina ndugu kwa kazi nzuri inayofanywa. Pia, mhubiri aliyejitayarisha vizuri atoe wonyesho linaloonyesha jinsi ya kutoa toleo la kichapo la sasa katika huduma ya nyumba kwa nyumba.
Wimbo 25 (151) na sala ya kumalizia.
JUMA LINALOANZA JUNI 13
Wimbo 10 (32)
Dak. 10: Matangazo ya kwenu na Matangazo yaliyochaguliwa kutoka Huduma ya Ufalme Yetu. Ripoti ya hesabu. Toa maneno ya uthamini kwa utegemezo wa kifedha wa kundi. Tia ndani barua ya shukrani kutoka kwa Sosaiti kwa michango yo yote iliyopelekwa na kundi.
Dak. 20: “Kutangaza Habari Njema—Nyumba kwa Nyumba.” Maswali na majibu. Toa kielezi cha jambo kuu lililoelezwa kwenye fungu la 3 kwa jambo fupi lililoonwa mahali penu. Baada ya kuzungumzia fungu 4, mhubiri mmoja au wawili waliojitayarisha waeleze jinsi wao binafsi wamenufaika kutokana na kushiriki katika huduma ya nyumba kwa nyumba. Watie moyo wahubiri wote kuwa na wakati ulioratibiwa kila juma kwa ajili ya kutoa ushuhuda nyumba kwa nyumba kwa kutumia toleo la kichapo la kawaida.
Dak. 15: “Vuka Uje Makedonia.” Hotuba. Rekebisha habari ilingane na hali za mahali penu. Kazia uhitaji wa wazee wenye madaraka kuratibu uenezaji wa eneo.
Wimbo 27 (53) na sala ya kumalizia.
JUMA LINALOANZA JUNI 20
Wimbo 9 (26)
Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Habari za Kitheokrasi.
Dak. 20: “Hotuba ikizungumzia makala “Upainia Msaidizi—Mlango wa Kuelekeza Kwenye Utendaji Mkubwa Zaidi” kutoka Huduma ya Ufalme Yetu ya Juni 1987.
Dak. 15: “Maisha na Huduma ya Yesu.” Hotuba changamfu pamoja na vielezi kuhusu njia ya kutumia mfululizo huu wa makala katika Mnara wa Mlinzi. Je! wazazi wanatumia makala hizi kusaidia watoto wakue katika upendo kwa Yesu na kuthamini kile ambacho yeye alifanya kwa aina ya binadamu? Watu wazima pia wananufaika kwa kufikiria makala hizi. Simulia mambo yaliyoonwa kwa kutumia makala hizi jinsi wakati unavyoruhusu.
Wimbo 1 (21) na sala ya kumalizia.
JUMA LINALOANZA JUNI 27
Wimbo 96 (71)
Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Mawonyesho mawili au matatu mafupi kuhusu utoaji wa magazeti unaofaa kwa ajili ya Jumamosi hii au siku ya soko inayofuata. Simulia mambo yaliyoonwa yaliyotangulia kuchaguliwa yakikazia uangushaji wa vitabu Kuokolewa na Furaha nyumba kwa nyumba.
Dak. 20: “Pata Manufaa za Kitabu Reasoning.” Mazungumzo pamoja na wasikilizaji. Tia ndani mambo yaliyoonwa mafupi ya mahali penu kutoa kielezi juu ya matumizi yaliyodokezwa ya kitabu Reasoning. Wahubiri waeleze jinsi wamefanyia maendelea huduma yao kwa kutumia kitabu Reasoning katika utumishi wa shambani, jinsi wakati unavyoruhusu.
Dak. 15: “Vijana Wanauliza . . . ” Mzee anasimamia mazungumzo yanayofanywa na vijana kadhaa wenye kielelezo kizuri juu ya thamani ya makala hizi katika Amkeni! Wanaweza kutia ndani maelezo kuhusu jinsi wamenufaika kibinafsi au jinsi wametumia makala hizo kuwasaidia wengine.
Wimbo 20 (46) na sala ya kumalizia.