Habari za Kitheokrasi
◆ Burma ilikuwa na kilele kipya cha wahubiri 1,552 katika Januari. Lilikuwa jambo zuri kuona 2,216 katika hadhirina na 58 walibatizwa kwenye “Tumaini Katika Yehova” Mikusanyiko yao ya Wilaya minne.
◆ Kilele cha wahubiri 122,608 kiliripotiwa na Jamhuri ya Muungano wa Ujeremani kwa Januari. Utendaji wa funzo la Biblia unaendelea kuongezeka upesi, kukiwa na kilele kipya cha 60,566.
◆ Kisiwa cha Guam kilifikia kilele kipya cha wahubiri 278 wakati wa Januari, ongezeko la asilimia 8 zaidi ya wastani wa mwaka uliopita.
◆ Ailandi iliripoti kilele cha wahubiri cha tano mfululizo kikiwa na 2,795 katika Januari. Wahubiri wa kundi walifikia wastani wa saa 13.2 shambani.
◆ Madagaska ilikuwa na ongezeko la asilimia 14 katika Januari ikiwa na kilele kipya cha wahubiri 2,764. Wahubiri wa kundi walifikia wastani wa saa 13.6, ziara za kurudia 7.4, na mafunzo ya Biblia 1.6.
◆ Afrika Kusini ilikuwa na kilele kipya cha wahubiri 43,184 kwa Januari, ongezeko la asilimia 7 zaidi ya wastani wa mwaka uliopita.
◆ Trinidadi ilikuwa na kilele kipya cha wahubiri 5,116 katika Januari kwa ongezeko la asilimia 9.
◆ Kilele cha Venezuela cha wahubiri 40,001 kwa Januari kinawakilisha ongezeko la asilimia 11 zaidi ya wastani wa mwaka uliopita.
◆ Zimbabwe ilikuwa na kilele kipya cha wahubiri 15,935 katika Januari na kilele kipya cha mafunzo ya Biblia 15,206.
◆ Makusanyiko mawili ya mzunguko yalimalizika hivi karibuni katika Uganda yakiwa na hadhirina iliyounganishwa ya 1,142 na 36 walibatizwa.
◆ Programu ya siku ya Pekee ya Kusanyiko katika Tanzania ilimalizika kwa mafanikio wakati wa Aprili. Jumla ya 4,320 walihudhuria hotuba ya watu wote na 44 wakabatizwa.