Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 7/88 kur. 1-2
  • Kunena Neno la Mungu Kwa Ujasiri

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Kunena Neno la Mungu Kwa Ujasiri
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1988
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • KUTWAA FURSA ZA KUNENA
  • TOA TOLEO KWA UJASIRI
  • ‘Sema Neno la Mungu kwa Ujasiri’
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2010
  • Je, Wahubiri kwa Ujasiri?
    Huduma Yetu ya Ufalme—2000
  • Mwige Yesu—Hubiri Kwa Ujasiri
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2009
  • Endelea Kusema Neno la Mungu kwa Ujasiri
    Huduma ya Ufalme—2005
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—1988
km 7/88 kur. 1-2

Kunena Neno la Mungu Kwa Ujasiri

1 Wewe unathiriwa jinsi gani unapokabili upinzani au unaponyanyaswa na maadui wa habari njema? Je! wewe unapiga moyo konde ili uendelee kutoa ushuhuda hata wapinzani waseme au wafanye nini? Ijapokuwa ni wachache ambao huenda wakaacha moyo wao ulegee au washawishiwe kuacha kuhubiri, sisi sote tunaweza kunufaika kutokana na kielelezo cha Paulo na Sila. Wao hawakuacha mnyanyaso uwavunje moyo au kuwanyamazisha. Paulo aliandika hivi: “Baada ya sisi kuteseka kwanza na kutendwa kwa ufidhuli . . . , sisi tulijipa ujasiri kupitia kwa Mungu wetu ili tunene habari njema kwenu ninyi.” (1 The. 2.2, NW) Waliweza kuendelea kuhubiri kupitia kwa imara kutoka kwa Yehova. (Zab. 138:3) Kwa msaada wa Yehova, sisi pia tunaweza kuonyesha ujasiri unaohitajiwa ili tuwe washindi tunapokabili upinzani.

2 Yehova ni kimbilio letu wakati wa taabu. Tunaomba yeye msaada kwa unyenyekevu. (Zab. 18:2, 3) Ndugu zetu katika karne ya kwanza waliomba Yehova awasaidie ‘waendelee kunena lake neno kwa ujasiri wote.’ (Mdo. 4:29, NW) Yehova alijibu sala hiyo kwa kuwajaza wale wanafunzi roho takatifu. Yeye atafanya vivyo hivyo kwetu sisi.—Mdo. 4:31.

KUTWAA FURSA ZA KUNENA

3 Katika kila kundi, mikutano ya utumishi wa shambani imepangwa ili kuandaa mazungumzo yenye kutia moyo ya mambo ya kiroho kabla ya kwenda kwenye eneo. Je! wewe unaunga mkono mikutano hii inapowezekana? Ikiwa ndivyo, utajengwa unapojitahidi kuwatia imara wengine pia. Tunapokuwa katika utumishi wa shambani, kuna fursa zaidi za kusaidia na kutia moyo mmoja na mwingine. Mapainia pamoja na wale ambao wanaweza kutumia wakati mwingi katika huduma huenda hasa wakaweza kuwapa wahubiri wengine manufaa ya ujuzi wao wanapoenda mlango kwa mlango. Kwa kutumia madokezo kutoka kitabu Reasoning, wote wanaweza kujiandaa ili wanene kwa usadikisho.

4 Katika maeneo fulani, akina ndugu wanapata kwamba watu wengi hawamo nyumbani wakati wa mchana. Njia mbalimbali zinaweza kutumiwa ili kuwafikia watu hao. Wahubiri fulani wanafanya kazi ya barabarani karibu na vituo vya basi na stesheni za gari-moshi au mbele ya nyumba za ghorofa saa ambazo watu wanaondoka kwenda kazini au kuja nyumbani. Wengine wanachukua hatua ya kwanza ili wanene na watu wanaoketi katika magari yao. Katika eneo moja akina dada wawili waliokuwa wakitoa ushuhuda kwa kutumia njia hii waliangusha magazeti 50 kwa muda ulio punde ya saa moja.

5 Mahali ambako vichapo vinaangushiwa watu walio katika mahali pa hadhara, unaweza kuchukua anwani yao ya nyumbani na kufanya mipango ya ziara za kurudia na mafunzo ya Biblia. Inahitaji uhodari na ujasiri kuwaendea watu usiowajua na kuanzisha mazungumzo pamoja nao, lakini matokeo yanaweza kuwa yenye kuthawabisha sana. Kama vile ilivyokuwa kwa mitume, ni jambo linalohitajiwa sana kunena “kwa ujasiri kwa mamlaka ya Yehova.”—Mdo. 14:3, NW.

6 Watu fulani wanapanga kufanyia kazi eneo lisilogawiwa mtu au lisilofanyiwa kazi kwa ukawaida, na jambo hili pia linahitaji ujasiri. Wakati wa miezi ya Julai mpaka Septemba mwaka huu, akina ndugu na dada wengi watashiriki katika kazi hii. Wengine watasafiri kilometa nyingi. Ni furaha kuona akina ndugu wakishiriki katika utendaji huu kwa hiari hata kwa kujidhabihu sana kibinafsi.

TOA TOLEO KWA UJASIRI

7 Wakati wa Julai toleo la kichapo ni Kuokolewa Kuingia Katika Dunia Mpya au Furaha—Namna ya Kuipata. Vichapo vyote hivi viwili vina habari za muhimu kwa wale ambao wanaona njaa na kiu cha ukweli. Toa vitabu hivi ukiwa na uhakika, ukitumia Kichwa cha Mazungumzo cha sasa. Rejeza kwenye kitabu Reasoning kwa utangulizi ambao utafaa katika eneo lenu.

8 Paulo alipokaribishwa na Yesu mara ya kwanza ili awe mfuasi wake, yeye aliitikia kwa bidii na kuhubiri kwa ujasiri. (Mdo. 9:5, 15, 16, 20, 27, 28) Yeye aliendelea kwa imani katika mwendo huo huo mpaka kifo chake. Sisi tunahitaji kuiga kielelezo chake na kuendelea kushiriki katika kazi ya kunena Neno la Mungu kwa ujasiri.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki