Kusaidia Wengine Watumikie Yehova kwa Nafsi Nzima
1 Kwa haki Yehova anataka kwamba kila mmoja wetu atumikie yeye kwa nafsi nzima. (Marko 12:30; Kol. 3:23) Ijapokuwa tuna uwezo unaotofautiana, sisi tukiwa watu mmoja mmoja tunataka kufanya yote tuwezayo katika kutumikia yeye.—Mt. 13:23.
2 Je! tunaweza kuwasaidia zaidi watoto wetu katika jambo hili? Je! kuna njia ambazo katika hizo tunaweza kutoa kitia-moyo zaidi kwa wale ambao sisi tunaongoza mafunzo ya Biblia pamoja nao? Je! kuna wengine katika kundi ambao wanaweza kufanyia maendeleo ubora au kiasi cha utumishi wao ikiwa sisi tunawapa msaada fulani wenye mafaa?
JINSI YA KUSAIDIA
3 Kuna hesabu fulani ya watu ambao wamekuwa wakihudhuria mikutano yote ya kundi kwa ukawaida. Wengine hata wamestahili kuanza kushiriki katika utumishi wa shambani. Hilo ni jambo la kusifika. Hata hivyo, si wote wameamua kujiweka wakfu na kubatizwa. Je! tunaweza kuwasaidia katika jambo hilo? Je! tumezungumza kibinafsi pamoja nao kutoka moyoni? Huenda ikawa kwamba kurudia kwa unyoofu na kwa fadhili makala “Ni Nini Kinachonizuia Nisibatizwe?” kwenye kurasa 19-24 za Mnara wa Mlinzi wa Februari 15, 1982 kutasaidia.
4 Pia kuna wale ambao wamebatizwa lakini hawajifanyi wapatikane kwa ajili ya mapendeleo kulingana na uwezo na hali zao. Huenda wengine wakawa wahubiri wa kawaida ambao wanafanya upainia msaidizi mara kwa mara. Je! wanaweza kufanya marekebisho yanayohitajiwa ili wawe mapainia wasaidizi wa kawaida? Je! inawezekana kwa wengine ambao ni mapainia wasaidizi wa kawaida kuwa mapainia wa kawaida? Nyakati nyingine, maneno yenye kusihi pamoja na madokezo machache yanayofaa kutoka kwa mzazi, mzee, au mmoja ambaye anatumikia akiwa painia wa kawaida yatasukuma watu wa namna hiyo kutumikia kwa kadiri kamili ambayo uwezo na hali zao zinaruhusu.—2 Tim. 4:2.
TOA KITIA-MOYO
5 Wengine wanaweza kustahili kuwekwa rasmi kama watumishi wa huduma au wazee baada ya kuitikia kitia-moyo kinachohitajiwa na “kufikia” mapendeleo hayo. (1 Tim. 3:1, NW) Kwa kutumia kwa faida msaada wenye mafaa unaotolewa kupitia Shule ya Huduma ya Kitheokrasi, watu fulani fulani wanaweza kuwa watoaji hotuba za watu wote wenye matokeo. Wazee fulani waseja na watumishi wa huduma wamesaidiwa kufanya marekebisho yanayohitajiwa ili kustahili kuhudhuria Shule ya Mazoezi ya Kihuduma au kutumikia katika makundi mengine ambamo uhitaji ni mkubwa zaidi. Je! wewe unaweza kufikiria mapendeleo mengine ambayo wengine katika jamaa yako au kundi wanaweza kustahili ikiwa wanapokea msaada fulani? Unaweza kuwasaidia katika njia gani?
6 Tunapaswa tumtolee Yehova utumishi bora zaidi tuwezao kumpa. (Ufu. 4:11) Tunataka kufanya mapenzi yake kwa nafsi nzima na kusaidia wengine wafanye vivyo hivyo. (Efe. 6:6) Wale wanaoitikia msaada na kitia-moyo kuelekea kutumikia Yehova kwa nafsi nzima wanaweza kuwa na uhakika wa kwamba Yehova atawapa “ujira wa urithi.”—Kol. 3:24.