Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 10/88 uku. 8
  • Kutangaza Habari Njema—Kwa Ujasiri, Lakini kwa Busara

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Kutangaza Habari Njema—Kwa Ujasiri, Lakini kwa Busara
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1988
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • KUWA WENYE USAWAZIKO
  • VIELELEZO
  • Uwe Mwenye Busara Lakini Thabiti
    Faidika na Elimu ya Shule ya Huduma ya Kitheokrasi
  • ‘Sema Neno la Mungu kwa Ujasiri’
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2010
  • Je, Wahubiri kwa Ujasiri?
    Huduma Yetu ya Ufalme—2000
  • Mwige Yesu—Hubiri Kwa Ujasiri
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2009
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—1988
km 10/88 uku. 8

Kutangaza Habari Njema—Kwa Ujasiri, Lakini kwa Busara

1 Petro na Yohana walipoagizwa waache kuhubiri, wao walijibu: “Maana sisi hatuwezi kuacha kuyanena mambo tuliyoyaona na kuyasikia.” (Mdo. 4:20) Ni nini kilichowawezesha waseme kwa ujasiri hivyo? Wao ‘waliomba’ na ‘wakajazwa roho takatifu, wakanena neno la Mungu kwa ujasiri.’ (Mdo. 4:31) Hakika sisi pia tunaweza kutiwa ujasiri ili tuhubiri tukifuata kielelezo chao.

2 Lakini tunaweza kusema kwa ujasiri jinsi gani na wakati ule ule tuwe wenye busara? Fasili ya kamusi moja ya busara ni ‘hisi nyepesi ya jambo la kufanya au kusema ili kuepuka kutia uchungu.’ Kuwekea msingi jambo ambalo tutakubaliana sote kunaweza kutuwezesha tuwe wenye busara. Kujifunza jinsi ya kusababu pamoja na watu kutatusaidia pia tuwe wenye busara. Ni kifaa gani kilicho bora zaidi tunachoweza kutumia kuliko Reasoning From the Scriptures ili kitusaidie tuwe wenye ujasiri na wenye busara.

KUWA WENYE USAWAZIKO

3 Kudumisha usawaziko kati ya ujasiri na busara ni jambo la maana ili kutimiza kazi ya kuhubiri kwa mafanikio. Mathalani, tunaweza kuwazungumzia jinsi gani wale wanaozusha swali, ‘Je! si kweli kwamba kuna wema katika dini zote?’ Jibu la moja kwa moja lakini lenye busara linapatikana kwenye ukurasa 323 wa kitabu Reasoning. Pia, ikiwa mtu anazusha swali juu ya kwa nini sisi tunawatembelea kwa kurudia-rudia watu ambao si Mashahidi wa Yehova na wana imani yao wenyewe, tunaweza kutoa jibu kwa ujasiri lakini kwa busara kama inavyoonyeshwa kwenye ukurasa 206 wa kitabu Reasoning. Watu fulani wanauliza kwa nini Mashahidi wa Yehova hawahusiki katika mambo ili kusaidia kufanya mtaa wao uwe mahali pazuri zaidi pa kuishi. Habari kadha wa kadha zimetolewa kwenye kurasa 207 na 208 ambazo zitatuwezesha tunene kwa ujasiri lakini kwa busara.

VIELELEZO

4 Petro alisema kwamba twapaswa ‘kuwa tayari sikuzote kumjibu kila mtu aulizaye habari za tumaini lililo ndani yetu.’ Kisha yeye aliongezea kwamba tufanye hivyo ‘kwa upole na kwa hofu.’ (1 Pet. 3:15) Ndiyo, Petro alitambua uhitaji wa kuwa na ujasiri lakini pia kutumia busara. Mafanikio waliyopata wahubiri waliofuata njia hii yameripotiwa katika vichapo vya Sosaiti.—wSW86 4/1 kur. 6-7; wSW86 8/1 kur. 21, 24; yb87 kur. 53-4.

5 Kutegemea Yehova katika sala, kama vielelezo vingi vinavyokazia, kutatuwezesha tupokee msaada wa roho takatifu, tuimarishwe hivyo tunene kwa ujasiri na busara.—Mdo. 5:29.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki