Maandikisho
1 Maandikisho ya Mnara wa Mlinzi na Amkeni! yamewasaidia watu wengi wafahamiane na Neno la Mungu. Tunaweza kufanya nini ili tuhakikishe kwamba waandikishaji wanaendelea kupata utumishi bora iwezekanavyo?
2 Hatuwezi kukazia kupita kiasi usahihi wa kujaza karatasi za uandikishaji. Maendeleo mazuri yamepatikana katika eneo hili. Hata hivyo, tatizo linaloendelea kukua linatokea wakati mwandikishaji anapohama. Mara nyingi Sosaiti haipashwi habari mara moja na utumishi wa uandikishaji unakatizwa.
3 Utumishi wa posta unarudisha magazeti yote ambayo hayakupokewa na wenyewe kwa malipo kwa kila moja. Katika 1987 Sosaiti ililazimika kutumia maelfu ya dola ili kulipia gharama za posta kwa magazeti haya yaliyorudishwa ambayo hayakupokewa na wenyewe. Yaliyo mengi ya hayo yalirudishwa kwa sababu mwandikishaji alikuwa amehama. Ili anwani ya maandikisho ya Mnara wa Mlinzi au Amkeni! ibadilishwe, lazima fomu ya Sosaiti ya Badiliko la Anwani ya Uandikishaji (M-205) ipelekwe ili kutoa anwani mpya. Msaada wako katika kupata anwani ya posta mpya iwezekanapo utasaidia Sosaiti ipunguze gharama zayo.
4 Vikaratasi vyote vya Maandikisho Yanayokwisha vyapaswa kushughulikiwa mara moja. Wahubiri wanatiwa moyo wafuatie mara moja uandikisho unaofanywa upya na kupelekea ndugu anayeshughulikia uandikishaji. Maandikisho yote mapya na yanayoandikishwa upya tena yanayopokewa na watu wasiobatizwa yangeweza kuripotiwa na mhubiri. (Ona Huduma Yetu, ukurasa 102.) Hata hivyo, ni jambo lenye msaada kwa Sosaiti ikiwa maandikisho yanayofanywa upya yanapelekwa mapema iwezekanavyo. Maandikisho yote yanapaswa yapelekwe kwa Sosaiti kila juma.