Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 6/89 uku. 1
  • Piga Mbiu Kuhusu Amani na Usalama wa Kweli

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Piga Mbiu Kuhusu Amani na Usalama wa Kweli
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1989
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • GAWANYA KITABU AMANI YA KWELI
  • Kutangaza Habari Njema-Kwa Kitabu Amani ya Kweli
    Huduma Yetu ya Ufalme—1989
  • KIchwa cha Mazungumzo
    Huduma Yetu ya Ufalme—1989
  • Kichwa cha Mazungumzo
    Huduma Yetu ya Ufalme—1989
  • Amani ya Kweli—Kutoka Chanzo Gani?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1997
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—1989
km 6/89 uku. 1

Piga Mbiu Kuhusu Amani na Usalama wa Kweli

1 Amani na usalama wa kweli unaweza kutoka kwa chanzo kimoja tu, Yehova Mungu. Mika anatujulisha kwamba Yehova “atafanya hukumu kati ya watu wa kabila nyingi, naye atawakemea mataifa wenye nguvu.” Tokeo ni nini? “Taifa halitainua upanga juu ya taifa lingine, wala hawatajifunza vita tena kamwe.”—Mika 4:3.

2 Kwa kuwa Yehova ndiye chanzo pekee cha amani ya kweli, watu wanahitaji ‘kwenda juu mlimani kwa Yehova,’ na kuagizwa juu ya njia zake ili watembee katika vijia vyake. (Mika 4:2) Wao watajifunza kwamba Yehova Mungu ataleta amani ya kweli duniani kupitia Ufalme wake. Lakini tunaweza kusaidiaje watu zaidi wajifunze juu ya Chanzo cha amani na usalama wa kweli?

GAWANYA KITABU AMANI YA KWELI

3 Kitabu Amani ya Kweli kina habari za wakati unaofaa kwa watu wanaotaka ‘kwenda juu mlimani kwa Yehova.’ Daktari mmoja anayeishi Finland alipokea nakala ya kitabu Amani ya Kweli. Yeye hakukisoma wakati huo bali alikiweka kwenye rafu ya vitabu. Baadaye mke wake alikumbuka kwamba walikuwa na kitabu hicho kisha akakisoma chote. Mara akasadikishwa kwamba alikuwa amepata ukweli. Alianza kujifunza na baadaye mume wake alijiunga pamoja naye. Sasa wamebatizwa, na watoto wao pia ni wahubiri wa habari njema. Ono hili linaonyesha thamani ya kukiacha kitabu Amani ya Kweli katika nyumba nyingi iwezekanavyo.

4 Kujitayarisha kwetu kwa ajili ya utumishi wa shambani kunapasa kutia ndani pitio la yaliyomo na sura za kitabu ambazo tunafikiria zitavutia watu. Tunaweza kuchagua mambo hususa kutoka katika kitabu ambayo tunaweza kutumia katika mazungumzo pamoja na wenye nyumba.

5 Unaweza kujaribu dokezo lifuatalo. Baada ya kusoma na kuzungumzia maandiko yaliyo katika Kichwa cha Mazungumzo, elekeza fikira ya mwenye nyumba kwenye ukurasa 8 wa kitabu Amani ya Kweli. Wakati ukiruhusu, fungua mengine ya maandiko yaliyotajwa kuonyesha tofauti kati ya yale ambayo Ufalme wa Mungu utafanya na yale ambayo viongozi wa kibinadamu hawawezi kufanya. Kisha soma fungu 13. Baadaye, unaweza kumwuliza mwenye nyumba ikiwa angependa kuzungumzia habari fulani katika sura inayofuata. Kwa njia hii, funzo la Biblia linaweza kuanzishwa mara hiyo. La sivyo, jaribu kuanzisha funzo unapofanya ziara ya kurudia.

6 Ni wazi kwamba wanadamu wasiokamilika hawawezi kuleta amani na usalama wa kweli. Ili kuwa na tumaini imara kwa wakati ujao, lazima watu waweke imani yao katika Mungu. Lakini “wamwaminije yeye wasiyemsikia? Tena wamsikieje pasipo mhubiri?” (Rum. 10:14) Wakati wa watu kuwa na fursa ya kugeukia Chanzo halisi cha amani na usalama wa kweli unamalizika. Na tufanye yote tuwezayo katika mwezi wa Juni ili kupiga mbiu kuhusu ujumbe wa amani ya kweli kwa watu wengi wenye mioyo yenye ufuataji haki katika eneo la kundi.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki