Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 1/90 kur. 1-3
  • Kaa Chonjo Kutoa Fasihi za Biblia

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Kaa Chonjo Kutoa Fasihi za Biblia
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1990
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • NYUMBA KWA NYUMBA
  • USHAHIDI WA VIVI HIVI
  • Je! Wewe Unathamini Fasihi Yetu?
    Huduma Yetu ya Ufalme—1992
  • Kutangaza Habari Njema Kupitia Mafunzo ya Biblia
    Huduma Yetu ya Ufalme—1990
  • Kutoa Vichapo Katika Eneo Lenye Lugha Mbalimbali
    Huduma Yetu ya Ufalme—2003
  • Tumia kwa Hekima Vichapo Vyetu Vinavyotegemea Biblia
    Huduma ya Ufalme—2005
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—1990
km 1/90 kur. 1-3

Kaa Chonjo Kutoa Fasihi za Biblia

1 Tunashukuru kama nini kwa ajili ya fasihi za Biblia ambazo Yehova anaandaa kwa ukawaida kupitia tengenezo lake! Tunathamini sana chakula hicho cha kiroho. Tukiisha pokea kichapo kipya tunafungua kurasa zacho kwa hamu. Halafu, tunapokisoma kwa uangalifu, tunapata uelewevu. Uthamini wetu kwa ajili ya Yehova na makusudi yake unakua.

2 Faida za kibinafsi tunazopata zinatusukuma tukashiriki na wengine mambo mema tuliyojifunza. (Mt. 24:14) Tunahangaikia kufikisha vichapo vya Sosaiti mikononi mwa watu wengi iwezekanavyo. Hiyo inawawezesha wao pia wajifunze kweli zilizomo ndani ya vichapo hivyo vya Biblia vyenye kuagiza. Kama tumejitayarisha vizuri na kuwa chonjo kuchukua hatua ya kwanza kutoa toleo la fasihi la wakati huu, huenda tukaweza kusaidia watu wengine wenye mioyo myeupe wamgeukie Yehova na kujiunga nasi katika utumishi wake.

NYUMBA KWA NYUMBA

3 Wakati wa Januari na Februari tutakuwa tukitoa vitabu mbalimbali vya kurasa 192 kwa nusu ya bei ya kawaida. Vitabu vitakavyotolewa ni kutia ndani kitabu chochote cha kurasa 192 kilichotangazwa kwa chapa kabla ya 1980 isipokuwa Maisha ya Jamaa, Mwalimu Mkuu, Uzima Huu, Kweli, na Ujana. Makundi ambayo hayana vitabu hivi akibani yaweza kutoa kitabu Usalama Ulimwenguni Pote.

4 Nyakati nyingine tunapozuru watu wanakuwa wenye shughuli nyingi kikweli. Chini ya mastakimu hizo, huenda ikafaa kutoa tu kitabu kama ilivyodokezwa kwenye kielelezo cha pili kwenye ukurasa wa 20 wa kitabu Reasoning. Au huenda ikafaa tuseme kwa maneno yetu wenyewe jambo linalofanana na kielelezo cha tatu kwenye ukurasa huo, tukionyesha tunaelewa na hali ya mwenye nyumba na kusema hivi kwa njia ya kumvutia: “Lakini kwa kuwa huna wakati wa kuongea sasa, tunadokeza kwamba ukubali magazeti haya mawili kwa mchango wa _________ kisha uyasome ikufaapo zaidi. Utaona shangwe kujifunza juu ya ahadi ya Mungu ya kitu fulani kipya.” Mifikio hiyo inaonyesha kufikiria mastakimu za mwenye nyumba, na wakati ule ule, fasihi inatolewa.

5 Yaweza kufanywa nini ikiwa tayari mtu ana kichapo tunachotoa? Mbona usitumie kanuni ya Biblia inayopatikana kwenye 1 Wakorintho 3:6-9? Tayari mbegu imekwisha pandwa. Tumia vizuri fursa hiyo kunyunyiza maji kwa kumtolea mtu huyo ushahidi zaidi. Au huenda tukasema jambo kama hili: “Nimependezwa sana kwamba tayari una nakala ya kichapo hiki. Bila shaka umeona shangwe kukisoma. Kama ukiniruhusu, ningependa kukuonyesha jinsi unavyoweza kunufaika zaidi na kitabu hiki. Itachukua dakika chache tu.” Halafu toa wonyesho wa jinsi tunavyojifunza Biblia kwa msaada wa kichapo. Kusudi letu kwenye mlango halibadiliki wakati mwenye nyumba tayari ana kitabu hicho. Kumbuka, lengo letu la msingi ni ‘kufanya wanafunzi.’—Mt. 28:19.

USHAHIDI WA VIVI HIVI

6 Pia tunapaswa kuwa chonjo kuona fursa nyingi tunazoweza kuwa nazo za kutoa fasihi katika ushahidi wa vivi hivi. Fikiria njia za kutoa ushahidi kwa wageni, watu wa ukoo, wafanya kazi wenzi, wanashule wenzi, watu tunaokutana nao tunapoenda dukani, na wale tunaokutana nao katikati ya nyumba au milango tunapokuwa katika utumishi wa shambani. Panga kimbele, ukiwa na fasihi ambayo ipo ili uitoe katika pindi hizo wakati wowote iwezekanapo. Pindi nyingi, si vigumu kuchukua kichapo kimoja au zaidi kati ya vile vidogo. Wema mwingi waweza kutimizwa kupitia kutoa ushahidi wa vivi hivi.—1 Pet. 3:15.

7 Tengenezo la Yehova limetupa kwa ukarimu ugavi wa fasihi za kutuendeleza kuwa wenye nguvu kiroho na kutusaidia katika kueneza habari njema. Kuwa chonjo kuona fursa za kutoa fasihi za Biblia kutatusaidia tutukuze jina la Yehova.—Zab. 34:3.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki