Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 11/92 uku. 1
  • Je! Wewe Unathamini Fasihi Yetu?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Je! Wewe Unathamini Fasihi Yetu?
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1992
  • Habari Zinazolingana
  • Tumia kwa Hekima Vichapo Vyetu Vinavyotegemea Biblia
    Huduma ya Ufalme—2005
  • Kutoa Vichapo Katika Eneo Lenye Lugha Mbalimbali
    Huduma Yetu ya Ufalme—2003
  • Kuthamini Vitabu Vyetu
    Huduma Yetu ya Ufalme—2003
  • Sanduku la Swali
    Huduma Yetu ya Ufalme—2011
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—1992
km 11/92 uku. 1

Je! Wewe Unathamini Fasihi Yetu?

1 Almasi na vito vinginevyo ni vyenye thamani si kwa sababu ya uzuri wavyo tu bali pia kwa sababu ya gharama kubwa ya kuvipata na kuvichimbua. Maarifa juu ya Yehova na Yesu Kristo ni yenye thamani kubwa hata zaidi, na vichapo vyetu ndivyo pekee ulimwenguni vinavyoeleza juu ya thamani hiyo kubwa ya kiroho kwa kina sana na kwa hekima ya kimungu. (Rum. 11:33; Flp. 3:8) Tunaweza kuonyeshaje uthamini wa kweli kwa ajili ya fasihi yetu?

2 Kununua wakati wa kusoma na kujifunza fasihi yetu kibinafsi na kama familia huonyesha tunathamini chakula kingi cha kiroho ambacho Yehova huandaa kwa ukawaida. Kichapo kipya kinapotolewa, sisi hupata nakala upesi na kuisoma tupatapo fursa ya kwanza. Tuna uhakika hivyo ndivyo itakavyokuwa kuhusu kitabu kipya “Kila Andiko” kinachopatikana sasa katika Kiswahili. Vivyo hivyo, tutasitawisha zoea zuri la kusoma kila nakala ya magazeti yetu kuanzia jalada hadi jalada. Tunajua pia kwamba mtatia kila jitihada kuandalia kila mshiriki wa familia anayeweza kusoma nakala yake mwenyewe ya vichapo vinavyohitajiwa kwa ajili ya funzo la kundi. Na hata watoto wadogo wanaweza kufunzwa staha ifaayo kwa vichapo vyetu, wakijifunza katika umri mchanga jinsi ya kufungua kurasa na kuepuka kuharibu vichapo hivyo vyenye thamani. Tunapojifunza Biblia kwa ukawaida kwa vichapo hivyo, tunapata kumjua Yehova vema zaidi, tunapata kujua jinsi unabii unatimizwa na kujifunza kuishi maisha bora zaidi.

3 Pia, katika utumishi wa shambani, fasihi yetu haina kifani. Hatuwezi kukumbuka yote tunayosoma, wala hakuna wakati wa kuyazungumza yote milangoni, kwa hiyo kweli inapatikana kwa wengine kupitia vichapo. Mwenye nyumba anaweza kuvisoma wakati inapomfaa na wengi wamejifunza kweli kwa njia hiyo.

4 Inaripotiwa kwamba katika baadhi ya makundi, hesabu kubwa ya magazeti hurundamana, yanazeeka na hivyo hayatumiwi kamwe. Tunataka tuepuke kutumia vibaya fasihi. Fasihi inayoachwa kwenye rafu katika Jumba la Ufalme au nyumbani mwetu haitimizi kusudi layo, na thamani yayo haipatikani. Kwa hiyo, tuwe na mradi wa kuagiza magazeti ya kutosha lakini si zaidi ya tunayohitaji. Kila mhubiri apaswa aagize kiasi anachoona kuwa kinafaa kwa matumizi yake, halafu ikiwa anayaangusha upesi, nyakati zote anaweza kutumia fasihi nyingineyo. Wazee, hasa mwangalizi wa utumishi na ndugu wanaoshughulikia magazeti, wanapaswa wawe macho kuona uhitaji wa wahubiri na kurekebisha agizo kupatana na yanayotumika. Ikiwa magazeti hayaangushwi kwa sababu ya kusanyiko au hali mbaya ya anga, basi wote wanaweza kutiwa moyo kutia jitihada za pekee kuyatumia juma linalofuata au punde baadaye na hivyo kuyapelekea watu ambao huenda wakataka kuyasoma.

5 Nyakati zote fikiri kwa uangalifu ni kiasi gani cha fasihi unachohitaji hasa kwa makusudi ya ugawanyaji. Uamuzi mzuri unahitajika. Ingawa kiasi cha kutosha kinafaa, hasa ikiwa unapainia, hakuna haja ya kudumisha ugavi mkubwa wa fasihi ya kibinafsi, kwa kuwa kiasi zaidi chaweza kupatikana kwenye Jumba la Ufalme kabla na baada ya mikutano. Jipatie mwenyewe fasihi ya kutosha kuanzisha mwezi na upate nyinginezo zaidi ugavi wako unapotumika.

6 Vichapo vyetu ni vyenye thamani kubwa zaidi vinapoangushiwa watu wanaothamini kweli ya Neno la Mungu. Sisi sote na tuwe wenye hekima na utambuzi katika kutumia yale ambayo tumeandaliwa, hivyo tukionyesha jinsi tunavyothamini sana fasihi yetu.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki