Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 12/11 uku. 2
  • Sanduku la Swali

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Sanduku la Swali
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2011
  • Habari Zinazolingana
  • Je! Wewe Unathamini Fasihi Yetu?
    Huduma Yetu ya Ufalme—1992
  • Tumia Machapisho ya Biblia kwa Hekima
    Daftari la Mkutano wa Huduma na Maisha Yetu ya Kikristo—2017
  • Tumia kwa Hekima Vichapo Vyetu Vinavyotegemea Biblia
    Huduma ya Ufalme—2005
  • Kutoa Vichapo Katika Eneo Lenye Lugha Mbalimbali
    Huduma Yetu ya Ufalme—2003
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—2011
km 12/11 uku. 2

Sanduku la Swali

◼ Tunawezaje kuamua ikiwa tutamwachia mtu machapisho?

Jambo lililo muhimu zaidi ni kutambua kama mtu anapendezwa. Ikiwa anapendezwa kikweli, tunaweza kumwachia magazeti mawili, broshua, kitabu, au machapisho mengineyo. Tunaweza kumwachia hata tukitambua kwamba ana kiasi kidogo cha pesa au hana pesa za kutoa mchango kwa ajili ya kazi ya ulimwenguni pote. (Ayu. 34:19; Ufu. 22:17) Hata hivyo, hatutawaachia watu wasiothamini machapisho yetu yenye thamani.—Mt. 7:6.

Mwenye-nyumba anaweza kuonyeshaje kwamba anapendezwa? Kwa kuwa tayari kuzungumza nasi. Kusikiliza kwa makini tunapozungumza, kujibu maswali, na kutoa maelezo ni mambo yanayoonyesha kwamba anapendezwa na mazungumzo. Kufuatana nasi tunaposoma Biblia kunaonyesha kwamba anaheshimu Neno la Mungu. Nyakati nyingine ni vizuri kumuuliza ikiwa atasoma machapisho tunayompa. Wahubiri wanapaswa kutumia utambuzi ili kujua ikiwa mtu anapendezwa. Kwa mfano, tunapohubiri barabarani, halingekuwa jambo la busara kumpa kila mtu tunayekutana naye magazeti, broshua, au vitabu bila kujali. Ikiwa hatuwezi kutambua kama mtu anapendezwa, ingekuwa vema kumpa mwaliko wa kuhudhuria mikutano au kumwachia trakti.

Vilevile, kiasi cha machapisho ambacho mhubiri anachukua kwenye dawati la machapisho kinapaswa kulingana na kiasi anachohitaji kutumia katika huduma, bali si kulingana na uwezo wake wa kutoa michango. Michango haikusudiwi tu kulipia machapisho, bali kutegemeza sehemu zote za kazi yetu ya kuhubiri ulimwenguni pote. Hata hali yetu ya kifedha iweje, uthamini utatuchochea kutoa kwa ukarimu kutokana na uhitaji wetu bali si kutokana na ziada yetu, ili kuunga mkono kazi ya Ufalme. (Marko 12:41-44; 2 Kor. 9:7) Pia, uthamini utatuchochea kuchukua machapisho tunayohitaji tu, na hivyo kutotumia vibaya michango inayotolewa.

[Blabu katika ukurasa wa 2]

Wahubiri wanapaswa kutumia utambuzi ili kujua ikiwa mtu anapendezwa

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki