Sanduku la Swali
◼ Tunawezaje kuamua ikiwa tutamwachia mtu machapisho?
Jambo lililo muhimu zaidi ni kutambua kama mtu anapendezwa. Ikiwa anapendezwa kikweli, tunaweza kumwachia magazeti mawili, broshua, kitabu, au machapisho mengineyo. Tunaweza kumwachia hata tukitambua kwamba ana kiasi kidogo cha pesa au hana pesa za kutoa mchango kwa ajili ya kazi ya ulimwenguni pote. (Ayu. 34:19; Ufu. 22:17) Hata hivyo, hatutawaachia watu wasiothamini machapisho yetu yenye thamani.—Mt. 7:6.
Mwenye-nyumba anaweza kuonyeshaje kwamba anapendezwa? Kwa kuwa tayari kuzungumza nasi. Kusikiliza kwa makini tunapozungumza, kujibu maswali, na kutoa maelezo ni mambo yanayoonyesha kwamba anapendezwa na mazungumzo. Kufuatana nasi tunaposoma Biblia kunaonyesha kwamba anaheshimu Neno la Mungu. Nyakati nyingine ni vizuri kumuuliza ikiwa atasoma machapisho tunayompa. Wahubiri wanapaswa kutumia utambuzi ili kujua ikiwa mtu anapendezwa. Kwa mfano, tunapohubiri barabarani, halingekuwa jambo la busara kumpa kila mtu tunayekutana naye magazeti, broshua, au vitabu bila kujali. Ikiwa hatuwezi kutambua kama mtu anapendezwa, ingekuwa vema kumpa mwaliko wa kuhudhuria mikutano au kumwachia trakti.
Vilevile, kiasi cha machapisho ambacho mhubiri anachukua kwenye dawati la machapisho kinapaswa kulingana na kiasi anachohitaji kutumia katika huduma, bali si kulingana na uwezo wake wa kutoa michango. Michango haikusudiwi tu kulipia machapisho, bali kutegemeza sehemu zote za kazi yetu ya kuhubiri ulimwenguni pote. Hata hali yetu ya kifedha iweje, uthamini utatuchochea kutoa kwa ukarimu kutokana na uhitaji wetu bali si kutokana na ziada yetu, ili kuunga mkono kazi ya Ufalme. (Marko 12:41-44; 2 Kor. 9:7) Pia, uthamini utatuchochea kuchukua machapisho tunayohitaji tu, na hivyo kutotumia vibaya michango inayotolewa.
[Blabu katika ukurasa wa 2]
Wahubiri wanapaswa kutumia utambuzi ili kujua ikiwa mtu anapendezwa