Mikutano Ya Utumishi Kwa Novemba
Juma Linaloanza Novemba 2
Dak. 10: Matangazo ya kwenu na Matangazo yaliyoteuliwa kutoka Huduma ya Ufalme Yetu. Elekeza fikira kwenye habari iliyo katika kisanduku kuhusu anwani za ofisi za tawi. Pongeza wahubiri kwa sehemu wanayoshiriki katika kazi ya kuhubiri Ufalme. Dokeza mambo ya kuzungumzia katika magazeti ya karibuni ya kutumiwa katika eneo la kwenu.
Dak. 15: “Uwezo wa Neno la Mungu.” Maswali na majibu. Watie moyo wote wasome trakti Sababu Kwa Nini Wewe Unaweza Kuitumaini Biblia, wakichunguza sehemu zenye mambo yenye kutoa sababu na hoja sahili zenye nguvu ya kutumiwa katika utumishi wa shambani.
Dak. 20: “Weka Msingi Katika Ziara Yako ya Kwanza.” Ndugu anayeshughulikia sehemu hii atoa utangulizi wa maonyesho ya mojawapo matangulizi mawili yaliyotajwa katika mafungu 2 na 3 na maonyesho ya kila dokezo katika mafungu 4 na 5. Onyesho la fungu 2 lapaswa lionyeshe jinsi Biblia na pia kitabu Neno la Mungu yaweza kutolewa wakati kupendezwa kunapoonyeshwa katika ziara ya kwanza.
Wimbo 52 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Novemba 9
Dak. 5: Matangazo ya kwenu.
Dak. 15: “Je! Wewe Hufuata Maagizo?” Hotuba ikitolewa na mwangalizi msimamizi ikitegemea makala katika Mnara wa Mlinzi la Oktoba 1, 1990, kurasa 30-1. Utumizi wa kwenu wapaswa ufanywe kwa mahitaji hususa: kuripoti wakati wa utumishi wa shambani, kusafisha Jumba la Ufalme, kuwahi kwenye mikutano ya utumishi wa shambani, kudhibiti watoto kwenye Jumba la Ufalme, na kadhalika. Toa pongezi inapofaa, na uwasaidie wote watambue jinsi kundi lote hunufaika na jinsi kazi ya watumishi waliowekwa hurahisishwa kila mtu anapofuata maagizo.
Dak. 10: “Uwe Painia Msaidizi Katika Desemba.” Pitia habari kwa uchangamfu na idili kwa maswali na majibu. Tangaza mipango ya kwenu ya utumishi wa shambani na mipango ya pekee itakayofanywa ya vikundi vikubwa zaidi katika Desemba.
Dak. 15: “Je! Wewe Unathamini Fasihi Yetu?” Hotuba yenye kutia moyo.
Wimbo 27 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Novemba 16
Dak. 13: Matangazo ya kwenu, tia ndani ripoti ya hesabu na shukrani kwa upaji. Pongeza kundi kwa uchangamfu kwa utegemezo wa kifedha wa kundi lenu na pia kazi ya Sosaiti ya ulimwenguni pote.
Dak. 20: “Jinsi ya Kusitawisha Kupendezwa.” Hotuba na maonyesho, ikishughulikiwa na mwangalizi wa utumishi. Toa wonyesho wa njia zilizoonyeshwa katika fungu 5 na 6. Maonyesho yawe sahili na rahisi kufuata.
Dak. 12: “Chagua Mambo Yafaayo ya Kuzungumzia.” Mazungumzo kati ya mume na mke wakijitayarisha kwenda kwenye utumishi wa shambani.
Wimbo 198 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Novemba 23
Dak. 10: Matangazo ya kwenu.
Dak. 15: “Kufuata Binafsi Kanuni za Afya.” Hotuba Ikitegemea Mnara wa Mlinzi la Juni 1, 1989, kurasa 16, 17, mafungu 6-10. Fanya habari ifae kundi lenu na ukazie umaana wa kujizoeza madokezo hayo kwenye mikusanyiko ya wilaya na programu za kusanyiko la mzunguko na la siku ya pekee.
Dak. 20: Sababu Kwa Nini Sisi Hatusherehekei Siku za Kuzaliwa. Mazungumzo kati ya mzee na mvulana asiye na baba ambaye bado si tineja na ambaye ni mfano mzuri. Mvulana amwendea mzee kumwuliza msaada wake katika kushughulika na msongo kutoka kwa marika zake ili ahudhurie karamu ya siku ya kuzaliwa. Yeye anaelewa kuwa haifai lakini angependa aweze kueleza wengine waziwazi. Kwa fadhili na maneno sahili, mzee apitia na mvulana huyo habari iliyo katika kurasa 30-1 katika Mnara wa Mlinzi la Septemba 1, 1992, na kurasa 356-8 za kitabu Kutoa Sababu.
Wimbo 24 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Novemba 30
Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Toa wonyesho wa jinsi jambo la kuzungumzia kutoka kwa gazeti la karibuni laweza kutumiwa mwisho-juma huu.
Dak. 20: “Yule Mtu Mkuu Zaidi Aliyepata Kuishi.” Ipitiwe kwa maswali na majibu. Unapopitia fungu la 4, panga kuwe na wonyesho mfupi kuonyesha jinsi ya kutoa kitabu hicho. Kazia umaana wa kufahamiana na kichapo hicho.
Dak. 15: Tumia Wakati Wako kwa Hekima Wakati wa Sikukuu. Watie moyo wahubiri wapange sasa kutumia wakati wa ziada wakati wa kipindi cha likizo ili kuendeleza masilahi ya kitheokrasi. Tia ndani madokezo ya kutoa ushahidi wa ki-vivi-hivi wakati wa kusafiri. Watie moyo wote kuweka miradi ya kibinafsi, kutia ndani kutokuachwa nyuma katika usomaji wa Biblia wa kila juma, kusoma vichapo vya Sosaiti, na kutumia kwa hekima wakati wa ziada katika kipindi cha likizo.
Wimbo 4 na sala ya kumalizia.