Uwezo wa Neno la Mungu
1 Neno la Mungu lina nguvu. (Ebr. 4:12) Leo, uthibitisho wa hilo waweza kuonwa katika maisha za mamilioni ya watu ambao wamebadilishwa na kuwa wema kwa kutumia binafsi mambo wanayojifunza kutoka kwa Biblia. Jambo hilo lilikuwa vivyo hivyo katika karne ya kwanza wakati wanafunzi wa Yesu waliposhiriki maarifa ya Neno la Mungu pamoja na wengine.—Rum. 12:2.
2 Ili watu wanufaike na mafundisho ya Biblia, wanahitaji kuiona Biblia kuwa Neno la Mungu. (1 The. 2:13) Katika Novemba tutakuwa tukiwatolea watu fursa ya kujifunza mengi kuhusu thamani ya Biblia tutakapokuwa tukiwatolea wale wanaopendezwa kikweli Biblia New World Translation of the Holy Scriptures na kitabu Biblia—Neno la Mungu au la Binadamu?
3 Kwa nini usipitie baadhi ya mambo ya kupendeza ya kitabu Neno la Mungu? Sehemu ya yaliyomo itakuongoza kwenye sura zinazozungumza juu ya miujiza, mambo yaonekanayo kuwa yapingana, upatano wa kisayansi, unabii mbalimbali, na habari nyinginezo. Kuna picha na vielezi vingi. Marejezo ya wasomi yameorodheshwa nyuma ya kitabu hicho. Mambo hayo yatatuwezesha kutoa kitabu hicho tukiwa na idili ya kweli, na usadikisho thabiti kwamba watu katika eneo letu wanahitaji kusikia habari njema zilizomo katika kitabu hicho.
4 Tunaweza kutumiaje kitabu hicho tunapokuta mwenye nyumba ambaye tayari anaamini kwamba Biblia ni Neno la Mungu? Kupendezwa kwaweza kusitawishwa kwa kukazia ama sura ya 2, inayosimulia juu ya historia ya vita vya Biblia ili kuishi, ama sura ya 14, inayotia moyo msomaji akubali msaada ili awe na ufahamu mzuri zaidi wa umuhimu wa Biblia kwetu leo. Kusoma maandiko yaliyo katika sura ya 14 kutamhakikishia mwenye nyumba kwamba mazungumzo yako yanategemea Biblia.
5 Wengi hukataa kukubali Biblia kuwa neno la Mungu kwa sababu ya mwenendo wa Jumuiya ya Wakristo. Sura ya 3, “Rafiki Bandia ya Biblia,” yaweza kutumiwa kwa matokeo katika hali hiyo.
6 Tunaposoma Biblia zetu, huenda mwenye nyumba akasema kwamba Biblia New World Translation inatumia maneno rahisi. Au huenda mwenye nyumba akapendezwa na ujumbe wetu lakini akose Biblia. Katika hali hizo, huenda tukaeleza juu ya mambo ya kipekee ya Biblia tunayotumia na sababu ya sisi kuipendelea. Miongoni mwa mambo mengine, tunaweza kumwonyesha orodha ya “Faharisi ya Maneno ya Biblia” inayosaidia kupata maandiko tunayojua. Pia, sehemu ya “Vichwa vya Mazungumzo ya Biblia” iliyo nyuma ya Biblia hiyo yaweza kusaidia wale wanaopendezwa kupata majibu kwa maswali mengi yanayoulizwa sanasana.
7 Kupitia Biblia, Yehova amejulisha shughuli zake na ainabinadamu na hivyo ametujulisha juu ya utu wake wa ajabu. Na tutumie Biblia New World Translation na kitabu Neno la Mungu kwa matokeo katika kusaidia wengine wajifunze kuhusu Yehova na uwezo wa Neno lake!—2 Kor. 10:4.