Rudi Usitawishe Kupendezwa Katika Ujumbe wa Ufalme
1 Wakati wa Agosti na Septemba tunapangia kufika maeneo ya mbali katika kampeni yetu ya Makedonia. Ijapokuwa tunapendezwa hasa na kupanda mbegu za Ufalme katika maeneo hayo yasiyofikiwa kwa ukawaida, tunapendezwa pia na kusitawisha kupendezwa kokote kunakoonyeshwa iwezekanapo.
2 Hapana shaka kwamba kutaniko limepanga kufanywa kwa eneo la Makedonia ili kuruhusu ziara za kurudia mahali ambapo kupendezwa kumeonyeshwa. Kwa hiyo, unapoenda mara ya kwanza hakikisha unaandika mambo vizuri kwenye rekodi yako ya nyumba kwa nyumba. Kisha unapojaza mfuko wako wa kutoa ushahidi, hakikisha kwamba umetia ndani nakala ya fasihi uliyoangusha ili uirejezee unapofanya ziara ya kurudia.
Ikiwa uliangusha broshua “Tazama!,” unaweza kusema:
◼ “Nina furaha kukuona tena. Tulipoongea wakati uliopita, nilikuonyesha jalada la broshua hii, na tulisoma andiko kwenye Biblia kuthibitisha hilo, kupitia Ufalme wake, Mungu ataandaa makao na kazi kwa kila mtu. Lakini pia Mungu ameahidi kukomesha ugonjwa, uzee, na hata kifo. Je! unaona hilo kuwa gumu kuamini? [Ruhusu itikio la mwenye nyumba.] Angalia jambo hili katika fungu la 4 la broshua niliyokuachia.” Soma fungu hilo, na mwangalie andiko moja au mawili yaliyoorodheshwa chini ya ukurasa huo. Funzo la Biblia linaanzishwa!
3 Ziara nzuri za kurudia zinazoongoza kwenye funzo la Biblia katika ile broshua Je! Kweli Mungu Anatujali? zaweza kutayarishwa kwa kuendelea na habari chini ya Sehemu ya 10 na kutumia vielelezo kwenye kurasa 25-27.
4 Kurudia Wale Tuliowaachia Trakti: Labda tulimwachia mwenye nyumba nakala ya trakti Ulimwengu Mpya Wenye Amani. Tunaporudi, tunaweza kuzungumzia mafungu ya kwanza ya trakti. Tunapofika mwisho wa fungu la kwanza kwenye ukurasa wa 3, ambapo Zaburi 37:29 imenukuliwa, tunaweza kusema:
◼ “Maneno hayo yanaonyeshwa katika kichapo hiki, Je! Kweli Mungu Anatujali? Angalia wazo hapa katika fungu la 22 kwenye ukurasa 27.” Kisha tunaweza kusoma fungu hilo na kuuliza swali lalo lililochapwa. Kisha tunaweza kusema: “Mungu atatimizaje ahadi hizi?” Mafungu yafuatayo yanaeleza hilo chini ya kichwa “Kubatilisha ya Wakati Uliopita.” Kisha soma fungu hilo na uangalie swali lililochapwa. Unaweza kukamilisha kichwa kidogo chote na kujaribu kupanga ziara ya wakati ujao au kufuatia katika namna inayofaa.
5 Kurudi ili kusitawisha kupendezwa katika ujumbe wa Ufalme ni kazi ya maana sana hata katika maeneo ya mbali. Yesu aliagiza wanafunzi wake wafundishe wengine yale waliyokuwa wamefundishwa. Tunamwomba Yehova apeleke wafanyakazi wengi. Hivyo basi, acheni tufanye sehemu yetu katika kutafuta wenye kupendezwa na kuwafundisha kuwa wafanyakazi wenzi katika mavuno.—Mt. 9:37; 28:19, 20.