Uwe Painia Msaidizi Katika Desemba
1 Sote tutafanya vizuri kujiuliza: ‘Ni kwa kadiri gani mimi nitakuwa mchukuaji nuru wakati wa Desemba? Je! ninaweza kuwa painia msaidizi?’—Mt. 5:14, 16.
2 Kwa ujumla, wachanga waliobatizwa watakuwa na msimu wa sikukuu baada ya kufunga shule. Huenda baadhi ya wazazi na wahubiri wengine wazima wakaweza kujiunga nao katika kupanua utumishi wa shambani katika mwezi huo. Vilevile wengi wanaofanya kazi wakati wote watakuwa na wakati wa ziada kutumika katika huduma hii ya kuokoa uhai.
3 Ili tuweze kutumika tukiwa mapainia wasaidizi, jambo kuu ni hiari yetu ya kutia jitihada ya ziada inayohitajika. (Lk. 13:24) Tukipanga utendaji wetu kwa uangalifu, kutia ndani mambo ya familia na kundi, wakati unaweza kupatikana ili tupate shangwe ya kutumika tukiwa mapainia wasaidizi.
4 Je! utaweza kupanua huduma yako wakati wa Desemba? Kufanya hivyo kwaweza kukusaidia uhisi ukiwa mwenye uhakika zaidi milangoni na kutokeze maono yenye kujenga. Hivyo, furaha nyingi zaidi yaweza kuwa yako.—Mdo. 20:35.