Sanduku la Swali
● Mashahidi wa Yehova wapaswa kuwa na maoni gani juu ya miredio ya tepe kutoka vyanzo vingine visivyo vya Sosaiti?
Sosaiti huandaa chakula tele cha kiroho kwa namna mbalimbali, kutia na mirekodio ya tepe za kaseti. Hiyo ni kutia ndani mirekodio ya kaseti za Biblia yenyewe na nyingine zinazotegemea vichapo vya Sosaiti, kama Mnara wa Mlinzi, na Amkeni! (Kiingereza) Kitabu Changu cha Hadithi za Biblia, na Kumsikiliza Mwalimu Mkuu (Kiingereza). Kingdom Melodies na drama kadhaa zimerekodiwa. Hata hivyo, twahitaji kutumia tahadhari kwa habari ya mirekodio ya tepe za faragha zinazoenezwa na ambazo huenda zikaonekana kuwa na chanzo kile kile. Kwa sababu ya kuwa udugu wenye kuaminiana sana huenda baadhi yetu wakapokea na kusikiliza nakala za tepe kutoka kwa wengine bila kuhakikisha chanzo chazo.
Nyakati nyingine hotuba zilizorekodiwa ambazo huenezwa hukaribia sana kuwa makisio-kisio au hutumia habari zenye kuchochea msisimuko. Kwa hiyo je! halingekuwa jambo la hekima kufuata ushauri wa Paulo kwenye 2 Timotheo 3:14? Humo, baada ya kuonya juu ya wasingiziaji, Paulo alikazia umaana wa kujua watu tunaowasikiliza. Tunahitaji kuhakikisha kwamba sisi hatusikilizi jambo lolote linalopita “yale yaliyoandikwa” katika Maandiko Matakatifu na katika chakula cha kiroho kinachoandaliwa na “mtumwa mwaminifu mwenye akili.”—1 Kor. 4:6; Mt. 24:45-47.
Katika maeneo fulani tepe za kufundisha watoto Biblia zinatangazwa na kuuzwa. Yaonekana kwamba tepe hizo asili yazo ni akina ndugu na zimeenezwa miongoni mwa baadhi ya makundi. Ingawa huenda kusudio likaonekana kuwa jema, je! hilo halingekuwa sawa na kutumia mahusiano ya kitheokrasi kwa faida za kibinafsi? (Ona Utumishi Wetu wa Ufalme, Julai 1977, ukurasa 4, na Huduma ya Ufalme Yetu, Septemba 1987 ukurasa 3.) Tengenezo la Yehova linaandaa mafunzo ya kutosha na hata zaidi yanayotegemea Biblia ili kuzoeza watoto wetu. Kwa hiyo, sisi tunavunja moyo uenezaji wa tepe hizo.
Baadhi ya watu mmoja mmoja huenda wakafanya mirekodio ya tepe ya mikutano ya kundi au programu za kusanyiko au mikusanyiko kwa ajili ya matumizi ya kibinafsi. Mirekodio kama hiyo huenda yakathaminiwa pia na wengine ambao kwa sababu nzuri hawawezi kuwapo mikutanoni. Hata hivyo, hiyo haipasi kufanywa kwa ajili ya kugawanywa miongoni mwa akina ndugu kwa ujumla au kuuziwa wengine. Sisi na tutumie kikamili yote ambayo Yehova ameandaa kupitia tengenezo lake kwa ajili ya kitia-moyo na kujengwa kiroho kwetu.