Macho kwa Vipofu
MIAKA fulani iliyopita mtu mmoja katika Indiana alipata pigo lililoharibu usemi wake. Kama matokeo, ilimpasa aanze upya kujifunza kuzungumza sawasawa. Kusudi ajisaidie kufanya hivyo, alijiunga na chama cha utepe, akitumaini kufanya maendeleo katika usemi wake alipokuwa akisoma habari za vipofu kuelekea tepu rekoda. Kwa kweli yeye alitaka awasaidie vipofu waone.
Mgawo wa kwanza alioupata ulikuwa kusoma nakala za The Watchtower na Awake! kwa mwanamke mmoja katika Canada, mmoja wa mashahidi wa Yehova kipofu aliyekuwa anasumbuliwa na moyo. Ijapokuwa tamaa yake kubwa ilikuwa kufanya maendeleo katika usemi wake, alipoanza kusoma The Watchtower na Awake! kwa Shahidi alifahamu kwamba aliyokuwa anayasoma yalitofautiana na aliyokuwa amefundishwa kanisani. Makala zenye Maandiko pamoja na mitajo yake ya Biblia ziliamsha kupendezwa ajue mengi zaidi ndani yake.
Kwa sababu ya kupendezwa kwake Shahidi katika Canada akamtumia nakala ya Kweli Iongozayo kwenye Uzima wa Milele na kushauri kwamba wote wawili wawe na funzo la Biblia la kawaida wakitumia kitabu hiki kidogo. Alikubali lakini akashangaa ni kwa njia gani Shahidi angeweza kufanya hivyo, kwa maana alikuwa kipofu. Ilitukia kwamba, Shahidi alikuwa na nakala ya kitabu hiki katika lugha ya Braille na kwa hiyo kwa zaidi ya miezi kumi na mmoja iliyofuata funzo la Biblia lilifanyika kwa kutumia utepe, likicheleweshwa kidogo na migomo ya posta.
Shahidi katika Canada alimtia mtu huyo moyo akawaone mashahidi wa Yehova katika eneo lake. Lakini ilikuwa vigumu, kwa maana hakuweza kama alivyopenda. Mwishowe, mhudumu wa mashahidi wa Yehova katika huduma ya kawaida ya nyumba kwa nyumba alibisha hodi mlangoni pake. Salamu ya mtu huyu iliyomshangaza Shahidi ilikuwa: “Ingia. Nimekuwa nikiwangoja ninyi kwa mwaka mzima sasa. . . . Najua imenipasa nifike kwenye mikutano yenu ya Kikristo. Nimekuwa nikiwangoja ninyi mje kunichukua.”
Sasa anafurahia kwa kawaida funzo la Biblia pamoja na mmoja wa wahudumu wa mahali pake na anasaidiwa kufika kwenye mikutano ya Kikristo katika Jumba la Ufalme. Hata hivyo, yeye hajasahau njia aliyoitumia kujifunza kweli ya Biblia. Ijapokuwa hayumo katika hali ya kimwili inayoweza kumruhusu ashiriki katika huduma ya nyumba kwa nyumba pamoja na mashahidi wa Yehova, yeye anaendesha kazi ya kuhubiri kwa kutumia tepu zinazotumwa kwa vipofu na waliolemaa walio washiriki wa chama cha utepe. Anatumaini kwamba, kama vile upofu wake wa kiroho ulivyoponywa kupitia kwa tepu, ataweza kuyafumbua macho ya wengine kwa kutumia kweli zenye kuelimisha za Biblia.