MAISHA YA MKRISTO
Kuboresha Ustadi Wetu Katika Huduma—Kuwahubiria Vipofu
KWA NINI NI MUHIMU: Vipofu wengi hawajihisi huru kuzungumza na mtu mgeni. Kwa hiyo, unahitaji kuwa na ustadi ili kuwatolea ushahidi. Yehova anawapenda na kuwajali vipofu. (Law 19:14) Tunaweza kuiga mfano wake kwa kuchukua hatua ya kwanza kuwasaidia vipofu kiroho.
JINSI YA KUFANYA HIVYO:
“Watafute” vipofu. (Mt 10:11) Je, unamfahamu mtu aliye na mtu wa ukoo ambaye ni kipofu? Je, eneo lenu lina shule au mashirika mengine ambayo yangependa machapisho yaliyotayarishwa kwa ajili ya vipofu?
Onyesha upendezi wa kibinafsi. Kuonyesha urafiki na upendezi wa kweli kutamfanya mtu ambaye ni kipofu ajihisi huru. Jaribu kuanzisha mazungumzo yanayotegemea habari inayofaa eneo lenu
Andaa msaada wa kiroho. Ili kuwasaidia vipofu na wale wenye uwezo mdogo wa kuona, tengenezo letu limetokeza machapisho ya aina mbalimbali. Muulize mwenye-nyumba angependa kutumia njia gani kujifunza. Mwangalizi wa utumishi anapaswa kuhakikisha kwamba mtumishi wa machapisho anatoa ombi la aina ya chapisho ambalo kipofu angependa zaidi