Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 11/90 uku. 7
  • Saidia Wengine Wawe Stadi Katika Kutumia Neno la Mungu

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Saidia Wengine Wawe Stadi Katika Kutumia Neno la Mungu
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1990
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • SAIDIA VIJANA NA WANAFUNZI WA BIBLIA
  • Mapainia Wasaidia Wengine
    Huduma Yetu ya Ufalme—1998
  • Msaada Wakati Unaofaa
    Huduma Yetu ya Ufalme—1990
  • Je, Unatimiza Huduma Yako Kikamili?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2019
  • Fanya Maendeleo Katika Kazi ya Kuhubiri
    Huduma Yetu ya Ufalme—2008
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—1990
km 11/90 uku. 7

Saidia Wengine Wawe Stadi Katika Kutumia Neno la Mungu

1 Yehova amefanya maandalizi mengi ili kutuzoeza tuwe wenye mafanikio katika kufanya huduma yetu binafsi. Kwa kutumia yale ambayo ameandaa, ‘hatua zetu wenyewe zimefanywa kuwa tayari.’ (Zab. 37:23) Kwa kielelezo, kwa karibu miaka 50 Shule ya Huduma ya Kitheokrasi imekuwa ikitoa mazoezi hatua kwa hatua katika ustadi wa kunena na kufundisha. Mazoezi hayo yameongezewa na ule Mkutano wa Utumishi wa kila juma, wenye hotuba, maonyesho, na vipindi vya mazungumzo vyenye kutumika.

2 Sisi tunanufaishwa na ziara za ukawaida za waangalizi wa mzunguko. Mwangalizi wa utumishi huzuru kila kikundi cha funzo la kitabu na kuandaa kitia-moyo chenye upendo ili kusaidia kufanyia maendeleo uwezo wetu mbalimbali katika huduma ya peupe. Pamoja na hayo yote, kila wakati tukutanapo kwa ajili ya utumishi wa shambani, dakika kumi zenye maagizo yenye kutumika hutupatia kitia-moyo na madokezo yenye mafaa kwa siku hiyo. (Ebr. 10:23-25) Mipango hiyo kupitia tengenezo lake huonyesha hangaikio la Yehova lenye upendo kwa wale ambao amewapa utume wa kuhubiri habari njema.

SAIDIA VIJANA NA WANAFUNZI WA BIBLIA

3 Wahubiri wachanga na wahubiri wapya zaidi huhitaji usaidizi wa kibinafsi katika huduma ya umma. Ingawa sisi sote twaweza kutoa msaada wakati kwa wakati, daraka kuu ni la wazazi na wale wanaoongoza mafunzo ya Biblia pamoja na watu hao. (Gal. 6:6; Efe. 6:4) Mafanikio katika kutumia Biblia hayajileti yenyewe tu kwa kupita kwa wakati na kuwa na kadiri fulani ya ujuzi. Badala ya hivyo, kuna uhitaji wa usaidizi na mazoezi ya kibinafsi yenye upendo.

4 Usaidizi wa kibinafsi wapasa kuanza kabla mtu huyo hajaanza kushiriki huduma kihalisi. Pitia Kichwa cha Mazungumzo. Saidia wale waliohitimu kushiriki huduma wastawishe utoaji sahili. Labda wanaweza kutumia andiko moja ya yale yaliyodokezwa mpaka wapate ujuzi zaidi na uhakika. Mfanyapo kazi pamoja katika utumishi, chukua wakati katikati ya milango kuwapongeza na kuwaandalia madokezo yenye fadhili juu ya jinsi ya kufanya maendeleo. Kazia uhitaji wa kudumisha mwelekeo wa sala nyakati zote.—Efe. 6:18, 19.

5 Ingawa mapainia wa kawaida na wahubiri wengine wenye ujuzi hushiriki huduma sana-sana katika siku za katikati ya juma, ni jambo zuri kama nini wakati wahubiri hawa wenye mafanikio wanapoweza kupanga ratiba yao ili waunge mkono utumishi wa shambani wa mwisho wa juma wakati kwa wakati. Dhabihu hizo za kibinafsi kwa upande wao zitathaminiwa sana na wengine ambao wangetaka kufanya maendeleo kwa kufanya kazi pamoja nao katika huduma. —Muh. 4:9, 10.

6 Wakati mmoja sisi sote tulikuwa wapya na wasio na ujuzi katika huduma ya shambani. Wengi wetu tulipokea kitia-moyo na mazoezi kutoka wahubiri na mapainia wenye ujuzi zaidi. Ustadi wetu wa sasa na shangwe iliyoongezeka katika huduma ni matokeo ya moja kwa moja kutoka kwa usaidizi huo. (Mit. 27:17; Mdo. 20:35) Uthamini wetu kwa yale ambayo Yehova ametufanyia kupitia mazoezi yenye bidii katika huduma na yatusukume tujifanye tupatikane ili kusaidia wengine wawe wenye ustadi zaidi katika kutumia Neno la Yehova.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki