Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 4/08 uku. 1
  • Fanya Maendeleo Katika Kazi ya Kuhubiri

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Fanya Maendeleo Katika Kazi ya Kuhubiri
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2008
  • Habari Zinazolingana
  • Saidia Wengine Wawe Stadi Katika Kutumia Neno la Mungu
    Huduma Yetu ya Ufalme—1990
  • Jinsi ya Kuwazoeza Wahubiri Wapya Katika Utumishi
    Huduma Yetu ya Ufalme—2010
  • Je, Unatimiza Huduma Yako Kikamili?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2019
  • Uwe Stadi Katika Huduma Yako
    Huduma Yetu ya Ufalme—1990
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—2008
km 4/08 uku. 1

Fanya Maendeleo Katika Kazi ya Kuhubiri

1 Baba yetu wa mbinguni anapendezwa watumishi wake wanapofanya maendeleo ya kiroho. Hilo linatia ndani kufanya maendeleo ili kuwa wahubiri wakomavu na wenye matokeo wa habari njema. Paulo alimtia moyo mwangalizi Timotheo aendelee kufanya bidii ili maendeleo yake yawe wazi. (1 Tim. 4:13-15) Sote tunapaswa kujitahidi kuboresha huduma yetu, hata sisi ambao ni wahubiri wenye uzoefu.

2 Jiwekee Miradi: Ili ufanye maendeleo, unahitaji kujiwekea miradi. Tunaweza kujiwekea miradi gani? Tunaweza kujitahidi kuwa stadi katika kutumia upanga wetu wa kiroho, Biblia. (Efe. 6:17) Labda kuna sehemu fulani ya huduma yetu ambayo tunahitaji kufanyia maendeleo, kama vile kuhubiri barabarani, kuhubiri kwa simu, au kwenye maeneo ya biashara. Labda tunaweza kujitahidi kufanya ziara za kurudia zenye matokeo zaidi. Mradi mwingine mzuri ni kuboresha uwezo wetu wa kuanzisha na kuongoza mafunzo ya Biblia.

3 Maandalizi: Mikutano ya kutaniko, hasa Shule ya Huduma ya Kitheokrasi na Mkutano wa Utumishi imekusudiwa kutusaidia kufanya maendeleo tukiwa wahudumu. Kadiri tunavyojitahidi kutayarisha na kuhudhuria mikutano hiyo na kutumia mapendekezo tunayopata, ndivyo tutakavyofaidika zaidi.—2 Kor. 9:6.

4 Pia, tunahitaji kusaidiana kufanya maendeleo. (Met. 27:17) Kuwasikiliza kwa makini wale tunaohubiri nao kutatusaidia kufanya maendeleo. Isitoshe, mwangalizi wetu wa funzo la kitabu anaweza kupanga tupate msaada wa kibinafsi. Ni baraka kama nini tunaposaidiwa na painia au mhubiri mwenye uzoefu kuwa wenye matokeo zaidi na kupata shangwe zaidi katika huduma! Je, kuna mhubiri mpya katika funzo letu la kitabu? Labda tunaweza kuchukua hatua ya kwanza ya kumwalika ahubiri pamoja nasi.

5 Huduma ya Kikristo ndiyo kazi muhimu zaidi leo. Tunapoendelea kumtolea Yehova ‘dhabihu yetu ya sifa,’ tunataka kumpa kilicho bora. (Ebr. 13:15) Tukijitahidi kufanya maendeleo katika kazi ya kuhubiri, tutakuwa wafanyakazi ‘wasio na lolote la kuonea aibu, tukilitumia sawasawa neno la kweli.’—2 Tim. 2:15.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki