Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 6/90 kur. 1-3
  • Uwe Stadi Katika Huduma Yako

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Uwe Stadi Katika Huduma Yako
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1990
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • JIFUNZE KUTOKA NENO LA MUNGU
  • TUMIA MADOKEZO
  • Saidia Wengine Wawe Stadi Katika Kutumia Neno la Mungu
    Huduma Yetu ya Ufalme—1990
  • Fanya Maendeleo Katika Kazi ya Kuhubiri
    Huduma Yetu ya Ufalme—2008
  • Fundisha kwa Ustadi na Bidii
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1985
  • Je, Unalitumia Neno la Mungu Sawasawa?
    Huduma Yetu ya Ufalme—1996
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—1990
km 6/90 kur. 1-3

Uwe Stadi Katika Huduma Yako

1 Mtume Paulo anatia moyo usitawishaji wa ustadi katika huduma. Yeye aliandika hivi: “Fanya yote yote uwezayo kujiweka mwenyewe mbele za Mungu katika hali ya kukubaliwa, mfanyi kazi asiye na lolote la kuaibikia, ukitumia lile neno la ule ukweli sawasawa.”—2 Tim. 2:15, NW.

2 Ustadi katika huduma ni wa kufanyiwa kazi. Kwa hiyo, ni lazima sisi ‘tufanye yote yote tuwezayo’—kujitahidi kwa bidii—ikiwa tutakuwa wahudumu wenye ustadi. Lakini ni nini kitakachotusaidia?

JIFUNZE KUTOKA NENO LA MUNGU

3 Maarifa yetu ya kibinafsi ya Maandiko yanahusiana moja kwa moja na kuwa kwetu wahudumu wenye matokeo. Jinsi tunavyofahamiana vizuri zaidi na yale ambayo Biblia hufundisha, ndivyo tutakavyokuwa wenye matokeo zaidi katika ‘kutumia neno la ule ukweli sawasawa.’ Kwa hiyo ni jambo la muhimu kuweka kando wakati kwa ajili ya funzo la kibinafsi.—1 Tim. 4:15, 16.

4 Njia nyingine ya kupata kufahamiana na Neno la Mungu ni ‘kuangalia zaidi kuliko kawaida’ maagizo yenye msingi wa Biblia yanayopokewa kwenye mikutano ya kundi. (Ebr. 2:1, NW) Mambo murua kwa ajili ya huduma yanazungumzwa katika hotuba za watu wote au yaweza kukumbizwa kwa Funzo la Kitabu la Kundi. Shule ya Huduma ya Kitheokrasi hutupa mazoezi yenye thamani tuwe walimu wenye ustadi, na Mkutano wa Utumishi huandaa madokezo yenye kusaidia na maonyesho yenye kutumika ili kutusaidia kuwa wahudumu wenye matokeo zaidi. Hata hivyo, ili kupata manufaa kubwa zaidi, tunahitaji kujitayarisha vizuri na kushiriki kihalisi katika mikutano yote.

TUMIA MADOKEZO

5 Paulo aliambia kundi katika Filipi lijizoeze mambo waliyojifunza kwa kukamatana na yeye. (Flp. 4:9) Sisi pia twahitaji kujizoeza mambo tunayojifunza kupitia tengenezo la Yehova. Kwa kielelezo, katika toleo la Julai 15, 1988 la Mnara wa Mlinzi, kurasa 15-20, tulijifunza njia ambazo kwazo twaweza kusitawisha eneo “jipya” katika sehemu ambazo zinafanyiwa kazi mara nyingi. Kuongezea kukazia uhitaji wa mfikio mpya, wenye kuvutia, na ulio chanya, makala hiyo ilitutia moyo tumzoeze mwenye nyumba atutazamie tuzuru kwa ukawaida. Ushauri ulitolewa tuwe wenye kutafuta wanaostahili kikamili, tukitafuta watu mmoja mmoja tofauti wanaoishi chini ya dari lile lile.

6 Hali moja na hiyo, toleo la Januari 15, 1985 la Mnara wa Mlinzi, kurasa 12-22, lilitoa madokezi fulani mazuri juu ya jinsi ya kuchunguza ishara za kukueleza mtazamo wa kidini ili kuongoza kwenye utangulizi wa kirafiki, wenye kuamsha kupendezwa. Kitia-moyo kilitolewa ili kutumia njia za kuhubiri za Yesu na Paulo, na kuwa wenye nadhari, kutafuta msingi fulani unaokubaliana na mwenye nyumba, na kunena kwa usadikisho na kwa usahili. Kwa kutumia madokezo hayo, tunajizoeza mambo tunayojifunza na kufanya stadi zetu katika huduma kuwa bora zaidi.

7 Je! sisi hutumia kwa ukawaida kitabu Kutoa Sababu katika huduma ya shambani? Tangulizi zinazodokezwa na pia kile kisehemu juu ya jinsi ya kujibu vizuia maongezi vinavyoweza kutokea chaweza kunoa stadi zetu za kutoa ushahidi. Kuongezea hayo, kutayarisha na kufanya mazoezi ya Kichwa cha Mazungumzo na njia ambayo tutatoa toleo la mwezi kutachangia fanaka yetu katika huduma.

8 Kama ungependa madokezo ya ziada juu ya jinsi ya kufanya huduma yako iwe bora zaidi, mfikie mwangalizi wa utumishi au kiongozi wa funzo la kitabu wako na kuomba msaada. Sisi sote twaweza kufanya stadi zetu tukiwa wahudumu ziwe bora zaidi, ‘tukitumia lile neno la ule ukweli sawasawa.’ Baada ya muda mfupi Yehova Mungu atakomesha mfumo mbovu huu. Hadi wakati huo, tamanio letu la moyoni ni kusaidia watu wengi tuwezavyo ili wapate wokovu na hivyo kuletea heshima Mungu wetu Yehova.—Yn. 15:8.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki