Kufanya Kazi kwa Njia Yenye Matokeo Nyumba kwa Nyumba
1 Leo “habari njema” zinahubiriwa kotekote duniani. (Mt. 24:14) Kimsingi, hilo linatimizwa kupitia huduma ya nyumba kwa nyumba.—Mdo. 20:20, 21.
2 Ni lazima utoaji wetu mbalimbali uwe na maana halisi kwa watu tunaokutana nao. Wanaume, wanawake, na vijana wanatofautiana katika mambo yanayowapendeza. Kwa hiyo ingefaa kuwa tayari na unamna-namna wa habari za Kimaandiko ambazo zinaelekea kuwavutia watu katika eneo letu.
3 Tumia Vichapo Ifaavyo: Kitabu Kuishi Milele huzungumzia habari nyingi mbalimbali ambazo zapaswa kuwavutia watu wengi kila mahali. Vielezi, vya picha na vya maneno pia, ni misaada yenye matokeo. Kitabu hicho huvutia moyo, na husaidia watu waone uhitaji wa kufanya maamuzi, naam, kubadilisha itikadi, mwenendo, mtazamo, na njia yao ya maisha. Kwa kufahamu kikamili yaliyomo katika kitabu Kuishi Milele, tutaweza kuzungumza na watu kwa matokeo juu ya vichwa mbalimbali. Hilo litatusaidia tujue kadiri ya kupendezwa kwa mwenye nyumba.
4 Ili kuwa wenye matokeo hudumani, tunahitaji kuonyesha kupendezwa kibinafsi kwa moyo mnyoofu. (Flp. 2:4) Jitahidi kuelekeza mazungumzo kwenye kichwa fulani cha Ufalme kinachohusisha mtu huyo na mahitaji yake. Jaribu kuelewa fikira za mtu huyo kwa kumwuliza maswali yanayomhusu. Sikiliza majibu yake kwa uangalifu. Huenda maelezo yake yakakusaidia ujue ni habari ipi itakayompendeza. Tunataka kuwasaidia watu waone thamani ya ujumbe wa Ufalme na kuwaonyesha jinsi ya kujifunza zaidi kuuhusu. Wenzi wawili waliooana walieleza kwamba walikubali funzo la Biblia kwa sababu ndugu aliyewahubiri alionyesha kupendezwa kibinafsi nao kwa moyo mnyoofu.
5 Katika Eneo Linalohubiriwa Mara Nyingi: Kusitawisha hali ya kuwa wenye matokeo ni kwa maana hasa katika eneo linalohubiriwa mara nyingi. Huduma yenye matokeo zaidi hutusaidia kupanua eneo letu. (w88-SW 7/15 kur. 15-20) Badala ya kutenda kana kwamba hatujapata kuhubiri nyumba hiyo kamwe, tunaweza kukumbuka mtazamo wa mwenye nyumba wa wakati uliopita na kuutumia kwa faida yetu. Tunaweza kutaja juu ya ziara yetu iliyopita halafu tujenge juu ya yale yaliyosemwa wakati huo. Utoaji mbalimbali uliodokezwa katika matoleo yaliyopita ya Huduma ya Ufalme Yetu na katika kitabu Kutoa Sababu yaweza kufanywa yafae eneo.
6 Kwa subira, Yehova anaendelea kuuweka mlango ukiwa wazi ili watu wengi zaidi wanufaike kutokana na baraka za Ufalme. Huduma ya Yesu ilikuwa yenye matokeo kwa sababu ya upendo wake kwa watu. (Mk. 6:34) Je! tunafanya yote tuwezayo kufuata mfano wake? (1 Pet. 2:21) Acheni tusijizuie kushiriki kikamili na kwa matokeo katika huduma ya nyumba kwa nyumba.—2 Tim. 4:5.