Tumia Magazeti Vizuri
1 Unapozuru mahali panapouzwa magazeti, unaona magazeti mengi ajabu yenye kuvutia yaliyo na habari nyingi kuanzia vichekesho hadi tekinolojia ya kisayansi. Wewe hungeweza kuyasoma yote. Ingawa magazeti fulani yana habari yenye mafaa, mengi yayo yana thamani yenye kutilika shaka. Mengi hayana staha na lazima yaepukwe.
2 Ni tofauti kama nini yanapolinganishwa na Mnara wa Mlinzi na Amkeni! Kusudi la magazeti hayo ni kutafuta na kupiga mbiu ya ile kweli inayoweza kutumiwa kwa ajili ya wokovu wa wote wanaoitikia upendo wa Mungu.
3 Amkeni! laweza kuwafikia watu wa aina zote kwa njia yenye matokeo kwa sababu ya habari zalo zenye mweneo mkubwa na makala zalo mbalimbali. Kama inavyoelezwa katika ukurasa 4 wa kila toleo, “ni gazeti la kupatia familia nzima nuru.” Linatokeza makala nyingi kuhusu habari mbalimbali, zinazotia ndani watu, dini, na sayansi. Huchunguza sana matukio ya sasa na hutoa maana ya kweli ya matukio ya sasa. La maana kuliko yote, hilo “hujenga uhakika katika ahadi ya Muumba ya kuleta ulimwengu mpya wenye amani na usalama.”
4 Toleo la Amkeni! la Oktoba 8 lina kichwa “Wewe Unaweza Kushinda Hisiamoyo Zisizofaa.” Maisha ya watu wengi yameharibiwa na hisiamoyo kama hizo. Kutoa gazeti hilo kwa kukazia juu ya shauri layo la Biblia lenye kutuliza kwaweza kutokeza itikio. Kwa habari ya toleo la Desemba 8 (Oktoba 22, Kiingereza), tutaweza kupata wenye kusikiliza kwa kuelekeza fikira kwenye mambo yenye kufariji katika mfululizo “Ulimwengu Mpya Unaoridhisha Wote.”
5 Mnara wa Mlinzi limejithibitisha kuwa mtetezi mashuhuri ulimwenguni wa habari njema kuhusu Ufalme wa Mungu na baraka za Paradiso utakazoleta. Toleo la Oktoba 1 litajibu swali lenye kuchungua “Je! Kweli Ainabinadamu Inahitaji Mesiya?” Hilo litatupa fursa nzuri ya kuzungumza kuhusu tumaini letu la Ufalme. Habari kuhusu “Maisha ya Familia Leo—Kukabiliana na Matatizo Yayo,” inayozungumzwa katika toleo la Oktoba 15, itatusaidia tuanzishe mazungumzo na washiriki wa familia wanaotamani kupata kitulizo kutoka kwa mikazo mingi ya maisha. Wengi wataona utangulizi wa mfululizo wa makala katika toleo la Septemba 15 “Kwa Nini Watu Wema Huteseka?” kuwa wa wakati barabara na wenye msaada katika siku hizi zenye ukame, njaa, na msukosuko wa jeuri unaoenea pote ambao huua watu wengi wasio na hatia.
6 Rekodi katika ofisi zinaonyesha kwamba wengi wanaandikisha wapate magazeti yetu, kwa hiyo dumisha mtazamo unaofaa unapotoa toleo hilo. Ikiwa toleo la uandikisho halikubaliwi basi hakikisha kutoa magazeti ya karibuni zaidi. Labda unaweza kusitawisha ziara hiyo kuwa sehemu yako ya njia ya kupelekea watu magazeti kwa ukawaida.
7 Tunaweza kupendekeza majarida yetu kwa watu wote, kwa kuwa tunasadikishwa juu ya thamani yayo. Tuna jambo zuri, na ni kufuata mfano wa Kristo kulishiriki na wengine.—Mit. 3:27; Ebr. 13:16.