Mnara wa Mlinzi—Chakula cha Kiroho kwa Wakati Unaofaa
1 Mnara wa Mlinzi limekuwa likiwahimiza wasomaji walo waendelee kuwa macho kiroho, kwa yapata miaka 114. Gazeti jenzilo Amkeni! hutia nguvu uhakika katika ahadi ya Muumba juu ya dunia mpya yenye amani na usalama katika kizazi chetu. Vikiwa pamoja, vichapo hivi viwili vimekuwa vyombo vyaminifu vikiangazia njia yetu kupitia ulimwengu uliotiwa giza. (Isa. 60:2) Kweli ya Neno la Mungu haibadiliki kamwe, lakini kulielewa kwetu huwa wazi zaidi Yehova atumiapo vifaa hivi na vinginevyo kutupa sisi ‘chakula cha kiroho kwa wakati unaofaa.’—Mt. 24:45, NW; Mit. 4:18.
2 Tumia Magazeti Vizuri Iwezekanavyo: Tunaweza kuonyesha shukrani zetu kwa mnurisho wa kiroho ambao tumepokea kwa kuwatia moyo watu kwa idili wasome Mnara wa Mlinzi na Amkeni! pia. Wakati wa mwezi huu tutatoa uandikisho tufanyapo ziara za kwanza katika kazi ya nyumba kwa nyumba au tutoapo ushahidi wa vivi hivi. Tolea uandikisho watu unaopelekea magazeti kwa ukawaida au wale wanaojulikana hufurahia kuyasoma magazeti yetu. Je! wale tunaojifunza nao Biblia wana maandikisho yao binafsi? Hii ni fursa nzuri kabisa ya kuwasaidia waone thamani ya kuwa mwandikishaji wa kawaida wa magazeti hayo. Mahali ambapo toleo la uandikisho halikubaliwi hakikisha umetoa matoleo ya karibuni pamoja na broshua.
3 Ufikirio wa hali ya watu ya milele hutusukuma sisi tuwe chonjo kutambua kupendezwa kwao na ujumbe wa Biblia wa tumaini na faraja. Waweza kutambuaje kama kuna kupendezwa halisi? Uonyeshapo jambo moja au mawili katika gazeti, trakti, au broshua, angalia jinsi mwenye nyumba anavyoitikia. Je! anasikiliza kwa makini? Je! anaiheshimu Biblia na kufuata maandiko ya Biblia yasomwapo? Je! anaitikia maswali ya maoni? Ikiwa ndivyo, hakikisha umepanga ziara ya kurudia katika juma moja au hata upesi zaidi na ufurahie mazungumzo zaidi wakati huo.
4 Matoleo moja moja ya magazeti hayo yaweza kutolewa kwa wafanyakazi wenzi, wanashule wenzi na watu wa ukoo. Magazeti hayo pia yaweza kutolewa kwa watu mnaofahamiana kibiashara na katika ushahidi wa barabarani.
5 Magazeti mapya yapasa kutolewa kwa wahubiri mara yapelekwapo kundini. Unapopokea toleo jipya, pata kulifahamu kikamili. Ni mambo gani yanayohusu watu sana katika eneo lenu? Amani na usalama wa ulimwengu? Uchumi? Je! ni mazingira? Jambo lenye kutokeza ni kwamba, Mnara wa Mlinzi huelekeza watu kwenye suluhisho pekee la kudumu, Ufalme wa Mungu. (Dan. 2:44; Mt. 6:9, 10) Kwa kweli hiyo ni zawadi isiyohesabika bei kutoka kwa ‘Mfunzi wetu Mtukufu.’—Isa. 30:20, NW.
6 Aprili na Mei yatoa fursa bora kabisa za kutumia wakati mwingi zaidi kwa ajili ya utumishi wa shambani. Kwa kuwa Mei una miisho-juma kamili mitano, wengi watajiandikisha kuwa mapainia wasaidizi. Sisi sote twaweza kuweka miradi ya kibinafsi sasa ili kuongeza utumishi wetu wa shambani wakati wa miezi hii miwili na kutia moyo kwa idili kila mtu tunayekutana naye asome Mnara wa Mlinzi na Amkeni!