Wasaidie Wapya Wafanye Maendeleo
1 Katika Aprili 17, 1992, karibu watu milioni 11.5 ulimwenguni pote walikutana ili kuadhimisha Ukumbusho wa kifo cha Kristo. Hii ilikuwa zaidi ya mara mbili unusu ya jumla ya idadi ya wahubiri wanaoshirikiana na makundi ya Mashahidi wa Yehova. Jinsi inavyofurahisha kuona umati huo ukimiminika “mlimani kwa BWANA [Yehova, NW]”! (Mik. 4:2) Kwa sasa kuna watu milioni saba hivi wanaoonyesha kupendezwa kwa kadiri fulani na ibada ya kweli na ambao bado si wasifaji hadharani wa Yehova. Kwa hakika maneno ya Yesu “mavuno ni mengi” hayajapata kamwe kuwa na umaana mwingi hivi!—Mt. 9:37, 38.
2 Katika mwezi wa Aprili, tutafanya jitihada ya pekee kuwasaidia wale wote wanaostahili kushiriki katika huduma ya shambani. Kiongozi wa funzo la Kitabu la Kundi, akisaidiwa na wahubiri na mapainia wengine wenye ujuzi katika kikundi chake, atakuwa na daraka kuu katika hilo. Miradi yetu mitatu ni (1) kupangia funzo la Biblia nyumbani na wapya wanaohudhuria hotuba ya watu wote ya pekee na Ukumbusho mwaka huu; (2) kuwatia moyo wale wanaojifunza wastahili kuwa wahubiri wasiobatizwa; na (3) kuongeza kushiriki kwetu binafsi katika huduma ya shambani.
3 Jitihada ya pekee yapasa kufanywa na wote ya kukaribisha na kufahamiana na wapya wanaohudhuria mikutano yetu yoyote. Je! twaweza kufanya nini ili kuwatia moyo watu wengine zaidi wanaopendezwa wawe na funzo la Biblia nyumbani la kawaida?
4 Kwa wastani, mafunzo ya Biblia 29,750 yaliongozwa katika Afrika Mashariki kila mwezi wa mwaka wa utumishi wa 1992. Wahubiri waweza kualika kiongozi wao wa funzo la kitabu aandamane nao kwenye mafunzo ya Biblia ili afahamiane na wanafunzi. Huenda ikawa baadhi ya wanafunzi hao wa Biblia wanahudhuria mikutano na wanastahili kushiriki katika kazi ya nyumba kwa nyumba. Je! wapya wanatoa ushahidi kivivi-hivi kwa ukawaida wa kadiri fulani? Je! wanatimiza sifa za kuwa wahubiri wasiobatizwa kama ionyeshwavyo katika Huduma Yetu, kurasa 97-9? Ikiwa ndivyo, waeleze jinsi wanavyoweza kuanza kazi ya nyumba kwa nyumba baada ya kukubaliwa kuwa wahubiri wasiobatizwa.
5 Tusipuuze kamwe kutiana moyo katika ushirika wetu wa Kikristo. (Ebr. 10:24, 25) Ikiwa kuna wowote ambao wamepunguza huduma yao, viongozi wa mafunzo ya vitabu wanapaswa kufanya mipango hususa ya kutoa msaada na kitia-moyo. Wakati mwingine mwaliko wa uchangamfu wa kuandamana nasi katika huduma ya shambani ndio unaohitajiwa.
6 Ushirikiano wa wote unahitajiwa ili kufanya Aprili uwe mwezi wenye kutokeza wa utendaji wa utumishi wa shambani. Mwongozo wenye idili wa kiongozi wa funzo la kitabu waweza kutokeza tofauti asaidiapo kila mshiriki wa kikundi chake awe na ushiriki kamili katika huduma. Mikutano ya utumishi ya ziada yaweza kupangwa. Wazee-wazee wanaweza kupewa uangalifu wa pekee, na vijana wanaweza kusaidiwa kwa njia zenye mafaa. Wazazi wanapaswa kuhakikisha kwamba familia nzima inashiriki katika huduma wakati wa Aprili. Ikiwa sote twampa Yehova yaliyo bora zaidi wakati huu wa mavuno, baraka zake nyingi zitakuwa zetu.