Mikutano Ya Utumishi Kwa Aprili
Juma Linaloanza Aprili 5
Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Pitia matoleo ya karibuni ya magazeti, ukikazia makala ambazo huenda zikawa na jambo la kupendeza hasa katika eneo lenu. Panga wahubiri wawili, mmoja mwenye umri mkubwa na mwingine mchanga wafanye maonyesho mafupi ya Kimaandiko.
Dak. 15: “Mnara wa Mlinzi—Chakula cha Kiroho kwa Wakati Unaofaa.” Mazungumzo ya maswali na majibu. Tia ndani maelezo ya jinsi ya kutambua kupendezwa halisi. Uthibitisho wa kupendezwa kwa moyo mweupe hutia ndani utayari wa kuzungumza na kueleza maoni, kuhusika katika mazungumzo, mwelekeo wa fadhili, nia ya kufuata na usomaji wa maandiko ya Biblia, na mwaliko wa kurudi tena kwa ajili ya mazungumzo zaidi.
Dak. 20: “Unganisha Trakti na Fasihi Nyinginezo.” Ipitiwe kwa maswali na majibu. Tia ndani maonyesho mafupi yanayotegemea madokezo kwenye mafungu 2-6. Zungumzia mambo kutoka kwa sanduku “Kumbuka Kutumia Broshua.”
Wimbo 14 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Aprili 12
Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Eleza mambo yoyote yaliyoonwa yenye kutokeza kuhusiana na uadhimisho wa Ukumbusho. Tia moyo wahubiri wote wafanye kazi na vikundi vyao vya utumishi wa shambani mwisho-juma huu.
Dak. 20: “Ziara za Kurudia Sahili na Zenye Matokeo.” Zungumza na wasikilizaji. Panga wonyesho mmoja unaoonyesha jinsi ya kuanzisha mazungumzo kwenye ziara ya kurudia.
Dak. 15: Sanduku la Swali. Mazungumzo chanya na yenye kutia moyo ya mwangalizi wa utumishi au mzee mwingine ambaye ametumikia akiwa painia msaidizi. Hoji mhubiri mmoja au wawili ambao hutumikia wakiwa mapainia wasaidizi mara kwa mara.
Wimbo 39 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Aprili 19
Dak. 10: Matangazo ya kwenu na matangazo yafaayo kutoka Huduma ya Ufalme Yetu. Soma ripoti ya hesabu na shukrani zozote za upaji. Soma Luka 6:38, na upongeze kundi kwa ukarimu wao katika kuitegemeza kazi ya ulimwenguni pote pamoja na mahitaji ya kundi.
Dak. 20: “Wasaidie Wapya Wafanye Maendeleo.” Mazungumzo kati ya viongozi wa funzo la kitabu wawili au watatu. Baada ya kupitia mambo makuu ya makala hiyo, eleza ni mipango gani imefanywa ili kutumia mapendekezo hayo kwenu. Tunaweza kusaidiaje wapya wenye kupendezwa waliohudhuria Ukumbusho? Wapya wanapaswa kutimiza matakwa gani ikiwa wanataka kushiriki katika utumishi wa shambani? Nini linaloweza kufanywa kusaidia watu mmoja mmoja ambao ushiriki wao umekuwa usio wa kawaida katika wakati uliopita? Wote wanaweza kutiwaje moyo wawe na ushiriki kamili kila mwezi? Wahubiri wenye nguvu zaidi wanaweza kusaidiaje wengine?—Rum. 15:1, 2.
Dak. 15: “‘Twendeni Nyumbani kwa Yehova.’” Pitio la maswali na majibu la mafungu 1-8 ya nyongeza. Pitia kifupi mambo makuu ya vichapo vinavyotajwa katika fungu la 7. Panga mhubiri mwenye ujuzi afanye wonyesho wa jinsi ya kusaidia mtu mpya kuelewa kwa nini tumepangwa kitengenezo kuwa makundi. (w84-E 11/1 uku. 15 maf. 6, 7) Eleza sehemu za mikutano yetu ambayo ni tofauti sana na ibada za kidini za Jumuiya ya Wakristo. Tia moyo wale wanaoongoza mafunzo ya Biblia watie ndani kila juma mazungumzo mafupi yanayokusudiwa kusaidia mwanafunzi asitawishe uthamini mkubwa zaidi kwa tengenezo na uhitaji wa kuwa sehemu yalo.
Wimbo 28 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Aprili 26
Dak. 15: Matangazo ya kwenu. Habari za Kitheokrasi. Mazungumzo ya makala “Kuishi kwa Utimamu wa Akili na Uadilifu.” Tia moyo akina ndugu wapange kimbele kuhudhuria programu ya Siku ya Kusanyiko la Pekee ya 1993. Sehemu hiyo yaweza kupitiwa ikiwa kundi limehudhuria tayari programu hiyo.
Dak. 13: “Kuzaliwa Mara ya Pili.” Kitabu Kutoa Sababu, kurasa 150-4. Wonyesho wa wahubiri wawili wakikutana na mtu fulani katika kazi ya nyumba kwa nyumba anayeuliza, “Je! nyinyi mmezaliwa mara ya pili?” Wahubiri waitikia kwa njia mojapo zinazopendekezwa kwenye kurasa 150-4. Baadaye, wahubiri wazungumzia kufanya ziara ya kurudia wakitumia mambo kutoka maandiko yaliyo kwenye mafungu 1-3 ukurasa 152.
Dak. 17: “‘Twendeni Nyumbani kwa Yehova.’” Pitio la maswali na majibu la mafungu 9-14 ya nyongeza. Ukitumia madokezo katika mafungu 12 na 13, panga mhubiri aonyeshe jinsi ya kuongea na mtu fulani anayesita-sita.
Wimbo 127 na sala ya kumalizia.