Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 3/00 kur. 3-6
  • Je, Twaweza Kufanya Aprili 2000 Kuwa Mwezi Wetu Bora Zaidi?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Je, Twaweza Kufanya Aprili 2000 Kuwa Mwezi Wetu Bora Zaidi?
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2000
  • Habari Zinazolingana
  • Je! Aprili Utakuwa Mwezi wa Pekee Kwako?
    Huduma Yetu ya Ufalme—1992
  • ‘Lihubiri Neno la Mungu Kikamili’
    Huduma Yetu ya Ufalme—2002
  • Aprili—Wakati wa ‘Kufanya Kazi kwa Bidii na Kujikakamua Wenyewe’
    Huduma Yetu ya Ufalme—2001
  • Mipango Yako Ni Ipi kwa Ajili ya Aprili?
    Huduma Yetu ya Ufalme—1988
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—2000
km 3/00 kur. 3-6

Je, Twaweza Kufanya Aprili 2000 Kuwa Mwezi Wetu Bora Zaidi?

1 Jumatano Aprili 19, itakuwa jioni kuu ya mwaka wetu wa utumishi. Siku hiyo, jua lituapo hatua kwa hatua duniani pote, kila kutaniko na kikundi cha Mashahidi wa Yehova ulimwenguni pote kitakuwa na Ukumbusho wa kifo cha Kristo. Hata iwe waishi katika sehemu gani ya kuhesabia siku na tarehe, kuadhimisha dhabihu ya Yesu Kristo kutakuwa tukio kuu la mwaka. Tarehe ya Ukumbusho imetiwa alama katika mwezi wa Aprili kwenye 2000 Calendar of Jehovah’s Witnesses.

2 Mwezi wote wa Aprili unatupatia fursa nzuri ya kuonyesha kwa njia ya nafsi yote uthamini wetu kwa fadhili zisizostahiliwa za Yehova alizotuonyesha kupitia dhabihu ya Mwanaye. Jinsi gani? Mtume Paulo aliandika hivi: “Upendo alio nao Kristo hutushurutisha, kwa sababu hili ndilo tumehukumu, kwamba mtu mmoja alikufa kwa ajili ya wote; kwa hiyo, basi, wote walikuwa wamekufa; naye alikufa kwa ajili ya wote ili wale waishio wapate kuishi si kwa ajili yao wenyewe tena, bali kwa ajili ya yeye aliyekufa kwa ajili yao na alifufuliwa.” (2 Kor. 5:14, 15) Naam, katika mwezi wa Aprili twaweza kuonyesha kwamba hatuishi kwa ajili yetu wenyewe, bali twaishi kwa ajili ya yeye aliyetufia, tukiufanya uwe mwezi bora zaidi tukiwa wahudumu wa Ufalme!

3 Jiandikishe Ufanye Upainia-Msaidizi Aprili: Mtume Paulo alituwekea kielelezo chenye kuchochea aliposema: “Siifanyi nafsi yangu kuwa kitu chenye thamani sana kwangu, kama tu ningepata kumaliza mwendo wangu na huduma niliyopokea ya Bwana Yesu, kutoa ushahidi kamili kuhusu habari njema ya fadhili isiyostahiliwa ya Mungu.” (Mdo. 20:24) Tuna pendeleo lilelile la kutoa ushahidi kamili juu ya Yehova Mungu. Tukiwa na lengo hilo, tungependa kufanya mwezi wa Aprili uwe bora zaidi katika kufanya upainia-msaidizi!

4 Ukiwa na miisho-juma mitano kamili, Aprili 2000 utakuwa mwezi bora kabisa kwa wengi kufanya upainia. Huko nyuma katika Aprili 1998, tulifikia kilele kikuu cha mapainia-wasaidizi, wale 3,924 walioshiriki waliwakilisha asilimia 13 ya jumla ya wahubiri. Mwaka mmoja baadaye, jumla ya idadi ya wahubiri ambao waliripoti Aprili 1999 iliongezeka kwa asilimia 10. Hiyo yamaanisha kwamba tuna uwezekano mkubwa wa kupita kilele chetu cha mwaka uliopita cha mapainia-wasaidizi. Kwa kuongezea, tangu wakati huo takwa la saa limepunguzwa, ikifanya wengi zaidi kutanikoni waweze kufanya utumishi huu. Kila mhubiri aliyebatizwa apaswa kufikiria kwa sala kama anaweza kufanya upainia-msaidizi mwezi huu wa Aprili.

5 Ukitumia mwezi wa Aprili kwenye 2000 Calendar, katika nyongeza hii, panga ratiba yako sasa kwa mwezi ujao. Amua ni siku gani utakazoweza kushiriki katika utumishi wa shambani, na uongeze muda wa saa unazoona unaweza kutumia katika kuhubiri mwezi huo. Tia ndani wakati unaoweza kutumia kutoa ushahidi rasmi na ushahidi wa kivivi hivi. Je, jumla inakaribia takwa la saa 50 kwa mapainia-wasaidizi? Ukikosa muda wa saa zinazotakiwa, je, unaweza kufanya marekebisho yoyote katika ratiba yako ili ununue wakati ufanye upainia-msaidizi? Utahitaji kutumia wastani wa saa moja na dakika 40 kila siku ili kufikia muda wa saa 50 kwa mwezi.

6 Sasa kwa kuwa takwa la saa limepunguzwa kwa mapainia wa kawaida, je, umekuwa ukifikiria kuingia utumishi wa wakati wote? Kwa nini ungoje hadi mwaka ujao ili uanze? Aprili utakuwa mwezi mzuri kuanza! Ikiwa huna uhakika juu ya uwezo wa kutimiza takwa la saa 70 la mapainia wa kawaida, kwa nini usifanye upainia-msaidizi Aprili na kuweka mradi wa saa 70? Unapoona kwamba unaweza, huenda ukajaza ombi la kujiunga na mapainia wa kawaida mara iwezekanapo.—Ona kitabu Huduma Yetu, ukurasa wa 113-114.

7 Shiriki Kikamili Ukiwa Mhubiri wa Habari Njema: Kwetu sote, wahubiri na mapainia vilevile, upendo wetu halisi kwa Mungu na kwa jirani hutuchochea tujitoe kwa nafsi yote kufanya yote tuwezayo katika utumishi wa Yehova kulingana na hali zetu za kibinafsi. (Luka 10:27) Hivyo basi, twaonyesha kwamba “tunafanya kazi kwa bidii na kujikakamua wenyewe, kwa sababu tumeweka tumaini letu juu ya Mungu aliye hai, ambaye ni Mwokozi wa namna zote za watu, hasa wa walio waaminifu.” (1 Tim. 4:10) Ndiyo sababu twapaswa kutazamia kuona asilimia 100 ikishiriki katika Aprili, kila mtu akishiriki kikamili katika kazi ya Ufalme.

8 Hebu tusisahau himizo la Yesu: “Mavuno ni mengi, lakini wafanyakazi ni wachache. Kwa hiyo, ombeni Bwana-mkubwa wa mavuno atume wafanyakazi katika mavuno yake.” Upesi baada ya kusema hayo, Yesu aliwaita mitume wake 12 na kuwatuma waende kuhubiri. (Mt. 9:37, 38; 10:1, 5, 7) Karibu mwaka mmoja hivi, baada ya wale 12 kuzoezwa vizuri katika utendaji wa kuhubiri, Yesu ‘alichagua sabini wengine na kuwatuma,’ akiwapa maagizo yaleyale: “Kwa kweli, mavuno ni mengi . . . Kwa hiyo mwombeni Bwana-mkubwa wa mavuno atume wafanyakazi katika mavuno yake.” (Luka 10:1, 2) Kitabu cha Biblia cha Matendo charipoti jinsi Yehova alivyojibu sala hizo. Kufikia Pentekoste 33 W.K., idadi ya wanafunzi iliongezeka ikawa karibu 120. Kisha, vilele vilivyofululiza vya wanafunzi 3,000 na 5,000 vikafikiwa. (Mdo. 1:15; 2:41; 4:4) Baada ya hapo, “idadi ya wanafunzi ikafuliza kuzidi sana.” (Mdo. 6:7) Vivyo hivyo, katika enzi ya sasa, lazima twendelee kumwomba Bwana-Mkubwa atume wahubiri zaidi wa Ufalme! Kupatana na sala zetu, kila mhubiri wa kutaniko apaswa kufanya mipango hususa ya kushiriki katika huduma kila mwezi.

9 Tafadhali angalia tena mwezi wa Aprili kwenye 2000 Calendar. Kwa kuwa siku mbili za kwanza za mwezi ni Jumamosi na Jumapili, je, unaweza kufanya mipango ya kushiriki katika utumishi mwisho-juma huo, ili upate kuanza mapema mwezi huo? Je, unaweza kuunga mkono kila “Siku ya Magazeti” mwezi huo pamoja na kikundi chako cha Funzo la Kitabu la Kutaniko? Vipi kutumia muda wa saa moja au zaidi kila Jumapili katika huduma? Je, unaweza kupanga kushiriki kutoa ushahidi jioni? Na usisahau kutwaa fursa za kutoa ushahidi vivi hivi kazini, shuleni, au popote pale utakapokuwa katika shughuli za kila siku. Tia alama siku utakazoweza kuwa katika huduma, na utumie kalenda kuandika saa zako za utumishi za mwezi huo.

10 Mwezi wa Aprili utakuwa wakati unaofaa kwa wote wanaostahili na waliopendekezwa na wazee kuanza kutumikia wakiwa wahubiri wasiobatizwa. Ikiwa unajifunza Biblia na mtu fulani, je, mtu huyo amefanya maendeleo kiasi cha kumwendea mwangalizi-msimamizi kumwuliza kama angeweza kuwa mhubiri wa habari njema? Ikiwa una watoto wasiobatizwa, je, umeongea juu ya maendeleo yao ya kiroho na wazee? Je, huo haungekuwa wakati mzuri kwao kuanza kuhubiri?—Ona kitabu Huduma Yetu, ukurasa wa 97-100.

11 Katika jitihada yetu ya kufanya Aprili 2000 kuwa mwezi bora zaidi, sisi sote twahitaji kushiriki katika huduma kisha kutoa ripoti zetu za utumishi wa shambani mwisho wa mwezi. (Linganisha Marko 6:30.) Wahubiri wapya wasiobatizwa ambao wanashiriki katika utumishi wa shambani kwa mara ya kwanza wanapaswa kutiwa moyo kuripoti utendaji wao bila kukawia. Kwa kufanya sehemu yetu, twaweza kuchangia vizuri kwenye ripoti ya Aprili na kwa sifa kuu itakayotolewa kwa Yehova kupitia jitihada zetu za kutoa ushahidi.

12 Leta Wengine Kwenye Ukumbusho: Je, hatutasisimuka kuona kilele kipya cha hudhurio la Ukumbusho wa kifo cha Kristo mwaka wa 2000? Ndiyo! Itamaanisha kwamba watu walio wengi zaidi walikuja kuonyesha uthamini wao kwa wonyesho mkuu zaidi wa upendo ambao Yehova Mungu na Yesu Kristo wametuonyesha! (Yn. 3:16; 15:13) Fanya mipango yoyote ya lazima ili chochote kisikuzuie wewe na familia yako kuhudhuria Ukumbusho.

13 Sasa pia ni wakati wa kuanza kualika wengine kwenye Ukumbusho. Andika orodha ya kila mtu unayetaka ahudhurie. Tia ndani yeyote ambaye amejifunza Biblia wakati uliopita, wale wanaojifunza sasa, na ziara zako zote za kurudia. Katika orodha yako ongeza wale unaowafahamu kazini, shuleni, na kwenye ujirani na pia yeyote unayefanya biashara naye. Usisahau kutia ndani watu unaowajua na watu wako wa jamaa. Baada ya kutayarisha orodha hiyo, anza kualika kila mmoja kwa bidii wewe binafsi. Elewesha wazi wakati na mahali pa Ukumbusho. Aprili 19 ikaribiapo, wakumbushe wale walio katika orodha yako, kwa kuwatembelea kibinafsi au kwa simu. Waalike waandamane nawe kwenye Ukumbusho usiku huo.

14 Kupatana na mwelekezo uliopita wa Sosaiti, baraza la wazee litafanya jitihada ya pekee ya kutia moyo wahubiri wote wasiotenda katika eneo wahudhurie Ukumbusho. (Mt. 18:12-14) Wazee watataka kupitia barua ya Sosaiti ya Februari 2, 1999. Mwandishi wa kutaniko ataandika orodha ya wahubiri wote wasiotenda, naye mwangalizi wa utumishi atawapa wazee mgawo wa kuwatembelea ili kuwaalika kwenye Ukumbusho. Labda kwa kufanyiwa ziara ya uchungaji yenye kutia moyo upesi iwezekanavyo, watu hao wasiotenda wanaweza kusaidiwa kuwa watendaji tena katika huduma ya shambani, hata katika mwezi wa Aprili. Itawatia moyo wakialikwa kushiriki katika utumishi wa shambani pamoja na mhubiri mwenye uzoefu.

15 Tia Moyo Kuwe na Tegemezo Kubwa Aprili! Itahitaji mambo yaratibiwe vizuri na wazee wote, watumishi wa huduma, na vichwa vya familia ili kufanya Aprili 2000 kuwa mwezi bora zaidi. Wazee watakuwa na bidii ya kupanga kila kitu vizuri na kuongoza. (Ebr. 13:7) Mipango ifaayo yahitaji kufanywa kwa ajili ya mikutano ya utumishi wa shambani siku za katikati ya juma na miisho-juma. Mikutano ya ziada ya utumishi huenda ikapangwa kwa ajili ya saa za baadaye alasiri na kwa utendaji jioni-jioni. Ratiba kamili ya mambo yote yaliyopangwa kwa mwezi wa Aprili yapasa kuwekwa kwenye ubao wa matangazo. Mtu fulani atahitaji kugawiwa ashughulikie kila mkutano wa utumishi uliopangwa. Eneo la kutosha lapaswa kuwako ili kuangalia mahitaji ya kila kikundi.

16 Toleo la mwezi wa Aprili litakuwa magazeti ya Mnara wa Mlinzi na Amkeni! Katika jitihada ya kuanzisha mafunzo ya Biblia ya nyumbani, broshua Anataka itatolewa kwa wote wanaoonyesha kupendezwa. Kwa sababu hiyo, magazeti na broshua za kutosha zahitaji kuandaliwa.

17 Mwishoni mwa mwezi, viongozi wote wa funzo la kitabu na wasaidizi wao watatia moyo kila mtu katika kikundi chao atoe ripoti ya utumishi wa shambani upesi baada ya mwisho wa mwezi. Watataka kutia moyo kila mmoja katika kikundi chao atoe ripoti yake ya utumishi mara baada ya mwezi kwisha. Labda jambo hilo laweza kufanywa hata Jumapili, Aprili 30. Kisha mwandishi anapokusanya ripoti, na kuona kwamba wahubiri wengine hawajatoa ripoti zao, anaweza kuwakumbusha kwa fadhili wafanye hivyo kabla ya Mei 6, wakati ambapo anapaswa kupeleka ripoti ya kutaniko kwa Sosaiti. Anaweza kuomba viongozi wa funzo la kitabu wamsaidie kuwasiliana na wahubiri mmoja-mmoja.

18 Majira ya Ukumbusho ndicho kipindi cha maana zaidi mwakani kwa watu wa Mungu. Wapaswa kuwa wakati wenye shughuli zaidi kwetu sote katika utumishi wa Yehova. Utakuwa mwezi wenye shughuli ikiwa kila mmoja wetu atashiriki kikamili iwezekanavyo akiwa mhubiri wa habari njema, ikiwa wale wanaojaza fomu za kuwa mapainia-wasaidizi watafanya hivyo, na ikiwa tutaalika wengine kwa bidii waje kwenye Ukumbusho wa kifo cha Kristo. Na tusali kwa bidii tupate baraka tele za Yehova tunapojitahidi kufanya Aprili 2000 kuwa mwezi bora zaidi, kwa ajili ya sifa na utukufu kwa Mungu!—Ebr. 13:15.

[Sanduku katika ukurasa wa 3]

Mapainia-Wasaidizi 3,924

Kilele Chetu Kikuu Zaidi:

(Aprili 1998)

[Picha katika ukurasa wa 4]

Jumla ya Wahubiri 35,740

Kilele Chetu Kikuu Zaidi:

(Agosti 1999)

[Picha katika ukurasa wa 5]

Hudhurio la Ukumbusho la 99,566

Kilele Chetu Kikuu Zaidi:

(1999)

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki