Ratiba Ya Mkutano Wa Utumishi
Juma Linaloanza Machi 13
Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Matangazo yaliyoteuliwa kutoka Huduma ya Ufalme Yetu.
Dak. 15: “Twahubiri Habari Njema.” Toa utangulizi usiozidi dakika moja, na ufuatie kwa mazungumzo ya maswali na majibu. Toa vielelezo vya Kimaandiko vyenye kujenga vinavyoweza kukaziwa kwenye kitabu Ujuzi tunapokitoa katika huduma.
Dak. 20: “Je, Twaweza Kufanya Aprili 2000 Kuwa Mwezi Wetu Bora Zaidi?” (Fungu la 1-11) Maswali na majibu. Taja kilele cha idadi ya mapainia-wasaidizi katika historia ya karibuni ya kutaniko. Panga wengine ambao wako miongoni mwa idadi hiyo waeleze manufaa za kibinafsi walizopata kwa kuongeza ushiriki katika huduma. Tia moyo kutaniko lijitahidi kupata kilele kipya cha mapainia mwezi wa Aprili. Zungumzia sifa za ustahili zinazotajwa katika kitabu Huduma Yetu, ukurasa wa 113-114. Wahubiri wanaotaka kufanya upainia-msaidizi wanaweza kupata fomu baada ya mkutano.
Wimbo 187 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Machi 20
Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Ripoti ya hesabu. Habari za Kitheokrasi.
Dak. 15: “Naweza Kufanya Nini?” Kiongozi wa funzo la kitabu azungumzia makala hiyo na mtumishi wa huduma mmoja au wawili. Kwa sababu ya vizuizi mbalimbali, huenda wahubiri kadhaa wakahisi kwamba hawawezi kuchangia sana katika utendaji wa kutaniko. Zungumzia baadhi ya njia nyingi ambazo sisi sote tunaweza kuchangia ifaavyo kuimarisha kutaniko na kuendeleza kazi ya Ufalme. Malizia kwa kuonyesha jinsi kila mmoja anavyoweza ‘Kushiriki Kutoa Ripoti ya Mwisho.’—Ona Huduma Yetu, ukurasa wa 108-110.
Dak. 20: “Je, Twaweza Kufanya Aprili 2000 Kuwa Mwezi Wetu Bora Zaidi?” (Fungu la 12-18) Maswali na majibu. Tia ndani wonyesho mfupi wa jinsi ya kualika mtu unayemfahamu kwenye Ukumbusho. Chunguzeni mwezi wa Aprili kwenye 2000 Calendar, na ukazie mikutano ya utumishi iliyopangwa kwenu. Kumbusha kila mmoja apange ratiba inayofaa ili kushiriki kwa kadiri awezavyo katika huduma mwezi huo, hivyo, lengo likiwa kwamba kutaniko lishiriki kwa asilimia 100. Tia moyo wote wanaoweza wafanye upainia-msaidizi na wachukue fomu baada ya mkutano.
Wimbo 65 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Machi 27
Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Wakumbushe wote watoe ripoti zao za utumishi wa shambani za Machi. Tangaza majina ya wale watakaofanya upainia-msaidizi mwezi wa Aprili. Eleza kwamba si kuchelewa mno kujaza fomu. Eleza ratiba yote ya mikutano ya utumishi wa shambani iliyopangwa kwa ajili ya Aprili. Tia moyo kila mtu ashiriki katika huduma mwisho-juma huu, ili kuanza mwezi wa Aprili vizuri. Tutatoa nakala moja-moja za magazeti ya Mnara wa Mlinzi na Amkeni! mwezi huo. Kazia makala moja na jambo la kuzungumziwa ambalo laweza kutumiwa kwa matokeo katika utoaji mbalimbali wa kila ya matoleo hayo ya karibuni. Kila mtu apaswa kuwa na nakala ya broshua Anataka na kujitahidi kuitumia ili kuanzisha mafunzo ya Biblia na watu wenye kupendezwa.
Dak. 13: “Omba Msaada.” Hotuba na mazungumzo pamoja na wasikilizaji yakifanywa na mzee. Eleza jinsi sisi sote tulivyo na uhitaji wa msaada fulani mara kwa mara. Bila shaka, kila mmoja apaswa kubeba mzigo wake mwenyewe. (Gal. 6:5) Hata hivyo, tunaposhindwa kukabiliana na hali, hatupaswi kusitasita kutafuta msaada kutoka kwa mshiriki aliyekomaa wa kutaniko. Alika wasikilizaji wasimulie mambo yaliyoonwa kuonyesha jinsi ambavyo walitiwa moyo na msaada wenye fadhili ambao wengine waliwapa.
Dak. 10: Mahitaji ya kwenu. Tia ndani wonyesho uliofanyiwa mazoezi vizuri kuonyesha jinsi ya kutoa magazeti kwa mpango wa utoaji wa hiari.
Dak. 12: Pitia 2000 Yearbook. Mazungumzo pamoja na wasikilizaji na kupitia mambo makuu ya “1999 Grand Totals,” kwenye ukurasa wa 31. Pia zungumzia “A Letter From the Governing Body,” kwenye ukurasa wa 3-5. Omba watu fulani watoe maelezo ya jinsi watakavyotumia kitia-moyo kilichotolewa. Mahali ambapo hakuna 2000 Yearbook, tumia “Jumla Kuu” kama ionyeshwavyo katika Mnara wa Mlinzi, Januari 1, 2000. Kisha zungumzia “A Letter From the Governing Body,” ukurasa wa 3-5 wa 1999 Yearbook. Mahali ambapo hakuna Yearbook katika lugha ya kutaniko, mzee au mtumishi wa huduma agawiwe ambaye anaweza kutumia Yearbook ya lugha nyingine.
Wimbo 195 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Aprili 3
Dak. 10: Matangazo ya kwenu na mambo yaliyoonwa ya utumishi wa shambani juu ya kutoa vichapo kwa kutumia mpango mpya wa utoaji wa hiari. Tumia mambo yaliyoonwa ya karibuni yaliyoteuliwa kutoka katika eneo la kwenu ambayo yatatia moyo wengine washiriki.
Dak. 17: “Kujifunza Kitabu Unabii wa Danieli.” Maswali na majibu. Toa maelezo kifupi juu ya jinsi tunavyoweza kunufaika kutokana na kujifunza kitabu cha Biblia cha Danieli. (Ona sura ya 1, fungu la 15-17, katika kitabu Unabii wa Danieli.) Makutaniko ambayo hayatakuwa yakijifunza kitabu Unabii wa Danieli yatazungumzia manufaa za mkutano wa Funzo la Kitabu la Kutaniko kama ionyeshwavyo katika kitabu Huduma Yetu kwenye ukurasa wa 74 hadi 76. Tia moyo wote wahudhurie Funzo la Kitabu la Kutaniko kwa ukawaida.
Dak. 18: Je, Niripoti Kosa Zito? Hotuba yenye uzito itolewe na mzee, ikielekezwa hasa kwa vijana. Matatizo mengi yametokea katika jamii ya kisasa ambayo yamekuwa na matokeo mabaya kwa vijana: viwango vinavyoharibika vya adili, jeuri inayoongezeka, uraibu wa dawa za kulevya, na ukosefu wa staha kwa mamlaka. Matineja wengine huishi maisha maradufu, wakificha mwenendo wao usio mzuri. Hilo hutisha sana hali ya kiroho ya kutaniko lote. Wengine hufanya kosa zito na kutaka kulificha. Ukijua ndugu au dada katika kutaniko amefanya kinyume cha sheria ya Mungu, wapaswa kufanya nini? Fikiria kanuni iliyo kwenye Mambo ya Walawi 5:1. (Ona Mnara wa Mlinzi, Agosti 15, 1997, ukurasa wa 27-30.) Rejezea kitabu Vijana Huuliza, ukurasa wa 68-69, na ueleze kile ambacho mtu anapaswa kufanya katika kisa kama hicho.
Wimbo 68 na sala ya kumalizia.