Kushirikiana na Kiongozi Wetu wa Funzo la Kitabu la Kundi
1 Funzo la Kitabu la Kundi huwa na sehemu ya maana katika kusitawisha uwezo wetu tukiwa wahudumu wa habari njema. Vikundi hivyo hufanywa kuwa vidogo kimakusudi ili kuchochea hali ya uchangamfu, iliyo ya kifamilia kwa ajili ya funzo la Biblia na kimojawapo vichapo vya Sosaiti. Pia, vikundi hivyo vidogo huandaa hali zifaazo za kutuzoeza kuwa wenye matokeo zaidi katika huduma ya shambani. Kitia moyo cha kibinafsi na uangalifu hutolewa kwa utayari kwa watu mmoja mmoja kupitia mpango wa funzo la kitabu. Tunaweza kushirikianaje kikamili na kiongozi na kunufaika na uandalizi huo mzuri?
2 Kushiriki kwa Bidii Katika Huduma ya Shambani: Mojawapo daraka lililo la maana zaidi la kiongozi wa funzo la kitabu ni kusaidia kila mshiriki wa kikundi ashiriki kwa bidii katika huduma. Kuhusu hilo, kitabu Huduma Yetu hutukumbusha kwenye ukurasa 44 kwamba “ukawaida, bidii na shauku ambayo anaonyesha kwenye utendaji wa shambani itaonyeshwa na wahubiri.” Nyakati nyingine kiongozi atafanya kazi katika utumishi na washiriki wa familia yake mwenyewe, lakini pia atafurahi kuandamana na wengine katika sehemu mbalimbali za huduma kadiri hali zake zinavyoruhusu. Je! waweza kuunga mkono mikutano ya utumishi wa shambani kwa ukawaida? Kufanya hivyo kutathaminiwa sana na kiongozi wenu wa funzo la kitabu na wahubiri wengine.
3 Mikutano kwa ajili ya utumishi wa shambani hupangwa katika sehemu zifaazo ili wote waweze kushiriki kwa bidii katika kazi ya kuhubiri. Itafaa ikiwa kila kikundi kitaanza huduma mapema, huku kikifikiria hali za kwao. Wahubiri na mapainia wengi hupata mafanikio mazuri wanapoendelea katika huduma baada ya saa sita katika mwisho-juma.
4 Je! ungependa kupata msaada katika sehemu fulani ya huduma? Labda kiongozi wa funzo la kitabu lenu aweza kupanga ili mhubiri mwenye ujuzi katika kikundi afanye kazi nawe. Mwishoni mwa mwezi, hakikisha kutoa ripoti ya utumishi wa shambani bila kuchelewa. Kiongozi wa funzo la kitabu na mwandishi vilevile watathamini ushirikiano wako katika sehemu hiyo muhimu pia.—Linganisha Luka 16:10.
5 Wakati Mwangalizi wa Utumishi Anapozuru Kikundi: Kwa kawaida mwangalizi wa utumishi huzuru kikundi kimoja cha funzo la kitabu kila mwezi ili kutia moyo utendaji mwingi wenye matokeo zaidi katika huduma ya shambani. Sikiliza kwa uangalifu hotuba ya dakika 15 anayotoa kwenye umalizio wa funzo la kitabu, kwa kuwa itaandaa shauri hususa litakalosaidia kikundi kufanya maendeleo katika sehemu mbalimbali za kazi ya kuhubiri. Pia, mwangalizi wa utumishi ana hamu ya kufanya kazi pamoja na washiriki mbalimbali wa funzo la kitabu katika mwisho-juma. Hakikisha unatumia kwa faida uandalizi huo wa pekee ili uweze kunufaika na ustadi na uwezo wake wa shambani.
6 Mfano wetu binafsi wa ushirikiano na utayari wetu wa kusaidia wale wasio stadi sana utasaidia kuleta hali ya uchangamfu, iliyo ya kirafiki kwenye Funzo la Kitabu la Kundi huku ‘tukiwatendea watu wote mema, na hasa jamaa ya waaminio.’—Gal. 6:10.