Mikutano Ya Utumishi Kwa Februari
Juma Linaloanza Februari 1
Dak. 10: Matangazo ya kwenu na Matangazo yaliyoteuliwa kutoka Huduma ya Ufalme Yetu. Onyesha utoaji wa magazeti ukitegemea matoleo ya karibuni.
Dak. 20: “Kushirikiana na Kiongozi Wetu wa Funzo la Kitabu la Kundi.” Maswali na majibu.
Dak. 15: “Utoaji Mbalimbali Ulio Rahisi na Wenye Matokeo.” Zungumza pamoja na wasikilizaji. Unapopitia fungu la 3, toa wonyesho wa jinsi mhubiri anavyomfanya mwenye nyumba apendezwe na kitabu Kuishi Milele. Mwenye nyumba apaswa aonyeshe kupendezwa kwa waziwazi. Unapozungumzia fungu 5, onyesha jinsi mhubiri hutumia trakti ili kuendeleza mazungumzo na mwenye nyumba.
Wimbo 215 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Februari 8
Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Habari za Kitheokrasi
Dak. 20: “Ongoza Mafunzo ya Biblia Katika Kitabu Kuishi Milele.” Mazungumzo ya maswali na majibu. Baada ya kupitia fungu 6, onyesha jinsi kijana awezavyo kutoa na kuanzisha funzo la Biblia kwa kutumia kitabu Kuishi Milele. Simulia mambo yoyote yaliyoonwa ya kwenu ya wachanga ambao wameweza kuanzisha mafunzo.
Dak. 15: “Si Wachuuzi wa Neno la Mungu.” Hotuba na mwangalizi msimamizi au mzee mwingine ikitegemea kurasa 26-9 za Mnara wa Mlinzi la Desemba 1, 1992. Wapongeze akina ndugu kwa uchangamfu kwa ajili ya kushiriki kutegemeza kazi ya Sosaiti ya ulimwenguni pote kutia na kundi la kwenu. Huenda pia ukataja juu ya yale kundi linafanya katika kutegemeza miradi yoyote ya ujenzi ya kwenu ambayo labda inaendelea sasa.
Wimbo 53 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Februari 15
Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Ripoti ya hesabu. Toa maelezo ya Sosaiti ya uthamini kwa upaji uliopelekwa, na pongeza kundi kwa ajili ya utegemezo mwaminifu-mshikamanifu kwa mahitaji ya kundi lenu. Tia moyo ushiriki katika utendaji wa shambani mwisho-juma.
Dak. 20: “Kuwafundisha . . . Yote Niliyowaamuru Ninyi.” Ipitiwe kwa maswali na majibu pamoja na wasikilizaji. Unapozungumzia mafungu 4 na 5, toa mifano mingine ya maandiko na vichapo vinavyofaa hali za kwenu. Kuwe na wonyesho uliotayarishwa vizuri wa jinsi kiunzi chaweza kufanywa kutoka kwa mazungumzo yako ya utangulizi hadi kwa mojawapo trakti. Pitia fungu moja au mawili ya trakti hiyo kadiri wakati uruhusuvyo. Watie moyo wote waendelee kwa bidii-nyendelevu kujaribu kuanzisha mafunzo mapya ya Biblia.
Dak. 15: “Damu,” kitabu Kutoa Sababu, kurasa 52-53. Tumia kikao cha ziara ya kurudia ambapo mwenye nyumba auliza maswali yaliyo katika habari yenye maandishi mazito. Majibu ya mhubiri yapaswa yategemee maelezo kutoka kitabu Kutoa Sababu.
Wimbo 181 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Februari 22
Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Zungumzia mambo ya kunena kutoka kwa magazeti ya karibuni. Watie moyo wote washiriki katika utumishi wa shambani mwisho-juma huu.
Dak. 20: “Kuonyesha Uthamini Kwa Ajili ya Fidia.” Hotuba ikitolewa na mzee.
Dak. 15: Mahitaji ya kwenu au hotuba chanya ikitegemea habari katika makala ya Mnara wa Mlinzi la Oktoba 1, 1992, “Jifunze Utii kwa Kukubali Nidhamu.” Onyesha jinsi watumishi wote wa Yehova—vijana kwa wazee—hupokea nidhamu, na zungumzia manufaa yanayopatikana kwa kuwa na maoni chanya kuhusu nidhamu.
Wimbo 211 na sala ya kumalizia.