Wimbo 215
Kueneza Rehema kwa Wengine
1. Kale Yehova aliposema
Gharika iue waovu,
Ndipo agizo kapewa Noa:
‘Jenga safina! Uhubiri!’
Je! alikataa kwa sababu,
Hajajenga safina mbele?
La, aliitumia rehema,
Kajenga, kahubiri sana.
2. Mufumo wa kale unakoma,
Kwa rehema asema Mungu
Kwamba habari za mwisho wao
Zitolewe na kusikiwa.
Wasema “Siwezi kuhubiri
Kwa kuwa sijui kusema”?
Kama Mungu amekurehemu,
Roho itakusaidia.
3. Mungu ’meleta kweli, rehema,
Na furaha i katika “nchi.”
Lo! mwonjo wa hali za Ufalme
Zitakazotoka kwa Mungu!
Basi tuwarehemu wengine
Kwa kuwasihi watu wote:
Tenda sasa! Jiweke wakifu;
Uutumikie Ufalme.