Ongoza Mafunzo ya Biblia Katika Kitabu Kuishi Milele
1 Akirejezea kitabu Kuishi Milele, mwanamke mmoja alisema: “Kikiwa cha pili tu kwa Biblia yenyewe, nimepata kitabu hiki kuwa fasihi iliyo sahihi, yenye kutia moyo, na yenye kuchochea sana ambayo nimepata kusoma!” Sote tunakubali kwamba kitabu hicho ni kimojawapo vitabu bora zaidi kilichopata kutangazwa ili kusaidia watu waelewe Biblia na hasa kuwachochea wamsifu Yehova kwa bidii.
2 Katika 1982, mwaka ambao kitabu Kuishi Milele kilitolewa, wahubiri 6,414 walikuwa wanaongoza mafunzo ya Biblia 7,228 katika Afrika Mashariki. Sasa, wahubiri 18,603 huongoza mafunzo ya Biblia 29,750. Kufikia sasa, nakala milioni 62 za kitabu Kuishi Milele zimechapwa katika lugha 115. Jinsi kitabu hicho kinakuwa na matokeo makubwa katika kazi yetu ya ulimwenguni pote!
3 Weka Miradi: Ukuzi huo wenye kutokeza ni tokeo la baraka za Yehova na hamu ya watu wake ya kusaidia watu wanyofu kwa ujumbe wa Biblia wenye kuokoa uhai. (Rum. 10:13-15; 1 Tim. 2:4) Tunatambua uharaka wa nyakati na uhitaji wa bidii katika kupiga mbiu ya Ufalme wa Mungu.
4 Ingawa tengenezo linasonga mbele, vipi sisi mmoja mmoja. Je! tunaazimia kushiriki kikamili katika kazi ya maana ya kufanya wanafunzi? Ili kutimiza hayo, tunapaswa kuweka miradi ya kibinafsi. Je! tunaweza kuwa wenye bidii zaidi katika kufuatia kupendezwa? Kwa nini usiweke mradi wa kuanzisha funzo jipya la Biblia wakati wa mwezi wa Februari?
5 Ni Nani Awezaye Kuongoza Funzo la Biblia?: Wahubiri wengi kutoka malezi mbalimbali wamepata shangwe ya kuongoza funzo la Biblia katika kitabu Kuishi Milele. Uandishi wacho rahisi hufanya kuongoza kuwe rahisi zaidi, ukiwezesha hata wahubiri wapya zaidi kuwa na ushiriki katika kazi hiyo ya maana. Kwa kuongezea, wengi wetu tumekisoma sisi binafsi, kwa hiyo tunafahamu yaliyomo. Mhubiri mmoja ambaye hakuwa amepata kuongoza mafunzo ya Biblia hapo mbeleni kwa kutumia kitabu Kuishi Milele aliandika hivi kwa uthamini: “Nina mafunzo matatu na niko tayari kuanzisha la nne. Siwezi kuwashukuru vya kutosha kwa kufanya kuongoza mafunzo ya Biblia kuwe rahisi.”
6 Wachanga pia wanashiriki kwa bidii katika kazi ya kuongoza mafunzo ya Biblia kwa kutumia kitabu Kuishi Milele. Ndugu mmoja mchanga huacha kitabu hicho juu ya dawati lake shuleni. Hiyo imefanya kuwe na mazungumzo mazuri na mafunzo kadha ya Biblia. Wachanga wengine wametumia mfikio wa moja kwa moja kwa kuwaomba wazazi wanaowakuta katika huduma ya nyumba kwa nyumba ruhusa ya kuongoza funzo la Biblia na watoto wao. Watoto wetu si wachanga mno wasiweze kusema juu ya ahadi ya Yehova kwa ajili ya uhai wa milele katika dunia paradiso.
7 Tuwe wachanga au wazee, mojawapo shangwe kuu zaidi ambayo yeyote aweza kupata katika huduma ni ile ya kuongoza funzo la Biblia nyumbani. Kwa hiyo acheni kila mmoja wetu asali ili apate msaada wa Yehova na kutumia kila fursa ili kujulisha tumaini letu hadharani. Tumia kitabu Kuishi Milele ili kusaidia wengine wajifunze jinsi wanavyoweza kushiriki katika kumsifu Mungu, Yehova.—Zab. 148:12, 13.