Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 9/91 uku. 4
  • Sehemu ya 3: Kituo Kikuu kwa Huduma ya Shambani

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Sehemu ya 3: Kituo Kikuu kwa Huduma ya Shambani
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1991
  • Habari Zinazolingana
  • Kushirikiana na Kiongozi Wetu wa Funzo la Kitabu la Kundi
    Huduma Yetu ya Ufalme—1993
  • Mikutano ya Utumishi wa Shambani Inayotimiza Kusudi Lake
    Huduma Yetu ya Ufalme—2015
  • Funzo la Kitabu la Kutaniko Huchochea Utendaji Wenye Kuelimisha
    Huduma Yetu ya Ufalme—1994
  • Mikutano ya Utumishi wa Shambani
    Huduma ya Ufalme—2009
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—1991
km 9/91 uku. 4

Mpango wa Funzo la Kitabu la Kundi

Sehemu ya 3: Kituo Kikuu kwa Huduma ya Shambani

1 Pamoja na kuandaa mahali pa funzo la kikundi, mahali pa Funzo la Kitabu la Kundi hutumika kuwa mahali pa kukutania kwa ajili ya utumishi wa shambani. Nyakati za mikutano hiyo zapasa ziwafae wahubiri walio wengi, na mikutano yapasa kutoa usaidizi wenye kutumika katika kuwapanga wahubiri kwa utumishi wa shambani.

2 Vikundi vilivyopangwa ifaavyo kwa ajili ya funzo na utumishi hujenga hali ya kiroho. Ni nani ambaye hakufaidika kwa kitia-moyo na madokezo ya jinsi ya kushughulikia vipingamizi, jinsi ya kuanzisha mazungumzo, au mambo ya kusema katika ziara ya kurudia? Wahubiri wenzetu na mapainia wanaokutania mahali pa funzo la kitabu huandaa usaidizi kama huo.—Gal. 6:9, 10.

3 Daraka la Kiongozi: Kiongozi wa Fu- nzo la Kitabu la Kundi huongoza na ndiye mwenye daraka la kupanga utendaji wa kikundi. Yeye hufanya kazi na wahubiri kwa ukawaida shambani. (1 Pet. 5:2, 3) Mikutano ya utumishi iliyotayarishwa vizuri hukipa kikundi mafundisho ya Kimaandiko na yenye kutumika kukitayarisha kikundi kwa utumishi wa shammbani. Kwa kawaida inafaa zaidi kila kikundi cha funzo la kitabu kiwe na mkutano wao wenyewe wa utumishi wa shambani badala ya vikundi vyote kukutana pamoja mahali pamoja. Hata hivyo vikundi viwili vidogo vyaweza kuungana ikihitajiwa. Utumishi wa shambani ukifuata Funzo la Mnara wa Mlinzi, mkutano wa utumishi wa shambani wapaswa uwe mfupi. Baada ya hapo, kila kiongozi wa funzo la kitabu atashughulikia kikundi chake mwenyewe.

4 Mipango ya utumishi wa shambani ya ukawaida hutia moyo ushiriki katika huduma. Mikutano ya utumishi ikifanywa wakati na mahali iliporatibiwa, wahubiri hufanya mipango yao kwa kulingana nayo, wakitiwa moyo kwa kujua kwamba eneo litapatikana na wengine wa kufanya kazi nao. (Linganisha Luka 10:1.) Hata wakati ambao kiongozi wa funzo la kitabu hawezi kuwapo, yeye huandaa eneo na kufanya mipango kwa ajili ya kikundi. (om-SW kur. 44-5) Ikiwa hakuna ndugu anayestahili anayepatikana kuongoza mkutano wa utumishi, kiongozi humpa mgawo dada afanye hivyo. (om-SW kur. 77-8; km-SW 3/88 uku. 3) Mvurugo unaepukwa wakati kikundi kinapokutana kwa ukawaida katika wakati na mahali pao pa kawaida kwa ajili ya utumishi. Rekebisho lolote la muda katika jambo hilo lapasa litangulie kutangazwa juma moja ikiwezekana.

5 Ushirikiano Wahitajiwa: Wote wa- paswa wajitahidi kuwa na ushiriki wenye umaana katika zile pande mbalimbali za huduma ya shambani. Wahubiri waweza kuchukua hatua ya kwanza kutayarisha pamoja wakiwa na pindi za mazoezi, wakitumia vipingamizi vinavyopatikana kihalisi na hali ambazo yaelekea zaweza kutokea katika eneo lenu.—Mit. 27:17.

6 Je! ungependa mhubiri mwenye ujuzi akusaidie uwe stadi zaidi katika kazi ya kufanya wanafunzi? Ikiwa ndivyo, sema na kiongozi wenu wa Funzo la Kitabu la Kundi. Anaweza kupanga usaidiwe na mhubiri anayestahili. Ili ufaidike, tumia kwa bidii yenye kuendelea madokezo unayopokea na kutimiza miadi inayofanywa.

7 Wale wanaopewa migawo na kiongozi wa funzo la kitabu wapaswa kuwa wenye kusaidia na wenye kiasi katika matarajio yao. Mambo yaliyoonwa yameonyesha kwamba wale wenye maoni yanayofaa na yenye usawaziko kuelekea utumishi wa shambani na ambao wana njia zenye kutumika ndio wawezao zaidi kuzoeza wengine. (km-SW 8/79 uku. 2; km-SW 9/79 uku. 2) Sikuzote pongezi lapasa kutolewa maendeleo yanapofanywa. Ndipo miradi mingine yaweza kuwekwa.—Linganisha Luka 19:17-19.

8 Twataka kusaidiana mmoja na mwenzake, tuwe wenye mafanikio katika kuhubiri habari njema na kufanya wanafunzi. Hali za ulimwengu zenye kuzidi kuwa mbaya zashuhudia uharaka wa kazi hii. Maisha zinahusika, na Yehova anahimiza kazi ya kukusanya. (Isa. 60:22) Tukumbukapo huduma tuliyopewa, tutafanya kazi karibu karibu na kikundi chetu cha Funzo la Kitabu la Kundi kutimiza mgawo wetu kikamili huku tukihimizana na kutiana moyo mmoja na mwenzake.—Rum. 12:6-8; 2 Tim. 4:1, 2, 5.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki