Habari Za Kitheokrasi
Japan: Kilele chao kipya cha wahubiri katika Machi kilikuwa 177,591.
Kambodia: Katika Februari 8, 1993, cheti cha kisheria kilipokewa ambacho kinaruhusu kazi yetu na kufungua njia kwa wamishonari kuingia nchini. Tuna furaha kwamba baada ya miaka 25, habari njema zinahubiriwa waziwazi tena katika Kambodia.
Liberia: Wakati wa Machi akina ndugu waliweza kuwa na “Wachukuaji Nuru” Mkusanyiko wa Wilaya kwenye ardhi ya Sosaiti iliyo jirani ya ofisi ya tawi. Kilele cha wahudhuriaji kilikuwa 2,711, na 78 walibatizwa.
Saiprasi: Pamoja na kilele kipya cha wahubiri 1,462 katika Machi, tawi liliripoti vilele katika saa, ziara za kurudia, na mafunzo ya Biblia.
Ufilipino: Kilele kipya cha wahubiri 115,044 kilifikiwa katika Machi.