Rudi Ulikopata Kupendezwa
1 Wengi wetu tumefanikiwa kugawa magazeti na broshua. Ni jambo la maana turudi na kujaribu kuchochea kupendezwa zaidi. Mafanikio yetu katika kufanya hivyo huenda yakategemea ni kwa uzuri wa kadiri gani sisi hujitayarisha kabla ya kufanya ziara ya kurudia.
2 Kujitayarisha huanza na kuweka habari za maelezo marefu juu ya kumbukumbu la nyumba kwa nyumba. Angalia habari iliyozungumzwa katika ziara ya kwanza na itikio la mwenye nyumba. Huenda hata ukataka kuandika jinsi utakavyo kuanza mazungumzo urudipo.
3 Kwa kielelezo, ikiwa ulikazia “Mnara wa Mlinzi,” la Aprili 15, ungeweza kutaarifu jambo kama hili:
◼ “Katika ziara yangu iliyotangulia tulizungumzia mahali tuwezapo kupata mwongozo wenye kutumainika leo. Kuhusiana na wazo hilo, tafadhali angalia kile ambacho broshua hii, Je! Kweli Mungu Anatujali?, yaonyesha kuwa ndizo ahadi za Mungu zenye kutumainika kwa wakati ujao.” Halafu tumia habari zilizo chini ya Sehemu ya 10 kuanzia ukurasa wa 22 ili kuthibitisha baraka za mapenzi ya Mungu zitafanywa duniani.
4 Katika kutoa broshua, mfikio mwingine ungeweza kuwa:
◼ “Safari ile nyingine nilifurahia mazungumzo yetu mafupi juu ya wakati ujao wa dunia hii. Je! waweza kuwazia maisha yatakuwaje hapa Mungu amalizapo uovu na mateso? [Onyesha picha katika ukurasa 31 wa broshua Ni Nini Lililo Kusudi la Uhai—Wewe Waweza Kulipataje?] Angalia mistari yote hii ya Biblia katika kurasa 29 na 30 ielezayo baraka ambazo Ufalme wa Mungu utaleta. [Chagua andiko moja, na ulisome moja kwa moja katika broshua.] Ningependa kukuachia hii.”
5 Urudipo, labda utapata kujua kwamba mwenye nyumba hupokea fasihi yake mwenyewe ya kidini na ahisi kwamba hiyo yamtosha. Ungeweza kusema hivi:
◼ “Hata dini yetu iwe ipi, sisi sote huathiriwa na mengi ya mahangaiko yaleyale—uhalifu, ugonjwa mahututi, mahangaiko ya kimazingira—sivyo? [Ruhusu elezo.] Je! wewe wahisi kuna utatuzi wowote halisi kwa matatizo hayo? [Soma 2 Petro 3:13.] Kusudi la fasihi yetu lataarifiwa katika ukurasa 2 wa Mnara wa Mlinzi. [Soma sentensi moja au mbili zilizochaguliwa.] Watu wengi wasio Mashahidi wa Yehova hufurahia kusoma vichapo vyetu kwa sababu ya ujumbe wenye tumaini uliomo, ulio na msingi wa Biblia.” Halafu ungeweza kueleza programu yetu ya kujifunza Biblia.
6 Ungeweza kutumia mfikio huu:
◼ “Safari ya mwisho nilipokuwa hapa, tuliongea juu ya matazamio ya wakati ujao kwa ulimwengu wetu. Waionaje ripoti hii? [Taja kihabari fulani cha karibuni chenye kuhangaisha.] Watu wasikiapo mambo kama hayo, huwafanya washangae ulimwengu huu unaelekea wapi, sivyo? Sisi twaamini kwamba mambo hayo yaonyesha kwamba tunaishi katika ‘siku za mwisho’ zilizotabiriwa katika Biblia kwenye 2 Timotheo 3:1-5.” Baada ya kusoma mambo makuu, waweza kuuliza kama ameona watu wenye kulingana na elezo hilo. Endelea kuzungumzia kichwa kidogo kimojapo katika kurasa 297-301 katika kitabu Kutoa Sababu.
7 Tukijitayarisha vizuri na kuonyesha tamaa ya kweli ya kusaidia, twaweza kuwa na uhakika kwamba walio na mioyo ya kufuata haki watasikiliza.—Yn. 10:27, 28.