Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 7/94 uku. 4
  • Watasikiaje Bila Sisi Kurudi?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Watasikiaje Bila Sisi Kurudi?
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1994
  • Habari Zinazolingana
  • Ziara za Kurudia Sahili na Zenye Matokeo
    Huduma Yetu ya Ufalme—1993
  • Wasaidie Wengine Wajifunze Kweli
    Huduma Yetu ya Ufalme—1994
  • Jenga Kupendezwa kwa Kufanya Ziara za Kurudia Zenye Matokeo
    Huduma Yetu ya Ufalme—1993
  • Jifunze Biblia na Watu Wanaochukua Magazeti
    Huduma ya Ufalme—2007
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—1994
km 7/94 uku. 4

Watasikiaje Bila Sisi Kurudi?

1 “Wamsikieje bila mhubiri?” (Rum. 10:14) Kwa kweli, watapataje maana ya kweli tusipofanya ziara za kurudia zenye matokeo? Ziara yoyote tuliyoweza kuongea na mwenye nyumba juu ya ujumbe wa Ufalme yastahili ziara ya kurudia. Mwezi huu huenda tukaweza kufuatia mazungumzo yetu ya kwanza tukiwa na mawazo ya ziada ya Kimaandiko kutoka kijitabu chochote tulichoangusha, na kinachoweza kuongoza kimafanikio kwenye funzo la Biblia.

2 Ikiwa uliangusha kijitabu “Wakati Ujao Salama—Jinsi Unavyoweza Kuuona,” unaweza kuanzisha mazungumzo ambayo yataongoza kwenye funzo la Biblia kwa njia hii. Ukielekeza kwenye jalada la mbele, unaweza kusema:

◼ “Ungependa kuishi katika ulimwengu ambamo wakati ujao salama umehakikishiwa kwako na kwa familia yako? [Ruhusu itikio. Kisha geukia fungu la 2.] Sisi sote twashiriki tamaa hii, ijapokuwa wengi wanatia shaka kuwa itawezekana. Kwa Mungu, anayeahidi kufanya hili liwe halisi, si jambo lisilowezekana.” Soma Isaya 32:17, 18 kama ilivyonukuliwa katika fungu la 2, au usome kutoka Biblia yako. Endelea, kueleza kwamba kuna watu ulimwenguni pote ambao tayari wanaona shangwe na amani ya akili inayotokana na tumaini hakika la wakati ujao. Zungumzia mawazo ya Kimaandiko katika fungu la 3, kisha eleza jinsi funzo la kijitabu laweza kusaidia mwenye nyumba ajifunze zaidi. Mtu huyo akipendezwa, fanya mipango ya ziara za kurudia upesi kwa lengo la kuanzisha funzo la Biblia.

3 Unaporudi baada ya kuangusha kijitabu “Je! Mungu Anajali,” labda jambo kama hili litakuwa na matokeo:

◼ “Wakati wa ziara yangu iliyopita, tulizungumza juu ya swali, Je! Mungu anajali? Wafikiri Mungu hutujali ili akomeshe kuteseka na jeuri? [Baada ya mtu kuitikia, geukia fungu la 32, nawe uendelee.] Mungu ameahidi kuondoa ulimwengu huu mbovu na kuleta ule mpya utakaokaliwa na watu wazuri ambao wataweza kuishi kwa amani. [Soma Zaburi 37:11.] Wewe nami twaweza pia kufurahia maisha katika ulimwengu huo mpya ikiwa twaamini Biblia na kutumia shauri layo.” Eleza juu ya programu yetu ya kusaidia watu wajifunze Biblia.

4 Unapofanya ziara ya kurudia baada ya kuangusha broshua “Tazama! Mimi Ninafanya Vitu Vyote Kuwa Vipya,” unaweza kuanza kwa kuonyesha picha kwenye jalada na kisha uulize swali:

◼ “Unafikiri itakuwaje kuishi katika ulimwengu mkamilifu? [Pata maelezo ya mwenye nyumba.] Unayoona kwenye picha hii si mawazio tu; yanategemea ahadi hakika zilizoandikwa katika Biblia. [Soma Ufunuo 21:4 na Zaburi 37:11, 29.] Ningependa kueleza jinsi wewe na familia yako mwaweza kufurahia baraka hii.” Endeleza mazungumzo, na utoe funzo la Biblia.

5 Tunapopata watu wenye mioyo minyoofu wanaotafuta kweli, twaonyesha upendo wetu wa kweli kwa kurudi ili kuwasaidia watende kulingana na yale wamesikia. Twatumia kweli takatifu tulizokabidhiwa kwa ajili ya baraka za milele kwetu wenyewe na wale wasikilizao.—1 Tim. 4:16.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki