Wasaidie Wengine Wajifunze Kweli
1 Yesu alikuja duniani ili kutoa ushahidi juu ya ile kweli. Ili wengine wahubiriwe ile kweli, aliwazoeza wanafunzi wake wawe wafundishaji. Alikuwa na uhakika sana juu ya kufanikiwa kwao katika kufundisha wengine hivi kwamba aliwaita ‘wafunzi wa umma.’ (Mt. 13:52, NW) Alifananisha kila mmoja na mtu msomi mwenye hazina halisi kwenye ghala ya kutoa katika hiyo. Wanafunzi wa Yesu leo hutumia vichapo ili kuharakisha kazi ya kuhubiri Ufalme. Kwa kielelezo, makutaniko mengi yana vijitabu mbalimbali vya kutumia ili kusaidia wengine wawe wanafunzi. Vyombo hivi vya thamani vyaweza kutumiwaje?
2 Ili kuanzisha mazungumzo yanayoongoza kwenye kutoa kijitabu “Wakati Ujao Salama—Jinsi Unavyoweza Kuuona,” unaweza kuuliza:
◼ “Je! umepata kujiuliza ni kwa nini kwamba ijapokuwa jitihada zote za mwanadamu, matazamio ya wakati ujao salama waonekana ukikosa tumaini? [Ruhusu itikio.] Biblia hueleza ni kwa nini jitihada nyingi zimeshindwa kufaulu.” Soma Zaburi 146:3, 4. Baada ya kutoa sababu na mwenye nyumba juu ya habari iliyo kwenye fungu la 6, unaweza kuuliza: “Ni nani hasa awezaye kutupatia usalama wa kudumu?” Kwa kutegemea itikio la mwenye nyumba, unaweza kuamua kuzungumzia mambo yafaayo kutoka fungu la 7 kabla ya kutoa toleo.
3 Hapa kuna njia moja unayoweza kutumia kijitabu “Je! Mungu Anajali?”:
◼ “Watu wengi wameuliza swali linalopatikana kwenye maelezo mafupi chini ya vielelezo hivi viwili. [Soma swali lililo chini ya kurasa 6 na 7, na uruhusu itikio.] Kwa kuwa Mungu mwenye upendo hatatetea mema na mabaya wakati uleule, unafikiri nini kuhusu ahadi yake iliyorekodiwa hapa kwenye Isaya 65:21-24?” Ukipata elezo linaloonyesha kupendezwa kwa kadiri fulani, geukia fungu la 37, nawe ueleze litakalotimizwa na Ufalme wa Mungu.
4 Unapotoa kijitabu “There Is Much More to Life!,” unaweza kusema:
◼ “Kwa wengi thamani ya maisha imepungua ikawa yenye kutia huzuni, yenye uchovu wa kulemea. Unafikiri ni nini kinachohitajiwa ili kufanya maisha yawe ya maana? [Acha mwenye nyumba aeleze maoni yake.] Biblia yaonyesha kwamba Mungu ana mambo mazuri yanayotungojea. Ona analosema hapa kwenye Ufunuo 21:4, 5.” Ikifaa, endelea na mazungumzo na mambo ya kutoka fungu la 42 la kijitabu hicho.
5 Kwa kutumia broshua “Furahia Milele Maisha Duniani!,” mhubiri mchanga anaweza kuuliza:
◼ “Je! ungependa kuishi katika dunia-paradiso kama hii? [Onyesha mwanzo na nyuma ya jalada, na uruhusu elezo.] Familia yangu nami twatazamia kuishi humo kwa sababu ya yale ambayo Biblia yasema hapa kwenye Yohana 17:3.” Kupendezwa kukionekana baada ya kusoma andiko, mtolee broshua ili mtu huyo aisome.
6 Ikiwa unatumia vijitabu au broshua nyinginezo katika huduma yako mwezi huu, unaweza kufuatisha matangulizi na utoaji wako kulingana na mtindo wa madokezo yaliyoorodheshwa mwanzoni. Kumbuka kufupiza na kutoa maelezo chanya na yenye kujenga ili kuamsha upendezi wa wenye nyumba.
7 Yehova ametupatia kweli. Twapaswa kutumia fursa zilizo mbele yetu kuzishiriki na wengine, kwa namna ya vichapo na kwa mazungumzo pamoja na watu tunaowapata. Kwa njia hii twathibitika kuwa wafunzi wa umma kwa ajili ya manufaa za kudumu za wengine.—Mt. 28:19, 20.