Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 1/12 kur. 1-4
  • Je, Unazitumia Broshua Hizi?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Je, Unazitumia Broshua Hizi?
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2012
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Biblia—Ina Ujumbe Gani?
  • Kitabu kwa Ajili ya Watu Wote
  • Wewe Unaweza Kuwa Rafiki ya Mungu!
  • Jinsi ya Kupata Maisha Yenye Kuridhisha
  • Maswali Matano Muhimu Kuhusu Chanzo cha Uhai
  • Why Should We Worship God in Love and Truth?
  • The Pathway to Peace and Happiness
  • Our Problems​—Who Will Help Us Solve Them?
  • Je! Ulimwengu Usio na Vita Utakuwako Wakati Wowote?
  • Mwongozo Wa Mungu—Njia Yetu ya Kwenda Paradiso
  • Imani ya Kweli—Siri ya Kuwa na Maisha Yenye Furaha
  • Lasting Peace and Happiness—How to Find Them
  • Broshua Mpya Tutakayotoa!
    Huduma Yetu ya Ufalme—2010
  • Jinsi ya Kutumia Broshua Habari Njema Kutoka kwa Mungu!
    Huduma ya Ufalme—2013
  • Mwige Yehova kwa Kujali Wengine Kikweli
    Huduma Yetu ya Ufalme—1996
  • Tumia Broshua Mbalimbali Katika Huduma Yako
    Huduma Yetu ya Ufalme—1995
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—2012
km 1/12 kur. 1-4

Tunza

Je, Unazitumia Broshua Hizi?

Biblia—Ina Ujumbe Gani?

Imekusudiwa kuwavutia watu wasiojua mengi kuhusu Biblia, hasa watu ambao ni wafuasi wa dini zisizo za Kikristo

Jinsi ya kuitoa: “Tungependa kusikia maoni yako kuhusu maneno haya ya Maandiko (au kitabu hiki kitakatifu). [Soma andiko la Zaburi 37:11, linalorejelewa katika sehemu ya 11.] Je, unafikiri hali zitakuwaje duniani wakati unabii huu utakapotimia? [Mruhusu ajibu.] Hii ni mojawapo ya ahadi za Biblia zinazowapa watu wa tamaduni na dini zote tumaini na faraja.” Soma fungu lililo juu katika ukurasa wa 3, na umtolee mwenye nyumba broshua.

Jaribu njia hii: Endapo unajifunza kitabu Biblia Inafundisha pamoja na mtu aliye mfuasi wa dini isiyo ya Kikristo, tenga dakika chache mwanzoni au mwishoni mwa kila kipindi cha funzo kuzungumzia sehemu moja ya broshua hii ili kumsaidia kuelewa matukio muhimu ya Biblia.

Kitabu kwa Ajili ya Watu Wote

Imekusudiwa kuwavutia watu wenye elimu ambao hawajui mengi kuhusu Biblia

Jinsi ya kuitoa: Soma 2 Timotheo 3:16, 17, kisha useme hivi: “Je, unakubali kwamba waandikaji wa Biblia waliongozwa na roho ya Mungu? Au unafikiri Biblia ni kitabu kizuri tu? [Mruhusu ajibu.] Ingawa watu wengi wana maoni yao kuhusu jambo hili, sisi tumeona kwamba ni wachache tu kati yao ambao wameichunguza Biblia. [Soma jambo lililoonwa chini ya kichwa kikuu katika ukurasa wa 3.] Broshua hii inawapa watu wa malezi na dini zote sababu nzuri za kuichunguza Biblia.”

Jaribu njia hii: Mwenye nyumba akiikubali broshua, sema hivi: “Watu wengi hawaoni umuhimu wa kusoma Biblia kwa sababu wafuasi wa dini hawafuati sheria za Biblia wala kufundisha kweli za Biblia. Nitakaporudi ningependa kukuonyesha mfano mmoja.” Utakaporudi, zungumzieni habari katika ukurasa wa 4-5.

Wewe Unaweza Kuwa Rafiki ya Mungu!

Imekusudiwa kuwavutia watu ambao hawana elimu, au wasiojua kusoma vizuri

Jinsi ya kuitoa: “Je, unafikiri sisi tunaweza kuwa rafiki za Mungu? [Mruhusu ajibu, kisha usome Yakobo 2:23.] Broshua hii imechapishwa ili kutusaidia kuwa rafiki za Mungu, kama Abrahamu alivyokuwa.”

Jaribu njia hii: Katika ziara ya kwanza au ziara ya kurudia, mwonyeshe mwenye nyumba jinsi ya kujifunza Biblia kwa kuzungumzia mafungu yote au mafungu machache tu ya somo la 1.

Jinsi ya Kupata Maisha Yenye Kuridhisha

Imekusudiwa kuwavutia watu ambao si wanadini

Jinsi ya kuitoa: “Tunakutembelea leo kwa sababu tumeona kwamba watu wengi wangependa kupata uradhi zaidi maishani. Sote tunapatwa na matatizo yanayoweza kufanya tukose furaha. Tunapopatwa na matatizo, huenda tukamwendea mtu wa ukoo au rafiki tunayemwamini ili kupata ushauri. Huenda pia tukatafuta ushauri katika vitabu au kwenye Intaneti. Wewe umepata ushauri mzuri wapi? [Mruhusu ajibu.] Baadhi ya watu wameshangaa kuona kwamba Biblia ina ushauri mzuri sana. Ushauri mmoja unazungumziwa hapa. [Mwonyeshe mwenye nyumba sura ya 2, na usome andiko moja lililonukuliwa.] Broshua hii imechapishwa ili kutusaidia tuwe na maisha yanayoridhisha zaidi.”

Jaribu njia hii: Mwenye nyumba akiikubali broshua, sema hivi: “Watu wengi wamesikia kwamba Biblia ina habari nyingi zisizo sahihi. Nitakaporudi, ningependa kukuonyesha jambo moja linaloonyesha kwamba Biblia ni sahihi kisayansi.” Utakaporudi zungumzieni fungu la 4 katika ukurasa wa 12.

Maswali Matano Muhimu Kuhusu Chanzo cha Uhai

Imekusudiwa kuwavutia vijana Wakristo ambao wanafundishwa mageuzi shuleni, na pia kutusaidia tunapozungumza na watu wanaoamini mageuzi, watu wanaoamini kwamba haiwezekani kujua kama kuna Mungu, na watu ambao hawaamini kwamba kuna Mungu (Broshua hii haijakusudiwa kutolewa nyumba kwa nyumba.)

Jinsi ya kuitumia tunapozungumza na mtu anayeamini mageuzi au mtu ambaye haamini kwamba kuna Mungu: “Karibu vitabu vyote vya sayansi vya siku hizi vinafundisha kwamba viumbe hai walitokana na mageuzi. Je, unafikiri nadharia ya mageuzi imethibitishwa kuwa ya kweli? [Mruhusu ajibu.] Bila shaka, unakubali kwamba ni muhimu kuchunguza maoni yote kuhusu jambo fulani kabla ya kuamua kile tutakachoamini. Broshua hii inazungumzia baadhi ya mambo ambayo yamewasadikisha watu wengi kwamba viumbe hai waliumbwa.”

Jaribu njia hii: Endapo wewe ni mwanafunzi wa shule, acha broshua kwenye dawati lako. Huenda baadhi ya wanafunzi wenzako watauliza maswali kuihusu.

Why Should We Worship God in Love and Truth?

Imekusudiwa kuwavutia Wahindu

Jinsi ya kuitoa: “Sala moja ya Wahindu inayojulikana sana inatia ndani ombi la kupata ukweli na nuru. Je, unafikiri ni muhimu kumwabudu Mungu katika upendo na kweli? [Mruhusu ajibu.] Ona maneno ya Yesu kuhusu jambo hili.” Soma Yohana 4:24, kisha usome fungu la 4 katika ukurasa wa 3, na umtolee mwenye nyumba broshua.

Jaribu njia hii: Mwenye nyumba akiikubali broshua, sema hivi: “Baadhi ya Wahindu wenye hekima wanasema kwamba ukweli umefichwa katika mioyo yetu. Wengine wanasema kwamba ukweli unapatikana katika maandiko matakatifu. Nitakaporudi, ningependa tuzungumzie swali linalotajwa mwishoni mwa fungu la 3 katika ukurasa wa 4.

The Pathway to Peace and Happiness

Imekusudiwa kuwavutia Wabudha

Jinsi ya kumtolea Mbudha mwenye umri mkubwa broshua hii: “Huenda wewe pia, kama mimi, una wasiwasi kuhusu maoni mengi yaliyopotoka ambayo yanasambaa leo, na jinsi yanavyoathiri watoto wetu. Idadi ya vijana wanaoishi maisha yasiyo ya maadili inaongezeka. Unafikiri sababu ni nini? [Mruhusu ajibu.] Je, unajua kwamba jambo hili lilitabiriwa katika kitabu kilichoanza kuandikwa kabla ya dini ya Uhindu, Uislamu, na Ukristo kuanzishwa? [Soma 2 Timotheo 3:1-3.] Hali zinazotajwa katika andiko hili zinazidi kuwa mbaya ijapokuwa watu wanaendelea kuelimika. [Soma mstari wa 7.] Chapisho hili lilinisaidia kuelewa mambo ambayo watu wengi hawapati kujua kamwe. Je, ungependa kulisoma?”

Jaribu njia hii: Katika ziara ya kurudia, baada ya kuzungumzia habari za Biblia mara kadhaa, mwonyeshe mwenye nyumba maswali katika jalada la nyuma, na sanduku la kuagizia kitabu Biblia Inafundisha. Mwambie kwamba una kitabu hicho katika mkoba wako akitaka kukiona. Mwonyeshe yaliyomo, na mzungumzie fungu moja au mawili katika sura atakayochagua.

Our Problems​—Who Will Help Us Solve Them?

Imekusudiwa kuwavutia Wahindu

Jinsi ya kuitoa: “Watu wengi ambao tumezungumza nao wanahuzunishwa sana na uovu wanaoona ulimwenguni. Je, unafikiri kwamba siku moja Mungu ataondoa matatizo yaliyo katika ulimwengu? [Mruhusu ajibu.] Unabii huu unatupa matumaini. [Soma Zaburi 37:11.] Nimeisoma ahadi hiyo katika Biblia, kitabu ambacho mara nyingi kimeeleweka na kutumiwa vibaya. Huenda ukashangaa kujua kwamba Biblia si kitabu cha Wazungu tu; haiungi mkono ukoloni wala kupendelea jamii moja kuliko nyingine. Hata hivyo, inatupa tumaini kwamba hivi karibuni Mungu atatuondolea matatizo. Pia, ina kanuni ambazo zinaweza kutusaidia kukabili matatizo yanayotupata leo. Broshua hii ina habari nyingi zaidi.”

Jaribu njia hii: Katika ziara ya kurudia, baada ya kuzungumzia habari za Biblia mara kadhaa, mwonyeshe picha zilizomo katika ukurasa wa 4-5 wa kitabu Biblia Inafundisha. Soma angalau moja ya maandiko yaliyonukuliwa na umtolee kitabu.

Je! Ulimwengu Usio na Vita Utakuwako Wakati Wowote?

Imekusudiwa kuwavutia Wayahudi

Jinsi ya kuitoa: “Katika historia yote, wanadamu wameteseka sana kwa sababu ya vita. Unafikiri ni kwa nini vita vinaendelea kuwako ilhali watu husema wanataka amani? [Mruhusu ajibu.] Unabii huu wa Isaya unatupa matumaini. [Soma Isaya 2:4.] Hata hivyo, maswali fulani yanazuka: Unabii wa Isaya utatimia lini na jinsi gani? Kwa nini tunaweza kuamini kwamba Maandiko ndiyo chanzo cha matumaini ya kweli? Broshua hii inajibu maswali hayo.”

Jaribu njia hii: Mwenye nyumba akikubali broshua, mwonyeshe ukurasa wa 16-17, na useme: “Watu wengi hurejelea mambo mabaya kama Maangamizi au Machinjo Makubwa ya enzi ya Wanazi na kuuliza, ‘Ikiwa kuna Mungu, kwa nini anaacha watu wateseke?’ Tunaweza kuzungumzia jambo hilo nitakaporudi.”

Mwongozo Wa Mungu—Njia Yetu ya Kwenda Paradiso

Imekusudiwa kuwavutia Waislamu ambao wanaishi katika maeneo ambapo wana uhuru wa kujifunza Biblia

Jinsi ya kuitoa: “Ninaelewa kwamba Waislamu wanaamini kuna Mungu mmoja tu na vilevile wanawaamini manabii wote. Hilo ni kweli? [Mruhusu ajibu.] Ningependa kuzungumza nawe kuhusu unabii fulani wa kale ambao unatabiri kwamba dunia itafanywa kuwa paradiso. Ungependa nikusomee kile ambacho unabii huo unasema? [Soma Isaya 11:6-9.] Wengi wamejiuliza jinsi ambavyo Mungu ataleta mabadiliko hayo duniani. Broshua hii inaonyesha mambo ambayo manabii walisema kuhusiana na jambo hilo.”

Jaribu njia hii: Mwenye nyumba akiikubali broshua, sema hivi: “Kitabu hiki cha Mungu kinaeleza kwamba mwanzoni, mwanadamu aliishi katika paradiso. Tutakapoonana tena, ningependa kujibu swali hili, ‘Mwanadamu alipuuzaje mwongozo wa Mungu na kupoteza paradiso?’” Utakaporudi, zungumzia mwanzo wa sehemu inayoanza katika ukurasa wa 6.

Imani ya Kweli—Siri ya Kuwa na Maisha Yenye Furaha

Imekusudiwa kuwavutia Waislamu ambao wanaishi katika maeneo ambapo wana uhuru wa kujifunza Biblia

Jinsi ya kuitoa: Mwonyeshe mwenye nyumba picha katika ukurasa wa 16-17, na useme: “Mandhari hii ni tofauti na jinsi ulimwengu ulivyo leo. Unafikiri inawezekana kwamba ulimwengu utakuwa hivi siku moja? [Mruhusu ajibu.] Ona ahadi hii ya kitabu hiki cha Mungu. [Soma katika Biblia yako mojawapo ya maandiko ambayo yamenukuliwa.] Broshua hii inatusaidia kuamini kikweli kwamba ahadi kama hizo zitatimia.”

Jaribu njia hii: Mwishoni mwa ziara ya kwanza, mwombe mwenye nyumba achague mojawapo ya maswali yaliyo katika jalada la nyuma. Fanya mipango ya kurudi ili mzungumzie katika broshua hiyo jibu la swali alilochagua.

Lasting Peace and Happiness—How to Find Them

Imekusudiwa kuwavutia Wachina

Jinsi ya kuitoa: “Leo, kuna matatizo mengi maishani yanayoweza kutukosesha furaha. Ni nini ambacho hukusaidia kuwa na furaha licha ya matatizo? [Mruhusu ajibu.] Watu wengi wamepata furaha kwa kufuata mashauri ya Biblia. [Soma Zaburi 119:1, 2.] Wengi husema kwamba Biblia ni kitabu cha Wazungu tu. Lakini ona jambo hili. [Zungumzia fungu la 16 katika ukurasa wa 17.] Broshua hii inaonyesha jinsi tunavyoweza kupata amani na furaha ya kudumu.”

Jaribu njia hii: Mwenye nyumba akiikubali broshua, someni pamoja sentensi tatu za kwanza za fungu la 18 katika ukurasa wa 17, na useme: “Nitakaporudi, ningependa kukuonyesha mambo tunayoweza kutazamia ambayo yameandikwa katika Biblia.” Utakaporudi, zungumzieni hoja moja katika fungu la 6, ukurasa wa 30.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki